Hili nalo neno...
MGAO WA UMEME...
Uchumi wayumba
* Taifa lapoteza sh. trilioni 1 kwa mwezi
* Hofu yatanda maelfu ya vijana kukosa ajira
* Ukali wa maisha wawaacha Watanzania hoi
* Serikali yang'ang'ania mchezo wa Dowans
MWANDISHI WETU
Dar es Salaam
MGAO wa umeme unaoendelea umesababisha madhara makubwa kwa uchumi wa nchi, huku Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Prof. Benno Ndulu, akiweka bayana kuwa maelfu ya vijana wasio na ajira kwenye miji mikubwa kama Dar es Salaam, Mwanza, Mbeya na Arusha, wanaweza kuiyumbisha taifa.
Wakati makali ya mgao wa umeme yakiendelea, viongozi serikalini wanaonekana kuendelea kucheza 'mchezo mchafu' wa Dowans na kuiona mitambo ya kampuni hiyo tata kuwa suluhisho pekee la tatizo la nishati hapa nchini badala ya kufanya maamuzi mengine ya haraka.
Macho yote ya serikali sasa hivi yako kwenye mitambo ya Dowans ambayo inauwezo wa kuzalisha megawati 100 tu wakati uhaba wa umeme ulipo ni megawati 260.
"Tatizo tulionalo ni kuwa baadhi ya vigogo wa serikali na Bungeni wanatoa msukumo kwa mradi wa Dowans ili kufanikisha uporaji wa pesa za umma," mwanasheria mmoja aliye karibu na serikali ameiambia KuliKoni.
"Eti wanataka taifa liione mitambo ya Dowans kuwa ndiyo mkombozi pekee wa uhaba mkubwa wa nishati nchini. Ukweli ni kuwa hata mitambo ya Dowans ikiwashwa leo, mgao wa umeme bado utaendelea."
Akizungumza kwenye mkutano wa kimataifa wa uwekezaji uliofanyika Dar es Salaam mapema wiki hii, Gavana Ndulu amesema kuwa idadi kubwa ya vijana wasio na ajira kwenye miji mikubwa ya nchi ni tatizo linalo mkosesha usingizi.
"Nina hofu na tabaka linalokuwa kwa kasi kubwa kuliko yote la masikini waliopo kwenye maeneo ya mijini, ambao ni vijana waliokuja kutafuta ajira lakini hawapati hizo ajira," alisema Ndulu.
Katika ripoti yake mpya ya mwelekeo wa uchumi iliyotoka wiki hii (Monetary Policy Statement) Benki Kuu imeonya kuwa tatizo la umeme hapa nchini huenda likaleta madhara makubwa kwa uchumi.
Benki Kuu imesema kuwa italazimika kuchukua hatua kadhaa kuhakikisha kuwa mgao wa umeme na ongezeko la bei ya umeme lilioanza Januari 1 mwaka huu hayaendelei kuleta madhara makubwa kwa uchumi.
Gavana alisema kuwa ingawa lengo la serikali ni kwa uchumi kukua kwa asilimia 7.1 mwaka huu, kuna uwezekano kuwa lengo hilo lisifikiwe kutokana na hofu ya ukame na kupanda kwa bei ya mafuta kwenye soko la dunia.
Kwa mujibu wa Prof. Ndulu, kuna uwezekano ukuaji wa uchumi ukashuka mpaka kufikia asilimia 6.5 mwaka huu kutoka wastani wa ukuaji uchumi wa wasilimia 7.0 mwaka jana.
Baadhi ya viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wanakiri kuwa kundi kubwa la vijana wasio na ajira wanatishia utawala wa serikali.
"Vijana wengi maeneo ya mijini na kwenye vyuo vikuu wanaichukia sana CCM na serikali kutokana na hali ngumu ya uchumi na ukosefu wa ajira. Ndiyo maana wapinzani wameonekana kuwa na nguvu kwenye miji mikubwa hapa nchini," alisema kada mmoja wa CCM.
