FEBIANI BABUYA
JF-Expert Member
- Mar 5, 2022
- 1,035
- 1,925
- Thread starter
- #421
SAKATA LA UCHAGUZI-PESA KWENYE DAMU (ELECTION SAGA-MONEY IN BLOOD)
INTRO...
Miaka mingi sana iliyokuwa imepita ikiwa ni miaka miwili kabla ya uchaguzi, serikali ya nchi ya Tanzania ilipokea taarifa mbaya kutoka kwa magaidi nchini Kongo kwamba raia wa Tanzania waishio huko wametekwa na ili kuwaachia serikali ilitakiwa kupeleka madini ya kutosha.
Sababu hiyo inamuibua waziri wa ulinzi ambaye anagoma kuhusu kupeleka madini hayo, ndipo anakutana na mkuu wa majeshi na wanakubaliana kukituma kikosi cha makomando SITA ambacho kiliitwa 6.0 (SIX POINT ZERO (hiyo zero iliwekwa kwa sababu maalumu, mwanzo ilikuwa ni 7.0). Makomando hao wanafika Kongo na kufanikiwa kuwaokoa mateka wote, wakawapandisha kwenye ndege huku wao wakiwa karibu na ziwa Tanganyika kusubiri usafiri kwani walikuwa wanafuatwa kupewa msaada ili kutoweka haraka kabla hawajashtukiwa.
Lakini huko Kongo kuna mizigo ambayo waliiokoa pamoja na mateka bila kujua ni mizigo ipi, baadae walikuja kugundua kwamba ni madini.Wakiwa wanajiuliza inakuwaje wanarudi na madini tena? Ndipo wanashangazwa na kinacho tokea.
Ndege ya raia wa Tanzania inatunguliwa ikiwa angani na kulipuka yote.....makomando hao wanashangazwa sana na hilo tukio na ndipo wanashtuka kwamba huenda huko walitumwa kufanya oparesheni nyingine na sio kuokoa watu, hapo wanayakumbuka madini ambayo walisisitizwa warudi nayo na kupewa onyo kwamba wasije wakaangalia ni mzigo gani. Wakiwa kwenye mshangao wa raia wao kulipuliwa wote ndipo msaada ambao ulikuwa umewafuata unafika walipo.
Wanaume ambao waliwafuata hapo hawakuwa kwa ajili ya kuwachukua bali kuwaua. Makomando hao wanakuja kushtuka ikiwa ni TOO LATE hivyo wanapigwa risasi vibaya sana miili yao ikibaki inaelea ziwani tu. Wauaji baada ya kuhakikiki kwamba wamemaliza kazi wanayabeba madini na kutoweka kuyapeleka kwa waheshimiwa walio toa amri ya kazi. Waheshimiwa wanatoa taarifa kwamba MAKOMANDO wamelidhalilisha taifa kwani badala ya kuokoa watu wao wameenda kuua raia wote wa Tanzania kisha wametoroka na madini hivyo wanatakiwa kusakwa popote pale duniani (WANAUME WANAUZIWA MSALA)
Kwa bahati mbaya sana mtoto mmoja wa kishua alikuwa ndani ya nchi ya Kongo kufanya utalii.....anafanikiwa kuuona mwili wa mtu ukielea majini hivyo akatoa amri walinzi wake wautoe na ndipo anagundua kwamba mtu huyo kwa mbali bado anahema, anaamua kuondoka naye na kwenda kwao UGIRIKI na mwili wa huyo komando mmoja ambaye anaitumia miaka miwili kitandani na baada ya kuja kuamka MATATIZO YANAANZIA HAPA. Wakubwa wakijua waliua wote lakini kwa bahati mbaya kuna kiumbe kiliishi. UMWAGAJI WA DAMU NDANI YA TAIFA LA TANZANIA UNAANZIA HAPA bila kujali kwamba ni damu za wenye hatia au wasio na hatia, nchi inachafuka na kuna mambo mabaya sana yanakuja kutokea. Hapa ndipo tunaanza kuzifunua kurasa hizi rasmi;
Baada ya miaka kumi na miwili kupita, Tanzania inapitia kwenye kipindi cha uchaguzi ambapo vigogo watatu wanaanza kuiwania nafasi hiyo kwa udi na Uvumba, wa kwanza alikuwa ni raisi mwenyewe (Huyu hakuna mtu aliyekuwa anamjua sura yake hata wananchi ambao alikuwa anawaongoza) utakuwa unajiuliza inakuwaje raisi aliye ongoza miaka 10 wananchi hawamjui?RELAX, wa pili alikuwa ni wa chama kimoja na raisi ambaye alitaka kumchallenge bosi wake na kutaka atoke Ikulu kwa lazima (huyu alikuja kususiwa IKULU, na alipokuja kugundua sababu ya kususiwa IKULU! Alikuwa amechelewa (TOO LATE).
