GIAN JUNIOR
Member
- Mar 9, 2011
- 49
- 53
Jamani habarini wana JF.
Niko mbioni kufunga drip irrigation system shambani kwangu. Nimeona niachane na miradi mingine kwanza nikomae na hili. Nataka nilime vitunguu saumu kwa shamba lenye ukubwa wa mita 70 kwa 70).
Maji tayari ninayo nilichimba kwa mtambo (drilling), na kisima kiko hapo hapo shambani. Kwa sasa navuta maji kwa umeme wa Tanesco. Shamba liko tambarare safi. Maji yanapotoka underground yanapanda na kuingia kwenye reserve tank niliyojenga kwa cement.
Nimenunua pampu aina ya Pedrollo kwa ajili ya kutoa maji kwenye reserve tank na kuunga kwenye mfumo wa drip, ila hiyo pampu sijaifunga kwa sasa. Itafanyika wakati wa kufunga drip system. Kwa wazoefu wa kufunga drip, natamani kujua niandae sh ngapi kiuhalisia kwa ajili ya materials, na sh ngapi kwa ajili ya fundi.
Nimeambatanisha picha hapo chini ili kupata ramani halisi kichwani. Hii pampu ya kusukuma maji (Pedrollo) inlet na outlet zake ni upana 1 inch. Je bomba linalofaa kuungwa kwenye drip system ni inch ngapi? Natamani mtu mzoefu kabisa aje anipe details kuliko kusema tu makadirio ambayo yanaweza yasiwe halisi.
Niko mbioni kufunga drip irrigation system shambani kwangu. Nimeona niachane na miradi mingine kwanza nikomae na hili. Nataka nilime vitunguu saumu kwa shamba lenye ukubwa wa mita 70 kwa 70).
Maji tayari ninayo nilichimba kwa mtambo (drilling), na kisima kiko hapo hapo shambani. Kwa sasa navuta maji kwa umeme wa Tanesco. Shamba liko tambarare safi. Maji yanapotoka underground yanapanda na kuingia kwenye reserve tank niliyojenga kwa cement.
Nimenunua pampu aina ya Pedrollo kwa ajili ya kutoa maji kwenye reserve tank na kuunga kwenye mfumo wa drip, ila hiyo pampu sijaifunga kwa sasa. Itafanyika wakati wa kufunga drip system. Kwa wazoefu wa kufunga drip, natamani kujua niandae sh ngapi kiuhalisia kwa ajili ya materials, na sh ngapi kwa ajili ya fundi.
Nimeambatanisha picha hapo chini ili kupata ramani halisi kichwani. Hii pampu ya kusukuma maji (Pedrollo) inlet na outlet zake ni upana 1 inch. Je bomba linalofaa kuungwa kwenye drip system ni inch ngapi? Natamani mtu mzoefu kabisa aje anipe details kuliko kusema tu makadirio ambayo yanaweza yasiwe halisi.