Gamboshi: Makao makuu ya wachawi Kanda ya Ziwa

Kijiji cha Gamboshi, ambacho kwa miongo mingi kimekuwa kikiogopwa kama makao makuu ya wachawi na uchawi wa kutisha.

Kimekuwa ni kijiji kinachotafutwa na watu
wanaotaka utajiri na uongozi kwa njia ya mkato.

Mwandishi wa habari hii amejikuta akipata wakati mgumu kutoka kwa wasakamali na uongozi tangu alipoandika habari za kijiji hicho katika vyombo vya habari.

Haileweki ni vipi watu hao waliweza kupata
namba yake ya simu kwani kati ya March 12 hadi May 28, aliweza kupigiwa simu na
watu 19, na 11 kati ya hao wakitaka awapeleke au awatajie majina ya ‘Wazee’ maarufu watakaowawezesha kufanikisha malengo yao wakati wa uchaguzi mkuu ujao.

Huku 8 waliobaki wakiwa ni wachimba madini ambao wanaamini
wazee wa Gamboshi wanaweza kuwaonesha madini yalipo.

“Nasikia wewe ndiye unawapeleka watu
Gamboshi, tafadhali nisaidie nikawaone ili
waninyoshee mambo yangu. Mimi niko Mererani Arusha,” alisema mmoja wa watu hao katika simu aliyompigia Mwandishi wa habari hii.

Mwingine aliyejitambulisha kuwa ni mkazi wa Dodoma alisema: ” Bwana naomba nisaidie nifike Gamboshi ili wataalam hao wanisaidie katika uchaguzi ujao, kuna jimbo la uchaguzi nalowania".

Kwa mujibu wa wakazi wa kanda ya ziwa, Gamboshi si mahali pa kupakimbilia kwani kijiji hiki kimetajwa kuwa na mengi ya kutisha kiasi cha kuitwa ni ‘jiji
la miujiza’.

Moja ya visa vilivyowahi kuripotiwa na ambavyo viliwaogopesha sana watu ni pamoja na viongozi wa kiserikali na kichama kunyolewa nywele
sehemu za siri, kujikuta wamelazwa nje.

“Gamboshi si mahala pa kutembea kwa sababu ukienda kamwe hutarudi, nawafahamu vema wakazi wa huko si rafiki kabisa na watu wengine,” alinionya Epaphra Swai, mkaguzi wa
viwanda vya kuchambua pamba mkoani Simiyu.

Kijiji hicho ambacho ni nadra sana kutembelewa, kimepata umaaurufu mkubwa ndani na nje ya
nchi kama kama kitovu cha uchawi na
wachawi wanaoweza kufanya miujuza, hali
ambayo imekifanya kijiji hicho kupitwa na
mkondo wa kimaendeleo kitaifa.

Hata hivyo baada ya kukitembelea kijiji hicho, wakazi wake walidai kuwa mengi
mabaya yanayosemwa dhidi yao ni ya kuzusha tu, na chumvi nyingi kuongezwa, hali ambayo imeathiri maendeleo ya kijiji chao.

“Sisi ni wakulima wakarimu wa pamba, mahindi na mpunga. Yote mnayoyasikia kwamba sisi ni magwiji wa uchawi ni uvumi uliotiwa chumvi nyingi. Tunamuomba Rais wetu kwa kushirikiana
na mbunge wetu, Andrew Chenge atusadie
kulisafisha jina letu,” alisihi Zephania Maduhu, afisamtendaji wa kijiji cha Gamboshi.

Maduhu pamoja na wanakijiji wenzake walidai kuwa hofu iliyoenezwa kitaifa na kimataifa juu ya uchawi uliovuka mipaka wa kijiji cha Gamboshi umesababisha madhara makubwa kwa kijiji hicho
kiasi cha kutengwa na jamii yote ya Watanzania.

“Hakuna aliyetembelea kijiji hiki kwa miaka mingi sana. Hata sisi tunapotoka nje ya kijiji wengi hawataki kutusogelea wakiamini
tuwadhuru, ” alisema Musa Deus, 26, mmoja wa wakulima walionufaika sana kilimo cha mkataba kijijini Gamboshi.

Kwa mujibu wa afisa mtendaji,
tangu Uhuru hakuna kiongozi yoyote wa kitaifa aliyewahi kukanyaga kijijini hapo. Mtu wa pekee aliyewahi kuzuru kijijini hapo ni mbunge wa Bariadi Mashariki, Andrew Chenge, ambaye alifika kijijini hapo mwaka 2010 wakati akifanya kampeni
za ubunge.