Wa tatu alikuwa ndiye kipenzi cha Watanzania...huyu wananchi wote walihitaji aingie IKULU kwani walimpenda sana lakini siku chache kabla ya uchaguzi huyu anaye pendwa sana, mwanae mdogo anatekwa. Akiwa amepaniki asubuhi anapatiwa maiti ya mwanae ikiwa haina kichwa. ANACHANGANYIKIWA sana ila kabla hajapoa vizuri jioni mwanae mkubwa wa kike naye anapotea kwenye mazingira ya kutatanisha, anapagawa na kuamua kuibeba bastola yake kisha akaondoka nyumbani.
Alihitaji kwenda kuwabana wapinzani wake kwa kuhisi kwamba ndio ambao walihusika lakini aliishia kupigwa risasi nyingi sana na kupata koma na hapo ndipo simu inapigwa mpaka kwenye ardhi ya MALIKIA. Huko alikuwa anasoma mtoto wa kiume wa mzee huyo, lengo la kumpigia ilikuwa ni kumpa taarifa na kumtaka awe karibu na familia asije kuuawa.
Lakini kurudi kwake kunaibua mambo ya kutisha nchini, alidaiwa kuwa moja kati ya watu hatari sana na alikuwa na makubaliano ya kifo na shirika la kijasusi la MI6 Kwa siri sana ambapo alidaiwa kuhusika kukitengeneza kirusi kimoja hatari sana ambacho kiliishia kwenye mikono ya magaidi ikiwa ni siri ambayo aliishi nayo yeye tu maana familia ilimjua kama mtoto wa mama na hata vyombo vya usalama hivyo ujio wake unakuwa mwanzo mpya wa Tanzania nyingine ya kutisha kwa siri sana.
Unataka kujua kwamba kuna nini humu ndani? Basi ungana nami kwenye andiko hili la SAKATA LA UCHAGUZI-PESA KWENYE DAMU.
Simulizi hii ipo yote mpaka mwisho na unaweza kuipata kwa mfumo wa softcopy kwa bei ya shilingi 5000 tu za kitanzania.
5000 yako tu unapata burudani kubwa sana ya kusoma andiko bora sana hili la kipelelezi likiwa limejikita zaidi kwenye kuichambua SIASA na mambo yake ambayo yapo ndani.
Unaweza kufanya malipo kwa namba hizi.
0621567672
0745982347
Zote jina FEBIANI BABUYA.
Kwenye kalamu ni mimi FEBIANI BABUYA.
Chao
Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
INTRO...
Miaka mingi sana iliyokuwa imepita ikiwa ni miaka miwili kabla ya uchaguzi, serikali ya nchi ya Tanzania ilipokea taarifa mbaya kutoka kwa magaidi nchini Kongo kwamba raia wa Tanzania waishio huko wametekwa na ili kuwaachia serikali ilitakiwa kupeleka madini ya kutosha.
Sababu hiyo inamuibua waziri wa ulinzi ambaye anagoma kuhusu kupeleka madini hayo, ndipo anakutana na mkuu wa majeshi na wanakubaliana kukituma kikosi cha makomando SITA ambacho kiliitwa 6.0 (SIX POINT ZERO (hiyo zero iliwekwa kwa sababu maalumu, mwanzo ilikuwa ni 7.0). Makomando hao wanafika Kongo na kufanikiwa kuwaokoa mateka wote, wakawapandisha kwenye ndege huku wao wakiwa karibu na ziwa Tanganyika kusubiri usafiri kwani walikuwa wanafuatwa kupewa msaada ili kutoweka haraka kabla hawajashtukiwa.
Lakini huko Kongo kuna mizigo ambayo waliiokoa pamoja na mateka bila kujua ni mizigo ipi, baadae walikuja kugundua kwamba ni madini.Wakiwa wanajiuliza inakuwaje wanarudi na madini tena? Ndipo wanashangazwa na kinacho tokea.
Ndege ya raia wa Tanzania inatunguliwa ikiwa angani na kulipuka yote.....makomando hao wanashangazwa sana na hilo tukio na ndipo wanashtuka kwamba huenda huko walitumwa kufanya oparesheni nyingine na sio kuokoa watu, hapo wanayakumbuka madini ambayo walisisitizwa warudi nayo na kupewa onyo kwamba wasije wakaangalia ni mzigo gani. Wakiwa kwenye mshangao wa raia wao kulipuliwa wote ndipo msaada ambao ulikuwa umewafuata unafika walipo.
