Gari inauzwa toyota spacio new model (2002)

Gari inauzwa toyota spacio new model (2002)

Mark Francis

JF-Expert Member
Joined
Nov 19, 2010
Posts
605
Reaction score
310
Gari inauzwa, ni nzuri sana na ipo kama mpya.

AINA YA GARI: TOYOTA SPACIO NEW MODEL
ENGINE SIZE: 1,496 cc
FUEL: Petrol
Year of manufacture: 2002
BEI: TZS 14,000,000 (Negotiable)

Kwa maelezo zaidi, piga namba 0715-101740

Car 2.jpg Car 4.jpg Car 6.jpg
 
au anauza kwa mnada,tuanze sisi kutaja bei,laki moja,mwingine.......
 
Gari liko DSM na limeshasajiliwa, bei piga namba hiyo.
 
Acha nyodo wee dalali weka bei hapa...au unauza gari la shemeji yako?...mbona hujiamini?
Huweki bei huitaji kutuwekea namba na kutuchosha kukupigia bila sababu.

Natumai umetuelewa
 
Ukiona mtu anasita sita kuweka bei ujue lipo tatizo kubwa.
 
Gari liko DSM na limeshasajiliwa, bei piga namba hiyo.

You cant be serious. Kila kitu uweke hadharani isipokuwa bei?

Madalali bana!

Bora mtu ujinyooshee zako show room kuliko kumaliza air time yako eti kuulizia bei tu.
 
You cant be serious. Kila kitu uweke hadharani isipokuwa bei?

Madalali bana!

Bora mtu ujinyooshee zako show room kuliko kumaliza air time yako eti kuulizia bei tu.

Tatizo lako nn Asprin? Suala sio gari linauzwa nani, suala ni kwamba gari lipo linauzwa na wanunuzi wa kweli wanapiga simu kujua bei. Kwa mtu anaehitaji kununua, hawezi ona hasara kupoteza vocha ya 500/= kwa kitu chenye thamani ya milioni kadhaa.

Afu kama hujui Asprin, show room za kibongo nyingi wanachakachua vifaa original na kuweka vibovu. Njoo ukutane na gari ambayo haimjui fundi wa kibongo ambao huwa wanacheza na spare original za magari ya watu.
 
Acha nyodo wee dalali weka bei hapa...au unauza gari la shemeji yako?...mbona hujiamini?
Huweki bei huitaji kutuwekea namba na kutuchosha kukupigia bila sababu.

Natumai umetuelewa

Wanunuzi wa kweli, msibabaishwe na maneno kama haya. Gari ipo katika hali nzuri kabisa, imeagizwa toka Japan na imeshasajiliwa. Ni safi haina hata chembe ya vumbi kwa ndani, bado haijakutana na mafundi wa bongo wachakachuaji.
 
Nyuzi kama hizi ambazo hajitoshelezi ziwe zinafutwa!!🙁
maswali haya tunauliza kila siku ,weka bei ,picha ,na taarifa nyingine kibao!
..utasikia ni PM au piga simu!...****!
 
Wanunuzi wa kweli, msibabaishwe na maneno kama haya. Gari ipo katika hali nzuri kabisa, imeagizwa toka Japan na imeshasajiliwa. Ni safi haina hata chembe ya vumbi kwa ndani, bado haijakutana na mafundi wa bongo wachakachuaji.

Ushauri wangu kwako,ungeweka bei ingekusaidia kutafutwa na wateja wanaotaka kweli...lakini sasa hata mtu anayefanya 'window shopping' atakupigia.

Jambo lingine,jiulize kwa nini mteja aanze kuhangaika kuuliza bei kwa kupiga simu wakati yapo magari kwenye mitandao mbalimbali yenye bei tayari?

Kumbuka wateja wanapenda sana kurahisishiwa na kutumia muda kidogo sana kupata wanachohitaji

Nawasilisha
 
Wanunuzi wa kweli, msibabaishwe na maneno kama haya. Gari ipo katika hali nzuri kabisa, imeagizwa toka Japan na imeshasajiliwa. Ni safi haina hata chembe ya vumbi kwa ndani, bado haijakutana na mafundi wa bongo wachakachuaji.

sasa mtu akilinunua ataliendeshea wapi ambapo hakuna hao mafundi wachakachuaji? Au itabidi ahame aende zake Japan lilipotoka aendeshee huko au vip Mark? Nawaza tu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom