Gari hizi bei gani jamani?

Gari hizi bei gani jamani?

hizi zinapatikana Tanzania, au? iko wapi hii gari
 
Sijui kwa nini hii mvua isitulie kidogo, niko mitaani nimetembelea show room nyingi zilizopo wilaya ya Kinondoni, Ilala na Ubungo, hizi lori za maji washawasha sizioni wajameni.

Sasa hivi niko hapa Kibaki Rd. jamaa ananiambia hizo gari atanifanyia oda maalum kutoka nje. Naona anafungua computa mpakato yake. Naona uso wake umekunjamana na ghafla anazima computa yake.

Ananiuliza maswali mengi ambayo kwangu hayana maana, hitaji langu ni bei wajameni.

Anawasha tena computa yake, ananiuliza unahitaji bei ya lori moja?
Ndiyo lori moja, (namjibu) lakini mahitaji yangu ni kununua malori 777

Sawa mzee, bei ya kuanzia ya kununua, bila ya gharama nyingine za kusafirisha, kodi na ushuru mbalimbali ni US$ 430,000.00 kwa lori moja kwa malori 777 itakugharimu US$ 334,110,000.00

Kwa pesa ya Tanzania 334,110,000 x 2,050 = 684,925,500,000.00

Chungulia gari lenyewe likiwa kazini na mbwembwe zake.

Nipeni bei wajameni ..............

 
ebu jaribu kugugo trade carview au be forward utaona bei zake
 
Wajameni kampuni ya Lithotech Export ndiyo ilishinda tenda ya kununua bvr kit

Hawa pia ndio waliwauzia bvr kit tume ya uchanguzi ya Msumbiji, zikiwa ni pamoja na;

Computer
Camera
Finger print reader
na printer

Oda ya Tanzania na Msumbiji zinafanana kila kitu isipokuwa bei;

Tanzania $ 6,816
Msumbiji $ 4,286

TOFAUTI $ 2,670
 
Wajameni kampuni ya Lithotech Export ndiyo ilishinda tenda ya kununua bvr kit

Hawa pia ndio waliwauzia bvr kit tume ya uchanguzi ya Msumbiji, zikiwa ni pamoja na;

Computer
Camera
Finger print reader
na printer

Oda ya Tanzania na Msumbiji zinafanana kila kitu isipokuwa bei;

Tanzania $ 6,816
Msumbiji $ 4,286

TOFAUTI $ 2,670

Safi sana shamba la bibi!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom