Gari inauzwa toyota spacio new model (2002)

Gari inauzwa toyota spacio new model (2002)

Ushauri wangu kwako,ungeweka bei ingekusaidia kutafutwa na wateja wanaotaka kweli...lakini sasa hata mtu anayefanya 'window shopping' atakupigia.

Jambo lingine,jiulize kwa nini mteja aanze kuhangaika kuuliza bei kwa kupiga simu wakati yapo magari kwenye mitandao mbalimbali yenye bei tayari?

Kumbuka wateja wanapenda sana kurahisishiwa na kutumia muda kidogo sana kupata wanachohitaji

Nawasilisha

Kwanza hiyo sio Corolla Spacio new model. New model zinaanza 2003, weka bei acha kuuza kwa mnada.
 
Mark Francis kwani ukisema gari hilo linauzwa 13ml kuna tatizo gani?????

Mtu anapouliza bei ana maana nyingi, kwanza ni comparison. Kivipi????

Nataka kununua gari Bongo kwa labda 13ml Spacio nalingnisha na gharama za kuagiza toka Japan kama beforwad n.k na kisha kupata tofauti na kujiuliza kama ni material difference au immaterial for decision making mkubwa.

Halafu pili unakufahisishia hata wewe kupokea simu za wateja ambao wako na nia kweli mfano umeweka bei mtu akipiga simu anakuambia amepungukiwa kiasi gani kama mnaweza kufanya biashara.

Sasa mtu anakupigia anakuambia ana 6ml kwa hadhi ya gari itakuwa anakuchefua na unaweza kukuta unamjibu vibaya kwa kuhisi kalidharau gari lako kumbe kosa ni lako.

Bei ni muhimu sana japokuw unazunguka zunguka bila sababu za msingi.
 
Last edited by a moderator:
Kwanza hiyo sio Corolla Spacio new model. New model zinaanza 2003, weka bei acha kuuza kwa mnada.

Hiyo gari ni new model maana zipo Spacio za nyuma zaidi ya hiyo. Engine ya hiyo gari lazima ni VVTi mkubwa bila shaka itakuwa ZNE.
 
Mjomba,hata kuweka bei hapa jamvini ni moja ya njia za mawasiliano kama unavyotaka tukupigie simu,au unataka kila mtu umtajie bei yake upige ganji,acha hizo kaka biashara haziendi hivyo,pia ni vema kama ungesema na mileage yake
 
Nyuzi kama hizi ambazo hajitoshelezi ziwe zinafutwa!!🙁
maswali haya tunauliza kila siku ,weka bei ,picha ,na taarifa nyingine kibao!
..utasikia ni PM au piga simu!...****!


Some adverts utashangaaa.... watu wengine wanafanya biashara ya 20 century hapa...

TATIZO MUUZAJI ni dalali ndio maana haweki wazi.... weka wazi tujue...
 
Tatizo lako nn Asprin? Suala sio gari linauzwa nani, suala ni kwamba gari lipo linauzwa na wanunuzi wa kweli wanapiga simu kujua bei. Kwa mtu anaehitaji kununua, hawezi ona hasara kupoteza vocha ya 500/= kwa kitu chenye thamani ya milioni kadhaa.

Afu kama hujui Asprin, show room za kibongo nyingi wanachakachua vifaa original na kuweka vibovu. Njoo ukutane na gari ambayo haimjui fundi wa kibongo ambao huwa wanacheza na spare original za magari ya watu.


mkuu ungerahisha tu kwa kuweka bei! mbona kule kwingine umeweka bei kwanini jf inakuwa ngumu? au sio hii umeitangaza zoom Trucks 2002 Toyota Spacio
Price: TSH 14,000,000
Kilometers: 77182
Transmission: Automatic
Date Listed: Nov 1, 2012

Email Address: Click to Email
Phone: +255 715 101 740
Area: Dar Es Salaam

A car in good condition, it's like new and price is negotiable. For more info, call 0715-101740



2002 Toyota Spacio For Sale in Dar Es Salaam Tanzania | Classified
 
Anakusanya namba za watu huyu, hata mimi nimekutana na hii gari kule zoom! halafu hapa hataki kuweka bei ati mpaka watu wampigie...kwa nini usiseme wakubeep?..utashindwa kupiga kwa mia5 wakati unauza kitu cha millioni kumi?:majani7:
 
Kipofu kaona mwezi eti! Wazugaji utawajua tu. Wenzio tunaweka bei za Hummer jamvini, kuweka bei ya Corolla unaona shida gani?
 
