Gazeti RAI laishambulia CHADEMA

Gazeti RAI laishambulia CHADEMA

Udaku gani Rai wameandika? Hivi kuandika Chadema wamepata viti 5 ndio udaku?

Hawa jamaa vichekesho kweli. Eti tusubiri 2015! Sasa dalili ya vua si ni mawingu? Kama kwenye viti 29 wanapata 17% ilikuwa wakae chini wajiulize. Au watatoa wapiga kura Kenya?!
 
Serikali tunaomba mtupatie haki yetu ya kupata habari,lifungulieni Mwanahalisi) kwa nini mnatuonea?
 
M4C nimeiona inavyofanya kazi mikoani mpaka ulaya matunda yake tumeyaona imezaa kata 3.

Kumbe unakiri...imezaa kata 3 ...au kwa lugha nyingine CCM imenyanganywa kata 3.Kalaghabaho.
 
Siku zote ukikubali kusifiwa basi ukubali pia na kukashifiwa. Zote ni sehemu ya maisha.

lakin kwa upande wa habari, unapewa nafasi kujibu hoja hizo na kutolewa kwa wananchi kujua ukweli upo wapi na si kujificha chooni na kulalama.
 
Kada Maarufu Wa CCM Prince Bagenda ameanza Rasimi Kazi ya Kuua chadema na kumujenga Lowasa.
Waandishi wote Wenye mwelekeo wa Kuunga mkono Mageuzi wameminywa na amewaleta Waandishi wa zamani kutoka gazeti la Taifa Tanzania lilikuwa linamlinda Nazir Karamagi.

Mpango huu una andaliwa kutumia gazt La TAZAMA , Sauti Huru kwa malengo ya kulinda Mtandao Wa Lowasa

Waandishi walipangwa kwenye mkakati huo ni pamoja na

1.Brayceson Kayungilo aliyekuwa Taifa Tanzania
2.Julius Mapunda Kutoka TAZAMA
3.Esbon Kagya Kutoka Taifa Tanzania


Ukiangalia gazeti la RAI leo mtandao huo umeonyesha Uandishi wa Chuki na Ushabiki wa Kisiasa wenye lengo la kupotosha umma na Kumulinda Lowassa
 
-Hao jamaa huwa wanafanya propaganda za kizamani sana
Naamini turnover ya kampuni ni negative kwa kufanya kazi kwa hasara

Siku hizi wameshajua CHADEMA ndiyo habari ya mjini ni lazima watumie siku nzima kutafuta headline inayogusa chadema.Ni turn over boosting strategy
 
CDM WALIKUWA wanajitangaza kwa ajili ya kukijenga chama kwa ajili ya 2015.pia gazeti lingebainisha ni shilingi ngapi kila chama kimetumia.huwezi ukasema wapinzani wanapoteza pesa bure kwenye kampen kama za udiwan.wao ndiyo shughuli yao kuu,kujinadi.wanaopoteza pesa bure ni chama tawala ambao walitakiwa kutumia pesa hiyo kutekeleza ilani yao ya uchaguzi
 
Nimelinunua gazeti la Rai, na nimelisoma lote lakini sijaona sehemu yoyote limeishambulia Chadema. Rai limeandika Chadema wamepata viti 5 vya Udiwani, CCM wamepata viti 22 vya Udiwani...sasa hapo kuna kosa gani.

hehehe.. mkuu pro cdm hawataki kusikia habari yoyote mbaya kuhusu CDM hata kama ni ukweli..
 
Gazeti la RAI limeshambulia vikali chama cha CDM kwa kile lilichodai kufuja pesa ovyo kwa operesheni M4C huku chama hicho kikishindwa vibaya kwenye uchaguzi wa madiwani.
Gazeti hilo limedai matokeo hayo ya Chadema hayaridhishi kabisa wananchi ikilinganishwa na nguvu kubwa iliyotumiwa na chama hicho.
Matokeo ya udiwani yanaonyesha mgawanyo wa viti ulikuwa CCM 22 CDM 5 TLP 1 CUF 1.Hata hivyo CDM ikifanikiwa kurejesha viti vyake 2 huku ikiinyanganya CCM viti 3.

Kuchukua viti 3 vya CCm ni mafanikio tosha kabisa.

Hapo wakusikitika ni CCM ambao wamenyanganywa viti 3. Na endapo wakiendelea hivi CDM mwaka 2015 watapata viti vingi sana.



MIZAMBWA
NABII MTARAJIWA!!!
 