“Tume ya katiba ilitupita, mwenge wa Uhuru nao haujawahi kupita hapa. Tuko kisiwani mbali na Watanzania wengine,” aliseman afisa mtendaji.

Mijini na vijijini, kumekwepo na ubishani mkali kuhusu ni mkoa gani unaokimiliki kijiji hicho ambacho baadhi ya wakazi wake wanadai kuwa miongoni mwa vioja vyake ni mauzauza yanayoweza kuifanya Gamboshi ionekane kama jiji la New York au London wakati wa usiku.

Wakazi wa Shinyanga wanadai kuwa Gamboshi iko wilayani Magu, mkoa wa Mwanza, wakati wale Mwanza wakidai kuwa iko mkoani Shinyanga.

Kwa mujibu wa afisa mtendaji, Gamboshi iko katika wilaya Bariadi, karibu na mpaka
unaotenganisha na wilaya ya Magu iliyoko
mkoani Mwanza.

“Tunaomba sana ndugu mwandishi waambie Watanzania kuwa mengi wanayoyasikia kuhusu Gamboshi si kweli kabisa, tunawakaribisha wote
hapa waje kufanya biashara na sisi, waoleane na vijana wa Gamboshi kama wafanyavyo katika vijiji vingine. Sisi ni binadamu wema,” alidai mkulima Malimi Kidimi.

Lakini si wananchi tu wanaogopa kufika hapo hata baadhi ya makampuni ya ununuzi wa pamba.

“Kampuni Billlchard, moja ya mawakala wa kilimo cha mkatabaka alishindwa kutuletea mbolea hapa na badala yake akaenda kuibwaga katika kituo cha Polisi Bariadi kwa kile ambacho wafanyakazi wake walidai ni kuhofia usalama
wao,” alidai afisa mtendaji na kulaumu watu.

Wanaoneza hofu hiyo kuwa ina athari kubwa kwa kijiji na watu wake.
Kwa mujibu wa afisa mtendaji si kweli kabisa kila mtu ajaye Gamboshi hupotea moja kwa moja, huuliwa au kugeuzwa nyoka au fisi kama wengi wanavovumisha.

“Pigo tulilopata kutokana sifa mbaya
tuliyobambikiziwa haisemeki ila ni madhara
makubwa tunayapata kutokana na kutengwa na jamii. Wanakijiji wa Gamboshi ni masikini kwa sababu mkondo wa maendeleo na mageuzi umepita mbali sana nao,” alidai mtendaji huyo.

Akifafanua kiini cha chuki na hofu waliyonanayo wananchi juu ya kijiji cha Gamboshi, afisa mtendaji huyo alidai kuwa

"hapo zamani ilitokea
kijana mmoja kutoka kijiji jirani cha Ngasamwa kuwa na mahusiano ya kimapenzi na msichana mzaliwa wa Gamboshi. Siku moja kijana huyo alikuja kijijini hapo akimsandikiza mpenziwe na kisha kushindwa kurudi kijijini mwake. Juhudi za kumsaka kijina huyo hazikuweza kuzaa matunda hadi aliponekana kichakani baada ya siku saba huku ngozi yake imebadilika na kuwa nyeupe.
Alipouliza alifikaje kichakani hapo, kijana huyo alijibu kuwa ameteremshwa na ndege ya JET kutoka Ulaya na baada ya hapo kijana huyo alirukwa na akili kiasi cha kushindwa kuuongea. Ilibidi achukuliwe na kupelekwa kutibiwa na waganga wa jadi na akapona baada ya matibabu ya zaidi ya mwezi mmoja,” alisimulia
afisa huyo, na kudai kuwa, kisa hicho
inawezekana kuwa na ukweli kidogo sana, lakini kuongezwa chumvi nyingi kupita kiasi.

Kwa mujibu wa Maduhu, tangu siku hiyo
Gamboshi ikatangazwa uadui na vijiji vingine kiasi cha kukifanya kuogopwa na kuchukiwa mno.

“Uvumi kama Gamboshi inaweza kuonekana kama Ulaya au Marekani ilianzia hapo na umendelea kurudiwa kwa namna ambayo imekifanya kijiji hiki kiitwe jiji la maajabu,” alidai afisa huyo.