Lazima aringe, soko la magari Tanzania ni red hot, bei hataji na anabembelezwa na kila mtu, kigari chenyewe Spacio, watake wasitake watampigia simu
 
Mark Francis kwani ukisema gari hilo linauzwa 13ml kuna tatizo gani?????

Mtu anapouliza bei ana maana nyingi, kwanza ni comparison. Kivipi????

Nataka kununua gari Bongo kwa labda 13ml Spacio nalingnisha na gharama za kuagiza toka Japan kama beforwad n.k na kisha kupata tofauti na kujiuliza kama ni material difference au immaterial for decision making mkubwa.

Halafu pili unakufahisishia hata wewe kupokea simu za wateja ambao wako na nia kweli mfano umeweka bei mtu akipiga simu anakuambia amepungukiwa kiasi gani kama mnaweza kufanya biashara.

Sasa mtu anakupigia anakuambia ana 6ml kwa hadhi ya gari itakuwa anakuchefua na unaweza kukuta unamjibu vibaya kwa kuhisi kalidharau gari lako kumbe kosa ni lako.

Bei ni muhimu sana japokuw unazunguka zunguka bila sababu za msingi.

Nimekuelewa mkubwa, lakini kwa sasa acha hivyo hivyo ilivyo. Mwenye nia ya kununua atapiga simu na ataelekezwa, afu kumbuka kuwa gari sio bei tu, ni vitu vingi. Mnunuzi atapiga simu kupata bei na maelezo mengine anayohitaji kujua kuhusu gari hilo linalouzwa.
 
mkuu ungerahisha tu kwa kuweka bei! mbona kule kwingine umeweka bei kwanini jf inakuwa ngumu? au sio hii umeitangaza zoom Trucks 2002 Toyota Spacio
Price: TSH 14,000,000
Kilometers: 77182
Transmission: Automatic
Date Listed: Nov 1, 2012

Email Address: Click to Email
Phone: +255 715 101 740
Area: Dar Es Salaam

A car in good condition, it's like new and price is negotiable. For more info, call 0715-101740



2002 Toyota Spacio For Sale in Dar Es Salaam Tanzania | Classified

Nashukuru kwa msaada wako, lakini kumbuka hii ni mitandao tofauti. Huku masihara yamezidi sana tofauti na kule ambapo mtu hawez ku-comment chochote zaid ya kupiga simu na kuuliza
 
Kwanza hiyo sio Corolla Spacio new model. New model zinaanza 2003, weka bei acha kuuza kwa mnada.

Hiyo ni new model kaka, lakn ni second generation ambazo zimetoka kati ya 2001 - 2006, ingawa pia kuna third generation zilizotoka kati ya 2004 - 2009 ambazo ni adimu sana Tanzania. Pia kumbuka Spacio hazizalishwi siku hizi, ila zimetoka nyingne ku-replace hizo ambazo ni Toyota Verso.
 
kaa nalo gari lako. Hujui kufanya biashara kwani inaonesha huna uhakika na bei.
 
mkuu ungerahisha tu kwa kuweka bei! mbona kule kwingine umeweka bei kwanini jf inakuwa ngumu? au sio hii umeitangaza zoom Trucks 2002 Toyota Spacio
Price: TSH 14,000,000
Kilometers: 77182
Transmission: Automatic
Date Listed: Nov 1, 2012

Email Address: Click to Email
Phone: +255 715 101 740
Area: Dar Es Salaam

A car in good condition, it's like new and price is negotiable. For more info, call 0715-101740



2002 Toyota Spacio For Sale in Dar Es Salaam Tanzania | Classified
kweli huwezi danganya watu wote kila wakati na kila kitu "author" nahis alikuwa bob marley
 
kaa nalo gari lako. Hujui kufanya biashara kwani inaonesha huna uhakika na bei.

Mkuu wala sifikili kashindwa kufanya biashara - kuna kitu akija kaa sawa hapa kwa mfano: Angalia kwenye mtandao, kitu wanacho onyesha kwanza ni picha za mbele na nyuma ya gari, alafu ndio unaonyeshwa ndani - sasa ukiangalia kwa umakini hapa utaona sehemu hizo ziko conveniently hidden WHY? Haijasajilwa au nini....!!!!
 
Huyu bwana anaonekana ni mbabaishaji sana ana maneno mengi ambayo hayaoneshi kua yuko serious na biashara hii.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom