Gavana Balali Ajiuzulu!

JF members.....

hebu tuwekeeni hiyo ripoti muache KURUSHIANA VIJEMBE KAMA KHADIJA KOPA NA NASSMA KHAMIS...........
 
Any update from JK kuhusiana na kujiuzulu kwa Gavana au ripoti ya uchunguzi wa BOT?
 
Wakuu wa kaya na wanakaya ya JF

Cha kushangaza ukisoma ile thread ya ugonjwa wa balali kuna watu wancomplain kuhusu serikali kutotoa taarifa za ugonjwa wa Balali and his wareabout. Mtu/watu huyo huyo au hao hao anasema anayoreport ya ukaguzi BoT lakini hataki kuitoa wazi

Je nyie wote sio mafisadi kama wao(serikali)? Kama tutasema muda muafaka bado, kwa nini tusiamini na serikali inasema muda muafaka bado wa kutoa maradhi ya Balali(hadi kifo kimkute).

Hakuna sababu ya kutambiana tunayo wakati hakuna aliyonayo ili tuweke juhudi za kuipata.

Nawakilisha
 
Jamani taratibuuu, msije kuumbuka kama ile ishu ya.........
 
Mimi binafsi sina tatizo na serikali kufanya ugonjwa au hali ya Gavana siri. Hata hiyo ya kutosema alipo au hospitali aliyolazwa. Ni haki yao na mhusika yaani Gavana mwenyewe. Kinachonistua ni pale balozi anaposema hajui alipo au HALI ya mgonjwa. Angesema kuwa kuwa mahali alipo mgonjwa na hali yake vitaendelea kuwa siri mpaka pale watakapoamua kutueleza nisingeona tatizo. Wengi tunajua kuwa kuna wakati madaktari wanakataza mgonjwa kutembelewa ili aweze kupumzika na hasa ukiangalia tamaduni zetu za kiafrika. Huku kukana kujua aliko na hapohapo kusema kuwa mnamhudumia ni kucomplicate mambo bila sababu.
 
Sidhani kama kuna mtu anayo ripoti hiyo ya BoT na kama yupo basi labda ameiminya kwa makusudi. Vinginevyo, kitakachotolewa kwa Rais ndiyo hicho hicho... Rais anarudi ofisini kwa siku chache wiki ijayo..
 
hii ndiyo tanzania na michezo ya kitoto kwa ishu muhimu.
kwa nini balali afichwe?
kwa nini ripoti iwe siri kiasi hicho?
kwa nini habari kuhusu kujiuzulu kwake iwe siri?
kwa nini ajiuzulu akiwa nje?
je watanzania tuna amana na nchi yetu kweli?? au ndo tumewaachia wachache waisasambue wapendavyo? tena kwa jina la dhamana ya....
 
Ripoti ya BOT imeishia wapi? Au ndio imeshasahaulika!
 
Swali ni alikufa au hakufa?
 
Mzee mzee ....muda unakimbia
 
Dogo siku hizi kimya sana au unatafuna tu mihela
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…