Kwa maoni ya Malimi Kidima, Wana Gamboshi wangeweza kuitangazia dunia kuwa wao ni wasafi lakini, kwa miaka mingi wamekosa jinsi ya kuifanya sauti yao isikike.

“Redio ndiyo njia ya pekee inayotufanya sisi tuwe karibu na dunia. Hakuna mwenye luninga hapa kwa sababu hakuna umeme. Tunasoma magezeti kupitia vichwa vya habari vinavyosomwa kila siku redioni,” alidai Maduhu.
 
Naomba nielekeze jinsi ya kufika na kuwaona wazee wa kijiji cha Gamboshi waninyooshee mambo yangu.

Awamu hii mambo magumu, Gamboshi itanisaidia sana.
 
Habarini wana Jamii Forum,

Kwanza kabisa poleni na majukumu ya kila siku ya kulijenga Taifa letu la Tanzania. Naomba kujuzwa juu ya sifa ambazo nimekuwa nikizisikia juu ya Kijiji cha Gamboshi kuwa ni makao makuu ya wachawi je zinaukweli wowote? na kuna maajabu gani mengine ya ziada yanayopatikana katika Kijiji hicho?

Asanteni.
 
PICHA: Kanisa la RC lilivyozinduliwa ''Ikulu ya Wachawi'' Gamboshi.

Askofu Sangu akila chakula na wananchi wa Gamboshi.

Askofu Sangu akiwa na wanafunzi shule ya msingi Gamboshi
=====================================================
Gamboshi ni kijiji kinachopatika Kata ya Gamboshi wilaya ya Bariadi Mkoani Simiyu ni takribani kilometa 37 kutoka Makao makuu ya Mkoa wa Simiyu, Mjini Bariadi.Gamboshi siyo jina geni sana kwako unayesoma makala hii.

Gambosi kinatambulika kama kijiji ambacho ndiko makao makuu ya wachawi Tanzania “ Ikulu ya wachawi Tanzania” kinaelezwa kuwa ni kijiji chenye maajabu makubwa.

Historia ya kijiji hiki iliyosambaa nchi nzima, ndiyo inaweza kufanya kuwa Gamboshi lisiwe jina geni kwako, kwa bahati mbaya au nzuri historia hiyo imekuwa siyo nzuri hata kidogo.

Kijiji hicho kinatambulika kwa kila mtanzania kuzidi hata jina la wilaya au mkoa.Waandishi wa habari mbalimbali hapa nchini baadhi yao wamefanikiwa kufika katika kijiji hicho na wengine kukwamia njiani.

Waliofanikiwa kufika ndiyo wamesababisha Gamboshi kujulikana kwa kiwango hicho, lakini pia baadhi ya wananchi ambao baadhi yao ni wazawa wamekuwa wakitoa simulizi za kijiji hicho kupitia vyombo vya habari.

Simulizi na habari hizo zinaeleza kuwa kijiji hicho kimejaa mauza uza (miujiza), ukifika usiku Gamboshi inabadilika inaonekana kama mmoja wa mji mkubwa (Cairo), nyumba nyingi zenye ghorofa zaidi ya 50.

“Mchana kijiji hicho kinaonekana kawaida, mandhari yake kawaida kabisa ya kijijini, nyumba za nyasi na fupi, lakini usiku kunabadilika kijiji kinaonekana kama jiji, taa za wakawaka, jiji linalonga’aa” inasema moja ya simulizi.

Kutokana na historia ya Gambosi kuwa ya kutisha na ambayo imesambaa nchi nzima, inaelezwa kuwa toka Tanzania ipate uhuru hakuna kiongozi yeyote wa dini au serikali mkuu ambaye amefika.

Julai 27, 2016 ni siku ambayo wananchi wa kijiji hicho wanapata furaha ambayo inayotajwa kuwa haijawahi kuonekana, ni siku ambayo Askofu wa kanisa Katoliki jimbo la Shinyanga Mhashamu Liberatus Sangu anakanyaga ardhi ya Gamboshi.

Askofu Sangu anafika kijiji hapo kwa ajili ya kuzindua Kanisa Katoliki Kigango cha GambosHi, inaelezwa kuwa kanisa hilo limejengwa kwa nguvu za wananchi wa kijiji hicho, hali inayoshangaza kidogo.

Furaha kubwa ya wananchi wa GambosHi mara baada ya kuwasili kwa kiongozi huyo inaashiria jambo, wanasema haijawahi kutokea Kiongozi mkubwa wa serikali hata dini kufika kijijini hapo.

