<br />Sawa sawa si mke wa yule kijana mtoto wa yule mzee wa kiarusha anayekaa kibanda maziwa sakina. Pia hata watoto wake ambao huwatumia kwenye huduma mh! Hawana ushuhuda kabisa kuna yule mkubwa Niki a.k.a Nisher kulikuwa na post yake ktk jamii photos ka usher wa bongo. Hivi kuhusu wasaidizi wake waliohama na watu na kwenda kufungua huduma zao vp? Kuna mmoja anaitwa Channel yuko kisongo mbele ya Ngurumo kidogo mwezi wa 12 nilikuwa kansani kwake ktk mahubiri yake alidai kuna majambazi na wachawi toka Ngurumo ya Upako walitaka kumuua duh! Dini bana siku hizi ka siasa. Tumwachie Mungu tu, ila tutawatambua kwa matunda yao
<br />
<br />kweli ndugu,jamaa aliyevunjiwa ndoa ni ndugu yangu kabisa na mkewe anaitwa pamela.geo davie anaiishi nae km wake vile.huwa najiuliza,ni mtumishi gani wa mungu anaefanya mambo ya ivi wakati anajua huyu mwanamke ana mume tena wa ndoa na watoto watatu?mpaka leo sijapata jibu
Nabii GeorDavie ni mtumishi wa Mungu na huduma yake ipo Arusha Kisongo na ni Kilomita 13 kutoka mjini Arusha njia ya kwenda Dodoma na ni baada ya uwanja wa ndege tu. Huduma yake inaitwa "Ngurumo Ya Upako" na ni kati ya watumishi wa Mungu ambao wana Upako wa kipekee amabo umekuwa gumzo kwa watu wengi. Mungu ana njia nyingi sana ya kujidhihirisha kwa wanadamu na kama wakati wa zamani za kale aliwatumia watu mbali mbali kwa namna tofauti na hivyo hivyo kwa Nabii GeorDavie.
Kitu kinachonishangaza ni vile watumishi wa Mungu wanasakamwa kila kona! Ni kama watu wote walioandika wana uadui na huyu mtu! Ina maana huyu jamaa hajawahi kufanya jema hata moja! Ni kama yeye kuwa Mtumishi wa Mungu kimekera sana watu. Yeye ni mwanadamu tu kwani yeye ni Mungu! Watumishi wote, Mungu anawatumia kama punda au lorry! hivyo yeye kuanguka au kusimama hakuwahusu! Ikiwa anamwakilisha Mungu, wagonjwa wanapona, Mapepo yanatimuka, wachawi wanatupa vibuyu, watu wanafanikiwa na Mungu anainuliwa shida iko wapi! Msimwangalie mtumishi mwangalieni Mungu! Shida watu hawaamini kama Mungu anaponya wamezoea waganga hivyo wamemweka Mungu chini na kumwinua shetani. Hivi shetani anaponya?
Mapepo yangekimbia? wachawi wangejisalimisha? kwa kweli mimi ninatamani kumwona huyu jamaa kama kwa Jina la Yesu mambo makuu yanatokea huyu ndio mganga ninayemtaka kwani hakuna mganga kama Yesu Kristo. Nimemfuatilia sana huyu mtu ndio maana nimeandika yote haya! Mengi mliyoandika ni uongo mtupu, mpaka jina lake, ametokea wapi, cheo chake, mambo anayoyafanya, hilo limenihakikishia wengi hawamjui na wengi hapa ni maadui wanachafua kazi anayoifanya.
Tangu lini adui yako akakusifia! au akakusema vizuri! Kama haumwamini achana naye! Acha wale wanaoamini wakamwabudu Mungu na kupokea miujiza yao. Kweli wivu ni mbaya mlitaka awagawie hizo sadaka? Jamani Mungu akimwinua mtu kubalini!!! Mnafikiri Mungu amelala haoni yeye??? angeacha watu wote wapotee?? tena kwa taarifa yenu lol! watu wamejaa full j2 nilienda kuchungulia na ndio kwanza wanazidi kwenda!!! Hawa watumishi wanaojiona wema na wananguvu za Mungu si waombe ache basi! Mwacheni komandoo wa Yesu apige kazi kama mmeshindwa kuruka kwa ungo mseme!!
Wajameni Mimi ninamfahamu Nabii GeorDavie vilivyo! Mimi ni mtumishi ninayempenda Yesu kupita maelezo na nimekombolewa kwa damu ya YESU!! Ninataka niwatoe duku duku zenu. Maswali yote niulizeni nitawajibu moja baada ya lingine! Ila kwa wale wenye chuki binafsi, wivu na waongo na wale wanaoamini shetani ana nguvu kuliko Mungu nisingependa kupoteza muda!
Ila wale wanaohitaji kweli kufahamu kwa kina kuhusu Mhe. Nabii GeorDavie niko tayari kuwaelezeni! Ninakaribisha maswali yenu. Imenishangaza sana jinsi mwanadamu anavyoweza kutunga uongo kisa tu ameona tunguri zake zikishindwa kufanya kazi. Wanadamu maisha haya yanapita tujipange sawasawa!
Ni nani anayemjua vyema huyu ndugu?
Nasikia ni Nabii
je huduma yake ipo wapi ?
<br />inaonekana we ni ndugu yangu hatujuani. aliye vunjiwawa ndoa ni ndugu yangu sakina kibanda maziwa,saiv jama yetu ana mke mchungaji from kenya au sio mwanangu
Duh hii kali naona Mtume na Nabii GeorDavie katumia staili ya Nape wote mnatetea ujinga mmejiunga tarehe 30 - 31 / 08 / 2011 mshindwe na mlegee Mtume na Nabii wenu ni mpinga kristo tena ni Nabii wa uongo na uovu.
Eti kuna mtu alimnyang'anya mke....Huyo anayedai alichukuliwa mke alikuwa wapi??? watu wengine wakipata wake wazuri kazi kuwapiga ovyo na kuwatesa...mwanamke ameamua kujishika kisawasawa na Mungu wake. oooh nimenyang'anywa!!! alifikiri mke ni kibega!! ulipokuwa unampiga na kumchoma moto na kumpeleka police ulifikiri ni mtumwa!!!!
Mkamate Mungu wako kisawasawa mama!!! acha waseme mpaka wafe!!! Tena huyo jamaa asipotubu cha moto atakiona manake Mungu huwa anaangalia penye haki. Hivi GeorDavie ni mtu wa kumchukua mke wa Mtu??? kwa taarifa yake hakunyang'anywa na GeorDavie alinyang'anywa na Mungu...ajifunze jinsi ya kumtunza mwanamke, kumhudumia na kumpenda kwa dhati, Haoni hata aibu??!!! Mwanamke ni almas baba! sifa ya mwanamke ni abembelezwe!!
Kama ameshajifunza vya kutosha amwombe Mungu amrudishie mke wake. Watu wanaongea na kumsema mtu wa Mungu vibaya wakati hawajui ukweli uko wapi! Kwa hiyo alikuwa anampiga akifikiri kwa kuwa anamjua Mungu ataacha kuondoka au ataacha kusali. Tena ninamshauri huyo mwanamke asije akaondoka kwenye hiyo huduma hata angemrudia huyo mume!
Mkamate Yesu mama wa Upako!!! Simama Imara, kishujaa maneno yasikurudishi nyuma. walitaka wakukute kwenye nyumba ya mganga wa kienyeji. Sugua goti mama sijawahi kumwona aliyemkimbilia Mungu akiaibika!