Huruma anza kwanza kujionea wewe mwenyewe. Nadhani unatafuta bwana au unadhani ukijibu posts zangu utapanda chat. Sasa ni hivi, kuanzia sasa nakujibu inch by inch ili usijiweke kati ya wenye werevu. Douche bag.
Kwanza huwezi ukawakusanya 'Waarabu' wote na kuwaweka kundi moja na kusema eti 'waliwasaida Waafrika'. Kuna waarabu waovu vilevile kila mahali. Kuna wengine hadi leo hii wanaendesha biashara ya utumwa, kuna wengine waliwahifadhi maafisa wa Nazi, wengine wananyanyasa labourers, wengine wanaua Waafrika kule Darfur etc etc. Hivo cut the crap na u-bandwagon wako kwa waarabu.
Pili nimekupa ushauri wa bure hapo, badala ya kupaza sauti yako kama kichaa kwa watu ambao unajua fika hawahusiki na kadhia hii ungefanya la maana ukahamishia makazi yako Gaza, tukakuona wa maana. Bila ya hivo utaendeleea kuonekana kichaa tu na ndio maana nazidi kukupuuza kadr muda unavozidi kwenda.
Tatu, utandawazi kwangu haujatafsiriwa akilini mwangu kama u-bandwagon. Wewe endelea na ubandwagon wako ambao unaona ndio utandawazi. I have better things to do ktk maisha yangu badala ya kujihangaisha na maisha ya watu wasonihusu.
Abdulhalim ktk post #138 aandika :
"I have better things to do ktk maisha yangu badala ya kujihangaisha na maisha ya watu wasonihusu."
Neno wasionihusu ndilo lililoniingia, na neno hili amelirudia mara nyingi katika post zake zilizopita. Ah! siwezi kumshauri vinginevyo kwani Abdulhalim ni mmoja kati ya wale wasemao yanayotokea IKULU- Dar mimi hayanihusu, au mimi ni mfanyabiashara siwezi kuzungumzia siasa. Lakini inapopandishwa kodi nami nikaanza kufuatwa fuatwa ndio naanza kulia lia.
Bei ya mafuta inapopanda kutokana na vita vya Iraq au wasi wasi wa mashariki ya kati ndio ninipojua kuwa hata mimi wa Magomeni yanihusu.
Pengine hata mauaji ya Albino hayakuhusu kwa vile huna ndugu hata mmoja ambaye ni Albino, .....EGOIST.
Vizuri, huko nyuma nilidhani nakufahamu, kumbe nilikufahamu nusu, sasa hivi sura yako iko wazi na JF nzima yakufahamu kwa uwazi kabisa. Sasa hivi si tu kuwa nakuonea huruma bali nakupa POLE.
uNAKUJA NA MPYA za DaRFUR na ukaruka ruka bila kujua uliposimamia. Sikiliza ndugu yangu, hakuna Taifa hata moja utakaowakosa wahalifu. Kwa hiyo hakuna hata sehemu moja katika post zangu nilipoandika juu ya usafi wa Waarabu. Hapa sote tumezingatia suala la ukandamizaji wa Waisrael dhidi ya Wapalestine. Hapa ndipo tulipo, unakojitahidi kunipeleka hutaniingiza ukitaka fungua Thread mpya tujadili mambo ya Darfur na kwingineko.
Ushauri wako si wabure, ni ghali mno sijui kama hujui mahesabu, Pole tena.
Mwisho si lazima uwe GAZA tu ndio unaweza kushiriki katika kuwapinga Waisrael na kuwasaidia Wapalestina. Kuna njia Tatu ambazo binafsi nafanya katika kuwapinga Waisrael:
1. Kutonunua bidhaa zozote zile zitokazo Israel.
2. Kutoa mchango wa Pesa kwa Organisation ambazo zinahusika moja kwa moja katika kutoa misaada huko Gaza.
3. Kuwaelimisha watu kama wewe na wengine wanaodhani kuwa wanapouana nje ya nchi yangu, mimi hayanihusu na ninaweza kunywa chai kwa utulivu. Hivi unajihisi vipi unapoyasikia mauaji ya Rwanda, Burundi au Siera Leon, au ilipotokea Tsunami Thailand n.k. Basi moja kati ya kazi yangu ni kuwarudisha ktk uanadamu na kutoweka tofauti wakati haki za binaadam zinapokiukwa.
Najua ninachokifanya na ninaimani kuwa sisi waafrika ambao nchi zetu zimepata uhuru hivi karibuni ni wawakilishi wazuri wa utatuzi wa migogoro kwa njia ya mazungumzu na si utumiaji nguvu na kusamehe wabaya wetu.