Gesi kushuka bei kesho

Daah,kweli ukiwa interia mambo ni magumu tuu huku tunanunua 22,000 kwa kilo 6
 
Asante kwa kutujuza mkuu
 
Vizuri, hata hivyo bado bei juu sana ikizingatiwa ges tunavuna wenyewe hapa hapa Tanzania, ilipaswa kwa kg 15 angalau iwe tsh 30,000 na kg 6 tsh 11500.

Nasikia ile gesi ya Mtwara haina uhusiano na hii tunayopikia majumbani, wataalam watufahamishe zaidi
 
Asante sana kwa taarifa, je mamlaka husika zimejipangaje kuhakikisha bidhaa inauzwa kwa bei elekezi katika maeneo yote?
 
Ule mtungi wa kg 15 inatakiwa ishuke hadi 25,000 ndo itakuwa fair, na itaonyesha kweli tunachimba gesi
narudia tena mkuu gesi ya kuchimba haiji leo wala kesho inahitaji mambomengi sana tunayotumia tunatoa nje na wanapakia pale bandarini unaweza pita ukaona matanki yao
 
Shukrani kwa ufafanuzi wa hili jambo. Watu wengi wanapoona mitungi ya gesi wanadhani inatokana na gesi ya Mtwara. Kenya imezuia gesi kuingia nchin kwao kutokea Tanzania na wakati huohuo Kenya nao wana bandari kwahiyo kuna kamchanganyiko hapa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…