Gazeti la Uhuru: Tamati ya CHADEMA imefikia

Gazeti la Uhuru: Tamati ya CHADEMA imefikia

Verified

Senior Member
Joined
Apr 11, 2013
Posts
118
Reaction score
385
Gazeti la leo la Uhuru lina habari kuu isemayo tamati ya CHADEMA imefikia. Na sub heading inasema "viongozi wa juu kung'olewa".

Hii habari sio ya kusoma juu kwa juu, inahitaji tafakari kuielewa.

Kwa kifupi ni kwamba, yanayoendelea chadema kwa sasa ni mwendelezo wa nadharia ambazo CCM imepanga kuzitekeleza ili kuhakikisha CHADEMA inakufa kama ilivyonukuliwa na viongozi wa juu wa CCM akiwemo Wassira.

Baada ya nadharia kadhaa kufail zikiwemo za udini na ugaidi ni wazi kwamba CHADEMA wasipokuwa makini round hii chama kinakufa kweli kama CCM walivyopanga. Hii ni kwa sababu CCM wametenga hela nyingi sana kuhakikisha wanawaweka watu wao kwenye uongozi wa CHADEMA na ndio maana baadhi ya viongozi wa Chadema wanashirikiana na CCM kwa hali na mali kutaka kuuondoa uongozi wa CHADEMA.

Hii inamaanisha.. CCM wanajua fika kwamba iwapo tu, Mbowe na Slaa wakiachia ngazi.. basi kama CHADEMA haitakufa, basi wasahau 2015 kuitwa hata Chama kikuu cha upinzani.

My take:
Huu ndio muda mwafaka wa CHADEMA kuhakikisha wanawavua uongozi pamoja na uanachama viongozi wote wanaoonekana kupata backup kutoka CCM akiwemo zito na mwigamba.
Vinginevyo... naanza kuamini maneno ya Wassira.
 
Hyo mikakati CDM wameshaitambua siku nyingi ndio maana wako makini sana na wanajitahidi kufwatilia nyendo za baadhi ya viongozi ambao wamekua au wamehisiwa kukivuruga chama. Mathalan viongozi kama kina Mwigamba Zitto wanatumika sana kukihujumu chama. Pia kuna matatizo ya uongozi pale Shinyanga napo tunapashughulikia kwani wamekua hawana ushirikiano wao kwa wao. Tutahakikisha chama kinakua kisafi na kinaongozwa na wenye maadili.
 
Ccm watasubiri sana...Chama ndo kwanza kinachanja mbuga kama faru...Uzuri ni kwamba ubaya wa ccm pamoja na mapandikizi yao huwa yanastukiwa mapema....Tulianza na Mungu na tutamaliza na Mungu..
 
Baada ya viongozi wa CHADEMA kumshushia kipigo aliekuwa Mwenyekiti wa CDM mkoani Arusha,SAMSON MWIGAMBA hali imezidi kuwa tete na viongozi waandamizi ndani ya chama hicho wamesema muda wa kusambaratika umewadia.

Pia wamesema Ubabe na Kunajisiwa kwa Katiba na Demokrasia ndani ya chama hicho kamwe hakuwezi kukinusuru zaidi ya kuongeza kasi ya kukitafuna.

Mwigamba ambae anatajwa kuwa "Muhimili"Mkubwa na "Muhimu" ndani ya Chama hicho mkoani Arusha,alishambuliwa na viongozi wenzake na walinzi wa Red Brigade kwa madai ya kuwa msaliti, huku kiongozi mmoja akidaiwa kumtolea BASTOLA!!

CHANZO;GAZETI LA UHURU.
 
Day dreaming!
Ujinga na usaliti ndani ya CDM utashughulikiwa mapema kabisa kama hivi ilivyofanyika kwa huyu mwenyekiti. Uzuri wa CDM ni kuwa imewekeza kwenye technolojia na wote wasaliti watakamatika tu.
Kama unaota kusambaratika kwa CDM KUPITIA KUONDOSHWA KWA HUYU MWENYEKITI, UNAJIDANGANYA. Chama imara lazima kibaki na wanachama waaminifu. Nina hakika CDM ITAZIDI KUPAA kwa kuwaadabisha namna hii wasaliti. Tena uchungzi uwe advanced ili kuwabaini mapema.
 
Source: Gazeti la Uhuru!???

Sokoinei umekuja kuwaje mkuu?

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
 
Huoni aibu kutetea uongo na uovu unaofanywa na mbowe na slaa au na wewe ni mnufaika wa huo uozo ushindwe na ulegee.
 
Uhuru wangekua makini wasingeandika bali wangetekeleza mpango wao kimya kimya
Ben kinachokufa kinajulikana kijana mwenzangu ni vema taratibu za misiba mkaziandaa chama cha kupigana kwenye vikao hakiwezi kudumu.
 
Hama cha ukoo kitafia kwenye ukoo husika tusubiri makubwa tuone.
 
nyie hizo siasa bhana hacha wapigane watajua wenyew sis tuangalie maish ya mtanzania yanakwendaje na katiba pia inampa haki gani that iz
 
Ben kinachokufa kinajulikana kijana mwenzangu ni vema taratibu za misiba mkaziandaa chama cha kupigana kwenye vikao hakiwezi kudumu.

Pole sana. Ila tambua chama ni watu sasa angalia viongozi wa ccm wanavyodondoka kila siku mara diwani mara mwenyekiti wilaya katibu tawi mara mkoa hapo jua chama kinakufa.
 
Mwigamba kuongea na waandishi wa habari leo jumatatu, aahidi kusema uozo wote wa CHADEMA. STAY TUNED!
 
cc.m mbinu yao imegundukaaaa hii nchi iko chini ya utawala wa ccm so inabidi tuwe makini wanachama kwa kila linalotokea
 
Baada ya viongozi wa CHADEMA kumshushia kipigo aliekuwa Mwenyekiti wa CDM mkoani Arusha,SAMSON MWIGAMBA hali imezidi kuwa tete na viongozi waandamizi ndani ya chama hicho wamesema muda wa kusambaratika umewadia.

Pia wamesema Ubabe na Kunajisiwa kwa Katiba na Demokrasia ndani ya chama hicho kamwe hakuwezi kukinusuru zaidi ya kuongeza kasi ya kukitafuna.

Mwigamba ambae anatajwa kuwa "Muhimili"Mkubwa na "Muhimu" ndani ya Chama hicho mkoani Arusha,alishambuliwa na viongozi wenzake na walinzi wa Red Brigade kwa madai ya kuwa msaliti, huku kiongozi mmoja akidaiwa kumtolea BASTOLA!!

CHANZO;GAZETI LA UHURU.


Kuna majina JK aliyatumia 'kumsifia' Lisu pindi anatoa hotuba ya mwezi jana kuhusu katiba. nikikumbuka nikusifia nawe
 
Back
Top Bottom