Gazeti la RAI limeshambulia vikali chama cha CDM kwa kile lilichodai kufuja pesa ovyo kwa operesheni M4C huku chama hicho kikishindwa vibaya kwenye uchaguzi wa madiwani.
Gazeti hilo limedai matokeo hayo ya Chadema hayaridhishi kabisa wananchi ikilinganishwa na nguvu kubwa iliyotumiwa na chama hicho.
Matokeo ya udiwani yanaonyesha mgawanyo wa viti ulikuwa CCM 22 CDM 5 TLP 1 CUF 1.Hata hivyo CDM ikifanikiwa kurejesha viti vyake 2 huku ikiinyanganya CCM viti 3.

My Take:
Gazeti la RAI miezi iliyopita lilikuwa limeanza kurudu katika ramani yake kwa kutoa habari bila upendeleo lakini tangu Prince Bagenda aajiriwe kama Mhariri Mkuu amekuwa na chuki kubwa dhidi ya chama cha CDM na habari za gazeti hilo kila wiki zimekuwa zikikishambulia vikali chama hicho.Pia tangu Bagenda aajiriwe kumekuwa na makala maalum kila wiki za kushambulia viongozi wa chama hicho hasa Mkiti Freeman Mbowe n Katibu Mkuu Dr Wilbroad Slaa.Hata hivyo soko la gazeti hilo kwa sasa tangu aajiriwe Bagenda limeporomoka vibaya sana.

Dawa ndogo tu; kutolinunua. MIMI NILISHALIGUNDUA NA SITAMANI HATA KULISOMA, KAMA NILIVYOISUSIA TBC
 
Kwani tatizo liko wapi ..si limeandikwa ukweli mtupu... Jinsi cdm inavyojinadi na ilivyofanya kampeni chini ya mbowe na babu slaa haikustahili matokeo hayo... Ni jibu jepesi tu kuwa cdm bado hakikubaliki katika tz kipo moshi arusha na mwanza kidogo... Na ukweli kuwa cdm inawafuasi wa mikutano haina wapiga kura
 
Hata mimi si mnunuzi wa gazeti hili toka limemilikiwa na Rostam Aziz kutoka mikononi mwa Jenerali Ulimwengu & Co.
Lakini ni lazima twende mbele na turudi nyuma kidogo. Si kila kinachozungumzwa negative kuhusu CDM ni kibaya kweli. Negativity nyingine ni sehemu ya kujenga. Huwezi kuwa na taasisi Malaika isiyokosea au kuhitaji kukosolewa. Hii habari haiwezi kuwa shambulio.

Tunaweza tukabeza habari hii ya gazeti la RAI lakini principally unapoendesha project lazima uzingatie uwiano wa input na output. Kilichofanywa na gazeti la RAI ni kupima mambo hayo. Sasa kinachotakiwa kufanywa na CDM ni kukanusha kwa kuegemea mizania hiyohiyo ya INPUT na OUTPUT. Sasa suala linahojiwa na RAI ni Je Input ya CDM kwenye chaguzi hizo za udiwani inaona na output? Hapo ndipo pa kuanzia kujadili na kupatolea ufafanuzi.

Tukianza kushambulia gazeti bila kuona mantiki ya kilichoandikwa tutakuwa tunakosea sana na huko si kukisaidia chama.

heri yako umekuwa makini na wa unesha umma we umekomaa kifikira si mtu wa kukurupuka na kuropoka big up. Tunaiangalia input na out put kaka umeeleweka. Walopokaji achanana nao
 
Hivi kumbe bado linauzwa,Ndio kwanza na jua leo.I think limejifia.
 
Hata kama ukitumia HCL ACID & NITRIC ACID huwezi kumtakatisha huyu, anamagamba magamba magumu sana.
 
fmpiganaji, hili gazeti haliwezi hata siku moja kuiandika vizuri CDM kwa sababu ndio waliomfanya bosi wao ajiuzuru ubunge wa Igunga. Lakini pia 'Profesa' J. aliimba "ili nifanikiwe ninahitaji marafiki, ili nifanikiwe zaidi nahitaji maadui. Maadui wa CDM wamekuwa wakitoa mchango mkubwa sana (japo bila kulitambua hilo). M4C inatesa watu wengi sana, kwa kuona haraka unaweza kuona kuwa haijafanya kitu, ila kiukweli kuna kitu kikubwa sana kimefanyika, Vijana ambao bado wamenyimwa haki yao ya kupiga kura ni wangapi katika hizo kata, uandikishaji ulifanyika 2010. Siumizwi na wakala wa NYINYIEM (RAI) ila ni kuongeza umakini ktk M4C inayofuata.

Akili kubwa sana hizi,naunga mkono hoja mia kwa mia...huwezi kuwa na shilingi mia ukaporwa thelathini halafu ukaenda mtaani ukipiga kelele kwa majigambo kama zuzu lazima utakuwa mwehu tu....M4C ni kiboko yao na bado itawanyuka sana.
 
Rai,Mwananchi,Jamhuri yote hayana hoja hayana tofauti na kiu na sani na ijumaa udaku mtupu.
 
Back
Top Bottom