Germany Will Return 'Dinosaur' Remains To Tanzania

Germany Will Return 'Dinosaur' Remains To Tanzania

dinosaur huyu aligunduliwa kijiji cha tendaguru mkoani lindi ni moja ya kivutio kikubwa ktk Natural History Museum Berlin nchini Ujerumani.

sosi wikipedia
 
Itafika kipindi na sisi tutaanza kudai tembo wetu arudishwe kwasababu sasa hivi tunawaua kwa kwenda mbele

Wacha watutunzie tu
 
yale mabaki yalikua na single way visa, sasa tusubirie yakishapata return yatakuja. Source..kijiwe cha viroba
 
Ebwanaeeeeh since 1906, karne moja sasa na uchede wa miaka. Labda tusiende mbali sana kuwalaumu viongozi wa sasa ( niulize tu)
Hivi hii kitu hata nyerere aliikalia kimya ??? Usinambie alikua hajui because i'll conclude that, there is no foolish animal than human being
 
Hivi hadi tunalia lia hapa, je malalaimiko yalishapelekwa wizara husika?
 
Hivi hadi tunalia lia hapa, je malalaimiko yalishapelekwa wizara husika?

Not real sure mkuu, ila hii kitu ilishawahi fikishwa bungeni, ilivyopigwa chini kwakeli sikuelewa elewa

.made in mby city.
 
Na Nyie redusheni meli yao MV Liemba maana mnapiga hela hadi leo... Mla huliwa

ni kweli mla huliwa kwani walichukua vingi na pia walifanya vingi jambo la kusikitisha ni kua wakoloni pamoja na ubaya wao walijenga reli wakaleta meli shule hosipitali siwapongezi kwa wizi wao ila miaka 50 hamsini ya uhuru hata nusu ya walivyofanya ingawa hapa sio kwao.
 
Not real sure mkuu, ila hii kitu ilishawahi fikishwa bungeni, ilivyopigwa chini kwakeli sikuelewa elewa

.made in mby city.
Hili jambo anaweza kufikishiwa waziri wa maliasili na utalii akishilikiana na waziri wa mambo ya nje wakalifanyia kazi Mara moja. Vitu vingi sana vinachukuliwa hapa nchini kwa faida ya hao waliobahatika Kuwa ndani ya system ya uongozi wa hii nchi. Utakapopatikana uongozi wa haki nje ya mfumo huu wa kiccm, vitarudishwa vingi hapa na wananchi watabaki midomo wazi kwakushangaa kuwa hata hiki na chenyewe kilichukuliwa?!
 
Hili jambo anaweza kufikishiwa waziri wa maliasili na utalii akishilikiana na waziri wa mambo ya nje wakalifanyia kazi Mara moja. Vitu vingi sana vinachukuliwa hapa nchini kwa faida ya hao waliobahatika Kuwa ndani ya system ya uongozi wa hii nchi. Utakapopatikana uongozi wa haki nje ya mfumo huu wa kiccm, vitarudishwa vingi hapa na wananchi watabaki midomo wazi kwakushangaa kuwa hata hiki na chenyewe kilichukuliwa?!

Unachoongea mkuu ni kweli kabisa, mambo mengi sana tumefichwa utazani sisi wapangaji katika nchi ya kigeni
Kumbe sisi ndio wazawa
Mkuu i can't imagine what will happen finally

.made in mby city.
 
Haya ndo mambo ya kutetea. Kule mjengoni kimya . Wao ni mungano serikali sijui ngapi ngapi, yasokuwa hata maana wanaacha vitu vya uchumi kama hivi.
Nakupongeza sana sana kukumbuka mali ya taifa lako.
Sasa tutazame viongozi wangapi watatetea mali asili kama hizi, wao twiga tu basi

Hahahahaha nicheke mie. Mjengoni kwanza ukilitaja hilo jina la huyo ''mjusi'' mwenye urefu wa mita 12 na uzito wa tani 80 watakuona una kichaa. Wao wamezoea mipasho tu mule. Mambo magumu magumu kama haya, wala hayawahusu
 
Ni afadhali hao Wajerumani ambao walichukua huyo Mjusi enzi hizo watanzania wakiwa hawana elimu wala hawajui lolote enzi hizo za Chifu Mangungo wa Msovero, Usagara. Aidha, Aidha, enzi zile hawakuchukua kutoka Tanzania wala Tanganyika, bali ilikuwa German East Africa, hata hivyo, baada ya uhuru kupatikana wanakiri kabisa kuwa alitoka Tanzania na kwa namna hiyo wanaitangaza Tanzania kiutalii. Vipi kuhusu madini na wanyama ambao waliwaachia lakini sasa hivi mnawatoa kwa nguvu zote !!! Unachukua hatua gani kuzuia mali ya Tanzania inayoondoka sasa hivi ukiwa na elimu na akili ? Itafika wakati mtaanza kuwaomba wawarudishie madini yenu.
 
Twiga wanauzwa mchana kweupe, tembo wanauawa mchana kweupe, halafu mnadai ''Dinasosi'' ambaye hata elimu naye hamna ya kutosha, achilia mbali gharama za kutunza mabaki yake.
 
hiyo mifupa inatakiwa irudishwe tz, itaongeza kipato ktk sekta ya utalii.
 
Katika museum alipowekwa karibia 80% ya vitu vya kihistoria vilivyohifadhiwa vimetoka tanzania.
 
Huyu wa Lindi anatofauti gani na yule wa Rukwa niliyemuona Sabasaba Kwenye banda la Maliasili fupa ni kubwa ajabu kuimagine ukubwa wake ni jambo la kushangaza... ila yasemekana Mifupa ya mnyama mmoja ilipatikana sehemu tofauti tofauti duniani yaelekea Nyama yake iligawanwa kila mmoja aliyebahatika nayo alienda nayo sehemu na nchi yake.. maana lazima kulikuwa na majitu makubwa sana yaliyoweza safiri umbali mkubwa kwa muda mchache kwa mwendo wa kutembea au kupaa
 
Back
Top Bottom