Gerald Hando muombe msamaha Dr. Ulimboka

Gerald Hando muombe msamaha Dr. Ulimboka

wewe kidogo maneno yako yanaweza kuipeleka nchi mbele kama utapata supporters... ila nasikitika kuwa wakati wanaJF wakijiita Great thinkers.... wengi wao nina wasiwsi nao maana ninayoyasoma humu si yatokanayo na watu wa aina hiyo. Guys we need bold direction and bold action. sio kutetea madaktari. Hawa wanagoma....yesi ni vizuri....lakini strategy hii si yenye kuleta quick impact kwa walio na serikali. Tayari serikali(viongozi) wanajifaya hawasikii...sasa huwezi kumsikilizisha mbuzi kwa kusema eti ...we mbuzi usile mahindi ya watu hapo...... hawezi kusikia. na hawa serikali hawawezi kusikia....madaktari wakigoma. kwani athari za mgomo haziwagusi wao kwa kuwa hawatumii hospitali hizi. bali tukigoma tunawaua watu wasio na hatia...the 'absolute poor' (which is about 85% of Tz population). Swali ni je tuendelee kugomea kwenda kazini watu wafe wasio na hatia au tubadili 'lugha' ili hao 'mbuzi' wasikie haraka na tuwe tumeokoa maisha ya wananchi?
 
huyu gerald hando, ni mwanamke au ni mwanaume???! mwenye ufahamu anijuze tafadhali! LMAO!
 
Bado mnasikiliza hiyo radio?pole.wanawekaga issue binafusi hata akigombezwa huko mtaani inakuwa story akikamatwa na askali kwa makosa ya barabarani inakuwa kelele mpaka mpinga aje,wajinga sana,wamuombe kipanya arudi aokoe jahazi

Ha ha ha ha,you are right Nyambu hawa Jamaa sometimes wanakuwa ovyo sana,kama muda huu wapo na Kamanda Mpinga na mmojawapo analalamika eti alikuwa anaongea na simu akakamatwa,kweli kuna issue nyingine nyingi tu za radio yao huwa sizikubali lkn ya Hando naungana nayo mkono,amewakilisha kilio cha walio wengi trust me.
 
watangazaji wa clouds fm ni chakula cha ruge, si wanawake tu, mpaka wanaume kama hao kina hando... Kwa hiyo sishangai hando ku-behave like that, ruge ameshawaaribu....
tufiakwa!!!! Najitemea mate kifuani! Kumbeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee!
 
Hizi akili za kuunganishaunganisha taabu kweli. Hivi hata madaktari waki vunja mgomo wao na kurudi kazini hatafu hakuna dawa, vifaa vya kutibia hakuna,wagonjwa wanalala mzungu wa nne na kuambukizana magonjwa ina faida gani?

Kwahiyo afadhali yake ni wagome?,kweli akili za kuungaunga on work!
 
Hakutenda haki kwa nini alifanye personal na Dr. Ulimboka ikiwa anatumia redio na mwenziye hayupo kujitetea? angesubiri apone ili amwite ndo amwambie uso kwa uso. Kwa hili inabidi ajirekebishe huyu Gerald Hando.

Point of correction,yaliyotamkwa yalitamkwa kabla ya yaliyomkuta
 
Nilimsikiliza kwa uzuri sana Gerald Hando kwenye kile kipindi,Hando kama Hando alikuwa anatumia haki yake ya kikatiba kama Mtanzania yeyote wa kawaida isitoshe kilichosemwa na Hando kinaweza kuwakilisha mitazamo ya watu wengi sana including I, myself, ni kwa vile tu hatuna pa kusemea tukasikika na wengi kama Hando,ni lazima tukubali watu wameathirika sana kutokana na hii migomo ya madaktari,kama haukukugusa wewe ksbb una uwezo wa kwenda Hospital kubwa za Private ukafikiri kila mtanzania ana uwezo huo...anyway nisimsemee ngoja aamue mwenyewe kama anafikiri analazimika kuomba radhi kwa maoni yale.
Anselm, mleta mada Frozen ameeleza kwa ufasaha sana ukimsoma vizuri.

