Gari la Mbunge Babalevo T555 EPN halina bima?

Gari la Mbunge Babalevo T555 EPN halina bima?

Nashauri sifa za kuwa/kugombea ubunge zirekebishwe,mbunge angalao awe na elimu ngazi ya degree.
Uchague mgombea mwenye degree au darasa la saba matokeo ni yaleyale...........
Ukweli usiosemwa ni kwamba mbunge hana chochote cha kuwaletea wapiga kura wake zaidi ya kutatua kero ndogo ndogo tu......

Unless jimbo lake likutwe limo ndani ya mikakati au vipaumbele vya kitaifa.
mfano; Ni UONGO mbunge wa Tabora kuwaambia wapigakura wake nimewaletea maji kutoka ziwa Victoria.
Ni UONGO Mbunge wa Dodoma mjini kuwaaminisha Wananchi aliwaboreshea miundombinu.
Ni UONGO kwa mbunge yeyote wa Dar es Salaam kuwaahidi watu atatatua kero ya foleni kwenye eneo lake..
Hakuna Jimbo au wilaya ambalo hela hazipelekwi....isipokuwa mahitaji ni makubwa mno kuliko mgawo ulioletwa majimboni..
Sasa ni ubunifu wako wewe mbunge kuwaaminisha watu wajue kuna kitu ulifanya, iwe ni kweli au porojo.

Ndio maana mbunge kama Baba levo kwa kujua restrictions hizo ameamua kuwa mkweli kwa kutrend na vitu vyepesi vyepesi kama
Pilau la bure, daftari bure, bodaboda za mikataba nafuu,
Kuliko kuwalaghai watu kwa ahadi ngumu ambazo ni ngumu kuzipata hasa kwa kipindi hiki ambacho serikali ina hela za matumizi yake tu, sio za maendeleo.
 
Mfumo ulitakiwa uwe accessed na wasimamia sheria tu. Sio kila mtu ajue status ya gari ya mtu.
Gari kutokuwa na bima nayo ni privacy? Wabongo mnapenda kuficha ficha mambo.
Mfumo ukiwa kwa wasimamizi tu mteja mwenyewe atahakiki vipi kama gari yake ina bima?
 
Huelewi hata privacy ni nini.
Wewe ndio huelewi. Nazungumzia status ya gari kuwa na bima sio privacy ndio maana imeachwa mpaka sasa.yaani hata mimi ukinigonga inabidi nijue gari yako ina bima au haina na ina bima na kampuni gani?.kilichoondolewa ni majina ya mmiliki ambayo yanakidhi kuwa privacy ya mtu.
 
Wewe ndio huelewi. Nazungumzia status ya gari kuwa na bima sio privacy ndio maana imeachwa mpaka sasa.yaani hata mimi ukinigonga inabidi nijue gari yako ina bima au haina na ina bima na kampuni gani?.kilichoondolewa ni majina ya mmiliki ambayo yanakidhi kuwa privacy ya mtu.
Sawa.
 
Umejuaje kwamba haina bima? Kuingiza barabarani uninsured vehicle ni illegal. Mtunga sheria anakuwa wa kwanza kuvunja sheria?
Kabisa hili neno haujaliandika kimakosa?

Kwamba leo baba levo akutungie wewe sheria ya kukuongoza?watu mna utani sana aisee!
 
Back
Top Bottom