Mshangazi mdogomdogo
Member
- Sep 23, 2024
- 73
- 73
Kuna tukio limetokea huku kwetu Kijiji cha Msonga Kata ya Runzewe, Wilaya ya Bukombe Mkoani Geita, kama tutaendelea kubaki kimya hakuna kitakachofanyika na hatua hazitachukuliwa.
Kuna kijana amepoteza maisha kwa kupigwa risasi na Askari wa Hifadhi ya Hifadhi ya Msitu Kigosi ambayo inasimamiwa na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS), tukio limetokea jana saa kumi na mbili asubuhi, tarehe 13 Agosti 2025.
Vijana watani walikuwa ndani ya hifadhi hiyo wakikata miti kwa ajili ya mbao, ndipo wakatokea Askari hao wa hifadhi, vijana wakaamua kukimbia, mmoja wao aliyetambulika kwa jina la Eziboni ile anapiga hatua kukimbia askari hao wa hifadhi wakafyatua risasi ambayo ilimpiga kwa nyuma na kutokea kwenye kitovu.
Wakati wanakimbia ndugu wa Eziboni akaona tukio lote akaamua kugeuza na kwenda mwenyewe kwa hao askari na kuwaambia “Mmepiga ndugu yangu akiwa hana silaha wala madhara yoyote kwenu, niueni na mimi tu.”
Wale askari wakashangaa na kuanza kuogopa wakawa wanamgeuzageuza kijana aliyepigwa risasi baadaye wakambeba kumuweka kivulini, kisha wakamwambia yule ndugu yake kuwa aende akawaite ndugu zake wamchukue mwenzao kumpeleka hospitali kwa kuwa alikuwa bado hajakata kauli.
Wakati akigalagala pale chini Eziboni alikuwa akiwaambia wale Askari “Mnaniua ndugu zangu na sijawafanya lolote, mnaniua, mnaniua” huku akilia kwa uchungu.
Yule ndugu yake alivyoondoka kwenda kutoa taarifa nyumbani, waliporudi ili kumchukua mwenzao hawakuwakuta wale Askari na walikuta mwenzao ameshakata kauli.
Wakaubeba mwili hadi nyumbani kisha wakatoa taarifa Polisi ambapo walifika na kuuchukua mwili kuupeleka Hospitali.
Polisi wamewaambia ndugu wa marehemu kuwa wanaufanyia uchunguzi mwili kisha waende kuuchukua leo Tarehe 14, 2025, ndugu wamegoma kwa kuwa wanataka haki itendeke kwa waliohusika na mauaji ya ndugu yao.
Kijana huyo aliyefariki alikuwa na umri wa miaka 20+ kinachotokea wale askari wa Hifadhi wameingia mitini na hakuna mamlaka inayohusika kuchukua hatua kwa kuwa wanawaona ndugu wa marehemu hawajui chochote kuhusu masuala ya sheria.
Nimeandika kama raia mwema ambaye nimefika katika Kijiji hicho ili hatua zichukuliwe haraka, TFS nao watoe majibu na kuchukua hatua kuhusu tukio hilo.
TFS WAULIZWA KUHUSU TUKIO HILO
Meneja Uhusiano wa Wakala wa Mistu Tanzania (TFS), Johary Kachwamba alipoulizwa kuhusu hoja hiyo ya Mwanachama wa JamiiForums.com amesema:
“Tumepata taarifa kuhusu tukio hilo, Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya inatarajiwa kuwa na kikao muda sio mrefu leo hii (Agosti 14, 2025) wanatarajiwa kujadili kuhusu hilo ili kubaini kama lina ukweli au la na pia kuna taratibu za ndani zinaenda, hivyo, kukiwa na taarifa zaidi tutatoa mrejesho.”
Tamko la Jeshi la Polisi ~ Geita: Askari wanne wa Jeshi la Uhifadhi wakamatwa kwa tuhuma za mauaji
Kuna kijana amepoteza maisha kwa kupigwa risasi na Askari wa Hifadhi ya Hifadhi ya Msitu Kigosi ambayo inasimamiwa na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS), tukio limetokea jana saa kumi na mbili asubuhi, tarehe 13 Agosti 2025.
Vijana watani walikuwa ndani ya hifadhi hiyo wakikata miti kwa ajili ya mbao, ndipo wakatokea Askari hao wa hifadhi, vijana wakaamua kukimbia, mmoja wao aliyetambulika kwa jina la Eziboni ile anapiga hatua kukimbia askari hao wa hifadhi wakafyatua risasi ambayo ilimpiga kwa nyuma na kutokea kwenye kitovu.
Wakati wanakimbia ndugu wa Eziboni akaona tukio lote akaamua kugeuza na kwenda mwenyewe kwa hao askari na kuwaambia “Mmepiga ndugu yangu akiwa hana silaha wala madhara yoyote kwenu, niueni na mimi tu.”
Wale askari wakashangaa na kuanza kuogopa wakawa wanamgeuzageuza kijana aliyepigwa risasi baadaye wakambeba kumuweka kivulini, kisha wakamwambia yule ndugu yake kuwa aende akawaite ndugu zake wamchukue mwenzao kumpeleka hospitali kwa kuwa alikuwa bado hajakata kauli.
Wakati akigalagala pale chini Eziboni alikuwa akiwaambia wale Askari “Mnaniua ndugu zangu na sijawafanya lolote, mnaniua, mnaniua” huku akilia kwa uchungu.
Yule ndugu yake alivyoondoka kwenda kutoa taarifa nyumbani, waliporudi ili kumchukua mwenzao hawakuwakuta wale Askari na walikuta mwenzao ameshakata kauli.
Wakaubeba mwili hadi nyumbani kisha wakatoa taarifa Polisi ambapo walifika na kuuchukua mwili kuupeleka Hospitali.
Polisi wamewaambia ndugu wa marehemu kuwa wanaufanyia uchunguzi mwili kisha waende kuuchukua leo Tarehe 14, 2025, ndugu wamegoma kwa kuwa wanataka haki itendeke kwa waliohusika na mauaji ya ndugu yao.
Kijana huyo aliyefariki alikuwa na umri wa miaka 20+ kinachotokea wale askari wa Hifadhi wameingia mitini na hakuna mamlaka inayohusika kuchukua hatua kwa kuwa wanawaona ndugu wa marehemu hawajui chochote kuhusu masuala ya sheria.
Nimeandika kama raia mwema ambaye nimefika katika Kijiji hicho ili hatua zichukuliwe haraka, TFS nao watoe majibu na kuchukua hatua kuhusu tukio hilo.
================
TFS WAULIZWA KUHUSU TUKIO HILO
Meneja Uhusiano wa Wakala wa Mistu Tanzania (TFS), Johary Kachwamba alipoulizwa kuhusu hoja hiyo ya Mwanachama wa JamiiForums.com amesema:
“Tumepata taarifa kuhusu tukio hilo, Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya inatarajiwa kuwa na kikao muda sio mrefu leo hii (Agosti 14, 2025) wanatarajiwa kujadili kuhusu hilo ili kubaini kama lina ukweli au la na pia kuna taratibu za ndani zinaenda, hivyo, kukiwa na taarifa zaidi tutatoa mrejesho.”
Tamko la Jeshi la Polisi ~ Geita: Askari wanne wa Jeshi la Uhifadhi wakamatwa kwa tuhuma za mauaji