tanira1
JF-Expert Member
- Nov 18, 2011
- 942
- 159
hapo kwenye red umenikumbusha mbali sana mkuu nimekulia moroMwalimu Mkuu,
Wengine hatujaona hilo gazeti, unaonaje ukitupatia summary ya hiyo news, maana najua haliko mtandaoni na hivyo huwezi kutuwekea hapa habari nzima.
Kwenye mazishi nadhani kuna watu wa ubalozi wa Tanzania Washington DC walihudhuria ingawa hakuna aliyeruhusiwa kuona mwili wa marehemu.
Hayo maswala mengine ya kwamba serikali haikufuatilia hospitali aliyokuwa anatibiwa, sidhani kama ni sahihi maana aliugua akiwa Gavana wa Benki Kuu na lazima Benki Kuu ilikuwa inalipa gharama zake na bado aliendelea kupewa mshahara wake kama kawaida na pia hata barua ya kuomba kujiuzuru aliandika akiwa US. So, serikali ilikuwa inajua kila kitu ila haikutaka kuweka wazi may be kwa sababu zao wao wenyewe.
Lakini kuelekea 2015 kuna mengi sana yatafumka ili wale wanaowania kupeperesha bendera ya CCM kuelekea Magogoni waweze kumalizana wao kwa wao. CHADEMA kaeni mkao wa kupewa clues za ufisadi na inawezekana details zote zikawekwa wazi na hivyo unakuwa ni mtaji.
Mukama juzi amelia na Kamati za Bunge kwamba iweje tuhuma zinazojadiliwa kwenye Kamati ya Bunge zifike kwa waandishi wa habari kabla tuhuma hizo hazijafikishwa kwa Spika ili afanye maamuzi kama ziwe discuessed au la. Hatimaye akaropoka kwamba hizi zote ni njama za wanaotaka kuvuliwa magamba. Kwa hiyo joto ndani ya CCM ni kubwa sana na likiendelea hivi Mkapa akae mkao wa kueleweka maana ataumbuka tena na sijui ataficha wapi uso wake.
CCM ina hali mbaya sana kwa kuwa makundi yamekamiana, hata Mukama aliyekuwa anasema kuwa na makundi ni sawa, lakini victim mkubwa ni chama maana siasa za makundi zinaishia kukipaka matope chama chote na pia kuipaka matope serikali. Namna ya kuja kujinasua kutoka kwenye hilo tope itakuwa ngumu sana na mwisho wa siku wote watakosa. Ndugu zangu wa Morogoro wana msemo wa "kazopata", kwamba bora tukose wote maana ukipata utaringa sana na kututambia.