Wanaume ambao waliwafuata hapo hawakuwa kwa ajili ya kuwachukua bali kuwaua. Makomando hao wanakuja kushtuka ikiwa ni TOO LATE hivyo wanapigwa risasi vibaya sana miili yao ikibaki inaelea ziwani tu. Wauaji baada ya kuhakikiki kwamba wamemaliza kazi wanayabeba madini na kutoweka kuyapeleka kwa waheshimiwa walio toa amri ya kazi. Waheshimiwa wanatoa taarifa kwamba MAKOMANDO wamelidhalilisha taifa kwani badala ya kuokoa watu wao wameenda kuua raia wote wa Tanzania kisha wametoroka na madini hivyo wanatakiwa kusakwa popote pale duniani (WANAUME WANAUZIWA MSALA)
Kwa bahati mbaya sana mtoto mmoja wa kishua alikuwa ndani ya nchi ya Kongo kufanya utalii.....anafanikiwa kuuona mwili wa mtu ukielea majini hivyo akatoa amri walinzi wake wautoe na ndipo anagundua kwamba mtu huyo kwa mbali bado anahema, anaamua kuondoka naye na kwenda kwao UGIRIKI na mwili wa huyo komando mmoja ambaye anaitumia miaka miwili kitandani na baada ya kuja kuamka MATATIZO YANAANZIA HAPA. Wakubwa wakijua waliua wote lakini kwa bahati mbaya kuna kiumbe kiliishi. UMWAGAJI WA DAMU NDANI YA TAIFA LA TANZANIA UNAANZIA HAPA bila kujali kwamba ni damu za wenye hatia au wasio na hatia, nchi inachafuka na kuna mambo mabaya sana yanakuja kutokea. Hapa ndipo tunaanza kuzifunua kurasa hizi rasmi;
Baada ya miaka kumi na miwili kupita, Tanzania inapitia kwenye kipindi cha uchaguzi ambapo vigogo watatu wanaanza kuiwania nafasi hiyo kwa udi na Uvumba, wa kwanza alikuwa ni raisi mwenyewe (Huyu hakuna mtu aliyekuwa anamjua sura yake hata wananchi ambao alikuwa anawaongoza) utakuwa unajiuliza inakuwaje raisi aliye ongoza miaka 10 wananchi hawamjui?RELAX, wa pili alikuwa ni wa chama kimoja na raisi ambaye alitaka kumchallenge bosi wake na kutaka atoke Ikulu kwa lazima (huyu alikuja kususiwa IKULU, na alipokuja kugundua sababu ya kususiwa IKULU! Alikuwa amechelewa (TOO LATE).
Wa tatu alikuwa ndiye kipenzi cha Watanzania...huyu wananchi wote walihitaji aingie IKULU kwani walimpenda sana lakini siku chache kabla ya uchaguzi huyu anaye pendwa sana, mwanae mdogo anatekwa. Akiwa amepaniki asubuhi anapatiwa maiti ya mwanae ikiwa haina kichwa. ANACHANGANYIKIWA sana ila kabla hajapoa vizuri jioni mwanae mkubwa wa kike naye anapotea kwenye mazingira ya kutatanisha, anapagawa na kuamua kuibeba bastola yake kisha akaondoka nyumbani.
Alihitaji kwenda kuwabana wapinzani wake kwa kuhisi kwamba ndio ambao walihusika lakini aliishia kupigwa risasi nyingi sana na kupata koma na hapo ndipo simu inapigwa mpaka kwenye ardhi ya MALIKIA. Huko alikuwa anasoma mtoto wa kiume wa mzee huyo, lengo la kumpigia ilikuwa ni kumpa taarifa na kumtaka awe karibu na familia asije kuuawa.
Lakini kurudi kwake kunaibua mambo ya kutisha nchini, alidaiwa kuwa moja kati ya watu hatari sana na alikuwa na makubaliano ya kifo na shirika la kijasusi la MI6 Kwa siri sana ambapo alidaiwa kuhusika kukitengeneza kirusi kimoja hatari sana ambacho kiliishia kwenye mikono ya magaidi ikiwa ni siri ambayo aliishi nayo yeye tu maana familia ilimjua kama mtoto wa mama na hata vyombo vya usalama hivyo ujio wake unakuwa mwanzo mpya wa Tanzania nyingine ya kutisha kwa siri sana.
Unataka kujua kwamba kuna nini humu ndani? Basi ungana nami kwenye andiko hili la SAKATA LA UCHAGUZI-PESA KWENYE DAMU.
Simulizi hii ipo yote mpaka mwisho na unaweza kuipata kwa mfumo wa softcopy kwa bei ya shilingi 5000 tu za kitanzania.
5000 yako tu unapata burudani kubwa sana ya kusoma andiko bora sana hili la kipelelezi likiwa limejikita zaidi kwenye kuichambua SIASA na mambo yake ambayo yapo ndani.
Unaweza kufanya malipo kwa namba hizi.
0621567672
0745982347
Zote jina FEBIANI BABUYA.
Kwenye kalamu ni mimi FEBIANI BABUYA.
Chao
Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app