Hajakataa Hando kutoa mawazo kama haki yake, na wala hajaonyesha kutetea upande wowote.
Alichokisema ni kuwa vyombo vya habari lazima viwe makini katika kuleta habari. Kumtaja Dr Uliomboka ambaye ni kiongozi wa chama cha Madaktari haikuwa kumtendea haki. Ilikuwa ina maana ya kumtwisha mzigo kama Ulimboka na si mwenyekiti. Hili linaitwa character assassination kama alivyofanya Rais kuhusu sifa za Ulimboka pale Diamond

Hata kama baadhi hawakubaliani na Dr Uliomboka chama cha madaktari kinamkubali kama kiongozi wao,
na hivyo anastahili heshima kama kiongozi. Kauli za Ulimboka kuhusu masuala ya chama ni kauli za madaktari.
Kwa mantiki hiyo licha ya kumtwisha mzigo wa chama, Hando amewadhalilisha madaktari kupitia Dr Uli.

Hando kama mwandishi anapaswa kuelewa kuwa kuna mipaka, kanuni na taratibu za kuongea, kuongelea jambo na kulijadili. Radio ni chombo chenye nguvu na kimetumiwa vibaya sehemu nyingine na kuleta madhara.

Kama tutampa haki ya kikatiba isiyo na taaluma, maadili, sheria na mipaka ipo siku hango ataleta uchonganishi au madhara makubwa sana. Kuwa na mdomo pekee siyo sababu ya kuwa na haki za kuleta sintofahamu katika jamii.

Mwisho, taaluma ya habari nchini ina matatizo sana hasa ukisikiliza redio na kusoma magazeti.
Ni lazima jambo lifanyike kwasababu ilivyo sasa ni kama tumewakabidhi vichaa marungu! Let us be honest!
 
Mwenye njaa ni wewe ***** kwani hujui ulisemalo.ukichunguza vzri hata hela ya kutibiwa private hauna ila unajishebedua Kama tui zito la nazi likiandaliwa kuwa Mafuta ya kupaka.
 
Nilimsikiliza kwa uzuri sana Gerald Hando kwenye kile kipindi,Hando kama Hando alikuwa anatumia haki yake ya kikatiba kama Mtanzania yeyote wa kawaida isitoshe kilichosemwa na Hando kinaweza kuwakilisha mitazamo ya watu wengi sana including I, myself, ni kwa vile tu hatuna pa kusemea tukasikika na wengi kama Hando,ni lazima tukubali watu wameathirika sana kutokana na hii migomo ya madaktari,kama haukukugusa wewe ksbb una uwezo wa kwenda Hospital kubwa za Private ukafikiri kila mtanzania ana uwezo huo...anyway nisimsemee ngoja aamue mwenyewe kama anafikiri analazimika kuomba radhi kwa maoni yale.

..... I believe in equality for everyone, except reporters and photographers. Mahatma Gandhi
 
Kati ya lowasa na sumaye nani msitaafu na nan aliyejiuzuru
mshana naomba jibu au warudshe shule wafanyakaz wako
 
Jamani mwenye chake nu Serikali Madaktari wangeacha kabisa kz sio kung'ang'ania humo Hospitalini km hawamheshimu mwajiri
Msamamo wa G.Hando na mwajiri vinaendana allichosema Hando ni sahihi kwani Dr toka mwanzo si mwajiriwa wa Serikali msimtumie kisiasa mtamuumiza
 
simtetei Hando lakini ana haki ya kutoa mawazo kama mtu mwingine yeyote kulingana na alivyoguswa au alivyoathirika na tukio husika, ila kitu kimoja ambacho namshauri mdogo wangu Jerald kama wachangiaji wengine wlivyochangia radio ni sehemu ya kuwa makini sana ki matamshi sijui alikuwa na umri gani wa kuelewa matukio mwaka 1994 wakati wa tukio la mauwaji ya halaiki kule kwa rafiki yangu Kagame au kama anajuwa linalomkabili mtangazaji mmoja wa kituo cha radio kule Kenya anayekabiliwa na mashitaka kwenye mahakama kule kwa bwana Okampo Uholanzi (aliyekuwa mwendesha mashitaka mkuu) hivi sasa yuko mwafrica mwenzetu ingawa watu walio wengi wanadhani kaingia mwafrica hivyo yaliyokuwa yanajitokeza wakati wa Okampo ya kuwashitaki waafrica wenzetu tu kwa wingi yatapungua kama si kuondoka wanasahau kinachoongoza ni utaratibu uliowekwa na si kwamba yalikuwa ni maamuzi ya Ruise Moreno Okampo ok tuachane na hilo mana yangu ni kumpa baadhi ya mifano ya yaliyowakuta wanahabari wenzake kufuatia matamshi yao kwenye radio walizokuwa ama wakiziongoza au kuzifanyia kazi HANDO mdogo wangu una uhuru wa kuongea lakini angalia sana nini unakiongea wewe unasikilizwa na umma lakini unapendwa na umma huo huo unachokifanya ni hamasisho usishangae labda yaliyomkuta Dr. Uli inawezekana yalisababishwa na uliyokuwa ukisema namalizia kwa kusema haya ni maoni yangu
 
kimsingi kinachowasumbua watangazaji wa hii radio ni weledi wao duni na usemi usemao always watch ****** are doing and do the opposite
 
