GHANA: Jamaa wachukua mwili wakati ukitaka kuzikwa kisa deni la chumba cha kuhifadhia maiti

Ghazwat

JF-Expert Member
Oct 4, 2015
23,718
66,267
882c22882eb66f75d3882b199ad60579.jpg


Kizaazaa kilitokea wakati wahudumu katika makaburi walitoa mwili katika jeneza na 'kuuteka nyara' kwasababu ya deni.

Kisa hicho cha kushtua kilitokea Accra, Ghana. Iliripotiwa kuwa familia ya marehemu walishindwa kuwalipa wahudumu hao wa chumba cha kuhifadhia maiti waliodai familia hiyo Sh3,000 za Ghana.

Kisa kilianza wakati wanaume wawili wamesimama juu ya jeneza huku mamia ya watu wakiwa wamesimama kutazama kisa hicho.

Wahudumu hao wenye ghadhabu waliwapigia kelele umati huo huku wakiendelea kuutoa mwili huo katika jeneza.

Muda mfupi baadaye, wanaume hao wanaonekana wakibeba mwili huo mabegani! Baadhi ya watazamaji wanajaribu kuongea na wanaume hao ambao kwa hasira wanatumia mwili huo kuwaashiria watu kuondoka.

37c92e6daf4ef2fe2fa1751a09f69116.jpg


Wanaume hao waliondoka nao kabisa bila kujutia hatua yao hiyo. Haikujulikana ikiwa marehemu alizikwa na hao wanaume au waliendelea kumshikilia kwa kutaka kulipwa.

Chanzo: TaifaLeo
 
yaani umati wote huo unazinguliwa na mtu mbili tu?!! huku usukuma hatuwez kukubali huo upuuzi, kutula mikoma duhu
Mbona tunaambiwa kuwa wanaume wa Mikoani ndo waoga balaa...!
 
Imeandikwa: katika nyakati za mwisho watu watapenda sana pesa na kumsahau Mwuumba wao... YANATIMIA: Tujiepushe na laana hiyo..........
 
yaani umati wote huo unazinguliwa na mtu mbili tu?!! huku usukuma hatuwez kukubali huo upuuzi, kutula mikoma duhu
Kweli usukuman kabisa ufanye ujinga kama huu hiyo kitu haiwezekani aisee mikoma lazima itumike wamwise
Tena siyo mikoma tu had mbasa na magembe yatatumika
 
Back
Top Bottom