MTZ 255Dar
JF-Expert Member
- Sep 25, 2018
- 1,114
- 3,769
Wanajeshi wa Israel wakiwa kwenye vifaru wameiteka barabara kuu inayounganisha GAZA kusini na GAZA kaskazini. Wachambuzi wa masuala ya kisiasa wanasema kwamba jambo hilo litaifanya Israel kuugawa mji wa GAZA katika kipande cha Kusini na Kaskazini. Israel imevamia mji wa Gaza Kupitia Kaskazini ambapo raia wote wa Gaza waliamuliwa kuhamia upande wa Kusini ambao unapakana na Misri.
Wiki mbili zilizopita, Majeshi ya Israel yaliwataka raia wote waishio upande wa Kaskazini mwa GAZA kuhamia kusini kwa ajili ya usalama wao. Upande wa Kaskazini mwa Gaza ndio mji mkuu wa GAZA unapatikana. Amri hiyo ya Israel iliwalazimu Wapalestina zaidi ya Laki 6 kutii onyo hilo la kuhamia kusini licha ya Wapiganaji wa HAMAS kuwataka raia hao kupuuza agizo hilo.
Video kadhaa zinaonesha vifaru vya Israel vikishambulia magari ya Kiraia ambayo yalikiuka agizo la kuondoka, zaidi ya watu 28 wamekufa baada ya Kifaru kufyatua makombora kuelekea kwenye magari ya Kiraia ambayo yalikuwa yanataka kupita kwenye barabara hiyo kuelekea kusini.
Jeshi la Israel, IDF kupitia msemaji wake limewapa masaa 24 raia waliopo ndani ya mji mkuu wa GAZA kuondoka kabla ya Oparesheni kabambe ya kuusafisha mji huo na kuwasaka Mateka wa Israel. Wapiganaji wa HAMAS walipambana na wanajeshi wa Israel kabla ya kutelekeza Silaha zao na kukimbia.
Heavy clashes reported as Israeli armoured vehicles cut Salah al-Din Street in the middle of the Gaza City governorate. Heavy clashes as Israeli tanks briefly reach Gaza City outskirts
Wiki mbili zilizopita, Majeshi ya Israel yaliwataka raia wote waishio upande wa Kaskazini mwa GAZA kuhamia kusini kwa ajili ya usalama wao. Upande wa Kaskazini mwa Gaza ndio mji mkuu wa GAZA unapatikana. Amri hiyo ya Israel iliwalazimu Wapalestina zaidi ya Laki 6 kutii onyo hilo la kuhamia kusini licha ya Wapiganaji wa HAMAS kuwataka raia hao kupuuza agizo hilo.
Video kadhaa zinaonesha vifaru vya Israel vikishambulia magari ya Kiraia ambayo yalikiuka agizo la kuondoka, zaidi ya watu 28 wamekufa baada ya Kifaru kufyatua makombora kuelekea kwenye magari ya Kiraia ambayo yalikuwa yanataka kupita kwenye barabara hiyo kuelekea kusini.
Jeshi la Israel, IDF kupitia msemaji wake limewapa masaa 24 raia waliopo ndani ya mji mkuu wa GAZA kuondoka kabla ya Oparesheni kabambe ya kuusafisha mji huo na kuwasaka Mateka wa Israel. Wapiganaji wa HAMAS walipambana na wanajeshi wa Israel kabla ya kutelekeza Silaha zao na kukimbia.
Heavy clashes reported as Israeli armoured vehicles cut Salah al-Din Street in the middle of the Gaza City governorate. Heavy clashes as Israeli tanks briefly reach Gaza City outskirts