Hivi karibuni, imetangazwa kuwa zaidi ya viwanda 50 vikubwa nchini vimefungwa huku vingine vingi vikilazimika kupunguza uzalishaji kutokana na makali ya mgao wa umeme unaoendelea.
Hii ina maana kuwa maelfu ya vijana ambao walikuwa wanajipatia ajira kama vibarua kwenye viwanda hivi wameachwa solemba.
Mfanya biashara na mchumi aliyebobea, Ali Mufuruki, ameonya wiki hii kuwa uchumi wa taifa unapoteza shilingi trilioni 1 kwa mwezi tangu mgao wa umeme uanze.
Mufuruki ambaye ni mtendaji mkuu (chairman & CEO) wa kampuni ya uwekezaji ya Infotech Investment Group yenye makao yake makuu jijini Dar es Salaam,
Makali ya maisha yanazidi kuwakamata Watanzania, huku mfumuko wa bei ukiendelea kupaa.
Tayari bei za sukari, mafuta ya taa, mchele, sembe, maharage, mkate, nyama na mahitaji mengine muhimu zimekuwa zikiendelea kuongezeka kwa kasi siku hadi siku.
Wadadisi wa masuala ya kisiasa wamesema kuwa ufisadi serikalini, ukosefu wa ajira na ukali wa maisha vimechangia kwa kiasi kikubwa kukisaidia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kujizolea umaarufu miongoni mwa Watanzania, wengi wao wakiwa ni vijana.
Kutokana na hofu iliyopo serikalini kuwa vijana waliokata tamaa ya maisha wanaweza kuingia mitaani na kutaka kuleta mapinduzi ya wananchi kama yaliyofanyika Misri na kwingineko, Rais Kikwete ameonya kuwa amani ya nchi sasa iko hatarani.
Katika hotuba yake kwa taifa hivi karibuni, Kikwete aliwashutumu viongozi wa CHADEMA kwa kupanga kuindoa serikali yake madarakani kwa kutumia mabavu.
(Source: KULIKONI Toleo la Machi 4, 2011)
MGAO WA UMEME...
Uchumi wayumba
* Taifa lapoteza sh. trilioni 1 kwa mwezi
* Hofu yatanda maelfu ya vijana kukosa ajira
* Ukali wa maisha wawaacha Watanzania hoi
* Serikali yang'ang'ania mchezo wa Dowans
MWANDISHI WETU
Dar es Salaam
MGAO wa umeme unaoendelea umesababisha madhara makubwa kwa uchumi wa nchi, huku Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Prof. Benno Ndulu, akiweka bayana kuwa maelfu ya vijana wasio na ajira kwenye miji mikubwa kama Dar es Salaam, Mwanza, Mbeya na Arusha, wanaweza kuiyumbisha taifa.
Wakati makali ya mgao wa umeme yakiendelea, viongozi serikalini wanaonekana kuendelea kucheza 'mchezo mchafu' wa Dowans na kuiona mitambo ya kampuni hiyo tata kuwa suluhisho pekee la tatizo la nishati hapa nchini badala ya kufanya maamuzi mengine ya haraka.
Macho yote ya serikali sasa hivi yako kwenye mitambo ya Dowans ambayo inauwezo wa kuzalisha megawati 100 tu wakati uhaba wa umeme ulipo ni megawati 260.
"Tatizo tulionalo ni kuwa baadhi ya vigogo wa serikali na Bungeni wanatoa msukumo kwa mradi wa Dowans ili kufanikisha uporaji wa pesa za umma," mwanasheria mmoja aliye karibu na serikali ameiambia KuliKoni.
"Eti wanataka taifa liione mitambo ya Dowans kuwa ndiyo mkombozi pekee wa uhaba mkubwa wa nishati nchini. Ukweli ni kuwa hata mitambo ya Dowans ikiwashwa leo, mgao wa umeme bado utaendelea."
Akizungumza kwenye mkutano wa kimataifa wa uwekezaji uliofanyika Dar es Salaam mapema wiki hii, Gavana Ndulu amesema kuwa idadi kubwa ya vijana wasio na ajira kwenye miji mikubwa ya nchi ni tatizo linalo mkosesha usingizi.