Madaktar kazen buti mpak kieleweke. Tena huyo hando akija anaumwa mumdunge sindan ya virus vya ukimwi
 
hamna shaka kwa namna moja au nyingine kupigwa na kutekwa kwa dokta ulimboka kunatokana maneno ya kuhamsha na kuchochea hasira kwa dkt ulimboka yaliyofanywa na kituo cha radio cha clouds fm ktk kipindi cha power breakfast,segment ya jicho la ngombe majuzi,bwana gerald hando kwa makusudi au kwa kutokujua impact ya radio kwenye kurusha maneno ya chuki na kumkosoa mtu tena kwa kumuita jina lake moja kwa moja bila kufikiria reactions na response za watu kwa mtu husika. bwana hando alimsema sana bwana dkt ulimboka kwamba anapenda sifa, umaarufu,anatakuwa shujua ili sanamu lake liwekwe muhimbili..na maneno mengi ya ajabu ajabu, ambayo mtu yeyote ambaye ameguswa na mgomo wa madaktari angeweza fanya kitu chochote kumdhuru dkt ulimboka. Gerald hando na watangazaji wa radio clouds fm kuweni makini na lugha zenu, acheni unafiki, kumbukeni hata kama mnadhani hakuna watu wanaoweza kuwachukulieni hatua , hasira za watu na malalamiko yao kwenu personaly si jambo jema, wote tunajua mambo ya hovyo yanayofanywa na serikali, na hata serikali kama inashindwa tatua maombi ya madaktari kwa wakati mmoja. waonyeshe tu commitment ya dhati ya kutatua kero za madaktari tusingekuwa na migomo hii, plz gerald hando , angalia maneno yako brother , radio ni very powerful too , inaweza kuwa very destructive isipotumiwa kwa weredi

Kama ni kweli Gerald Hando kasema hayo basi ametumia Uhuru wake wa maoni lakini usio na uwiano katika mpaka, bila shaka ameingilia uhuru wa mwenzake pia. Ikumbukwe kuwa serikali na madaktari walishakubaliana mambo ya kutekeleza (yote na sio baadhi), kama wametekeleza nusu bila shaka ni khiyana kwa mtu mliyekubaliana. serikali haina pa kuchomokea kwa hili. Hebu chukulia mmekubaliana mambo ya msingi na mdau mwenzako anakutaka usahau mengine kwa kuwa katekeleza baadhi, ukikubali tu, atakudharau. Madaktari wana weledi na taaluma yao, wakikutibu wanakutibu kikamilifu hawakupi matibabu nusunusu. Hivyo, wanasiasa wamezowea longolongo na bahati mbaya wanadeal na wanasayansi: mziki wake lazima uwe mzito.
Wito: Gerald atumie uhuru wake bila kuathiri uhuru wa watu wengine wasio na fursa ya kutumia media kama yeye!
 
Yatakukuta subiri....
Hando hajakosea na aliyempa kichapo hando hakufanya makosa, unajuwa ni maelfu mangapi ya wagonjwa wanaoteseka kwa fitna zake. Akipona tumuone aendelee na ufataani wake.
 
Yatakukuta subiri....

Yamenikuta makubwa sana kuliko ya huyo Mnafik.

Ndugu, jamaa, marafiki, watoto, wanawake, wazee, vijana wasio na hatia, roho zao na maumivu yao yamewekwa rehani na madaktari wachache wasio na huruma wala kujali. Roho inaniuma na uchungu mkali sana nnaosikia kila nnapowafiria hao wagonjwa walio kwenye huu mtihani.

Bahati yao sana hao madaktari wanafanya kazi Tanzania, ingekuwa nje ya Tanzania hao saa hizi raia wameshawachukulia hatua za kinidhamu.
 
Back
Top Bottom