Sijakuelewa Mkuu! Nini hasa hakijakufurahisha? Kuonesha picha za majeruhi? Au kuonesha majeruhi wakiwa wamelazwa kwenye gororo moja?
Gazeti hili limetoa picha za majeruhi wa mabomu Mbagala ukurasa wa mbele wakiwa wamelazwa chini wawili wawili kwenye godoro moja.
Binafsi sijafurahishwa na picha hizo likiwa ni gazeti la chama tawala lisingeonyesha picha hizo.
Wengine mnasemaje?
wacha unafiki sasa wewe unataka ukweli ufichwe ?
Siyo kwamba ukweli ufichwe kwani nani hajui kuwa watu wengi wamedhurika, na si lazima utangazie watu wote hata wapita njia , zingewekwa basi hata ndani siyo front page!!!!!!!!
kwani gazeti la chama ndio nini? Ule si ukweli?gazeti hili limetoa picha za majeruhi wa mabomu mbagala ukurasa wa mbele wakiwa wamelazwa chini wawili wawili kwenye godoro moja.
Binafsi sijafurahishwa na picha hizo likiwa ni gazeti la chama tawala lisingeonyesha picha hizo.
Wengine mnasemaje?
Mhariri akificha ukweli hamtaki akiweka ukweli hamtaki,mnataka nini sasa? Nenda Amana Hospital, wagonjwa wanalala wangapi kitanda kimoja?
Siyo kwamba ukweli ufichwe kwani nani hajui kuwa watu wengi wamedhurika, na si lazima utangazie watu wote hata wapita njia , zingewekwa basi hata ndani siyo front page!!!!!!!!
Hata kurasa za ndani haitakiwi bila idhini yao.
Hii kawaida ya kuonyesha wagonjwa katika hali waliyonayo wamelala chini na vikanga havitoshi kuwasitiri kikamilifu ni kuwadhalilisha na kuvunja maadili ya siri za mgonjwa.