"Nina hofu na tabaka linalokuwa kwa kasi kubwa kuliko yote la masikini waliopo kwenye maeneo ya mijini, ambao ni vijana waliokuja kutafuta ajira lakini hawapati hizo ajira," alisema Ndulu.
Katika ripoti yake mpya ya mwelekeo wa uchumi iliyotoka wiki hii (Monetary Policy Statement) Benki Kuu imeonya kuwa tatizo la umeme hapa nchini huenda likaleta madhara makubwa kwa uchumi.
Benki Kuu imesema kuwa italazimika kuchukua hatua kadhaa kuhakikisha kuwa mgao wa umeme na ongezeko la bei ya umeme lilioanza Januari 1 mwaka huu hayaendelei kuleta madhara makubwa kwa uchumi.
Gavana alisema kuwa ingawa lengo la serikali ni kwa uchumi kukua kwa asilimia 7.1 mwaka huu, kuna uwezekano kuwa lengo hilo lisifikiwe kutokana na hofu ya ukame na kupanda kwa bei ya mafuta kwenye soko la dunia.
Kwa mujibu wa Prof. Ndulu, kuna uwezekano ukuaji wa uchumi ukashuka mpaka kufikia asilimia 6.5 mwaka huu kutoka wastani wa ukuaji uchumi wa wasilimia 7.0 mwaka jana.
Baadhi ya viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wanakiri kuwa kundi kubwa la vijana wasio na ajira wanatishia utawala wa serikali.
"Vijana wengi maeneo ya mijini na kwenye vyuo vikuu wanaichukia sana CCM na serikali kutokana na hali ngumu ya uchumi na ukosefu wa ajira. Ndiyo maana wapinzani wameonekana kuwa na nguvu kwenye miji mikubwa hapa nchini," alisema kada mmoja wa CCM.
Hivi karibuni, imetangazwa kuwa zaidi ya viwanda 50 vikubwa nchini vimefungwa huku vingine vingi vikilazimika kupunguza uzalishaji kutokana na makali ya mgao wa umeme unaoendelea.
Hii ina maana kuwa maelfu ya vijana ambao walikuwa wanajipatia ajira kama vibarua kwenye viwanda hivi wameachwa solemba.
Mfanya biashara na mchumi aliyebobea, Ali Mufuruki, ameonya wiki hii kuwa uchumi wa taifa unapoteza shilingi trilioni 1 kwa mwezi tangu mgao wa umeme uanze.
Mufuruki ambaye ni mtendaji mkuu (chairman & CEO) wa kampuni ya uwekezaji ya Infotech Investment Group yenye makao yake makuu jijini Dar es Salaam,
Makali ya maisha yanazidi kuwakamata Watanzania, huku mfumuko wa bei ukiendelea kupaa.
Tayari bei za sukari, mafuta ya taa, mchele, sembe, maharage, mkate, nyama na mahitaji mengine muhimu zimekuwa zikiendelea kuongezeka kwa kasi siku hadi siku.
Wadadisi wa masuala ya kisiasa wamesema kuwa ufisadi serikalini, ukosefu wa ajira na ukali wa maisha vimechangia kwa kiasi kikubwa kukisaidia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kujizolea umaarufu miongoni mwa Watanzania, wengi wao wakiwa ni vijana.
Kutokana na hofu iliyopo serikalini kuwa vijana waliokata tamaa ya maisha wanaweza kuingia mitaani na kutaka kuleta mapinduzi ya wananchi kama yaliyofanyika Misri na kwingineko, Rais Kikwete ameonya kuwa amani ya nchi sasa iko hatarani.
Katika hotuba yake kwa taifa hivi karibuni, Kikwete aliwashutumu viongozi wa CHADEMA kwa kupanga kuindoa serikali yake madarakani kwa kutumia mabavu.
(Source: KULIKONI Toleo la Machi 4, 2011)