“Historia mbaya ambayo imekuwa ikituandama imetufanya kuonekana watu ambao siyo watanzania, tunaishi kisiwani, toka tumepata uhuru huyu ndiye kiongozi wa juu wa kwanza kukanyaga hapa Gambosi”, anasema Magreth Magesa

Umati mkubwa wa wananchi wa kijiji hicho pamoja na wanafunzi unafurika kanisani hapo kwa ajili ya kumuona Askofu Sangu, huku wengine wakitamani kumshika hata mkono au nguo zake.

Wakati mwingine Askofu Sangu alijikuta amezungukwa na umati mkubwa wa watu, huku wasaidizi wake wakishindwa kuwazuia kutokana na furaha waliyonayo akiwemo na askofu mwenyewe.


“Haijawahi kutokea hata siku moja, historia imetufanya kuwa watu wanyonge kila sehemu, unapotoka nje ya Gamboshi ukaelekea sehemu nyingine wakati mwingine unalazimika usitaje unapotoka”, anaeleza Paschal Charels.

Wananchi hao wanaeleza kuwa ujio wa kiongonzi huyo ni neema kubwa kwao na unakuwa mwanzo wa kuweza kubadilisha mawazo hasi ya watanzania juu ya kijiji chao ambayo yamedumu vichwani mwao.
Wanabainisha kuwa siyo kweli Gamboshi kuwa ni makao makuu ya wachawi, badala yake wanaeleza hapo zamani zilikuwepo familia mbili ambazo zilikuwa zikishindana kwa uchawi.

Wanaeleza familia hizo ni Mwanamabula na Mwanamakulyu, ambao walikuwa wakishindana kwa uchawi hali ambayo ilikuwa ikiwavutia watu mbalimbali hapa nchini kufika kijijini hapo kwa ajili ya kuchukua dawa.

“ Waliokuwa wakichukua dawa ndiyo waliopeleka habari hizi mbaya kwa watanzania wengine, toka zamani hiyo mpaka leo historia haijafutika, bado watanzania wameendelea kuamini Gambosi ni ikulu ya wachawi” ,anasema Charles.

Bahame Kaliwa ni diwani kata ya Gamboshi aliyeshiriki hafla ya uzinduzi wa kanisa hilo, anasema licha ya umbali kuwa kilometa 37 kutoka mjini Bariadi makao makuu ya mkoa hakuna kiongozi yeyote wa mkoa ambaye amefika Gamboshi.

Bahame alieleza kuwa toka mwaka 2012 mkoa wa Simyu kuanzishwa hakuna mkuu wa mkoa ambaye amefika kijijini hapo, kutokana na historia mbaya inayotangazwa juu ya kijiji chake ndicho chanzo cha viongozi kutofika.

“ Leo ni shangwe kubwa kwetu wanakijiji, ni jambo la kihistoria Baba askofu kufika Gamboshi, hii itafuta historia mbaya inayotuandama toka zamani mpaka leo, ukweli Gamboshi ni sehemu sahihi, tulivu na wananchi wake siyo wachawi bali ni wacha mungu”, anaeleza Kaliwa


Kaliwa anaupongeza uongozi wa dini hiyo kuanzisha kanisa hilo, ambalo alieleza litafuta historia mbaya kwa wananchi wa Gamboshi kwa kutambulisha kuwa ni watu wanaomtegemea mungu na siyo uchawi.

“ Tumekuwa tukiumia na kukerwa kuitwa ikulu ya wachawi, tunataka kuwaambia watanzania kuwa sasa GambosHi na sehemu salama na watu wake wanamtegemea mungu na siyo uchawi kama inavyoelezwa” ,anaeleza Magreth Magesa mkazi wa Gamboshi.

John Mkinga ni Padri parokia ya Ngulyati ambapo Gamboshi ni eneo lake la kazi, anasema ambacho kimekuwa kikiongelewa juu ya kijiji hicho siyo kweli, huku akibainisha kuwa maisha kwa sasa yamebadilika kijijini hapo.

Padri John anabainisha wakati anaanza kazi katika parokia hiyo alipata wakati mgumu kuanzisha kanisa kijijini hapo, baada ya wananchi kumtaka aondoke huku akiulizwa kwa nini yeye ni mnene?.

“ Haikuwa kazi rahisi kufika mpaka hapa, hapa hapakuwepo kanisa bali tulikuwa tunasali chini ya mti (huo hapo), nilianza na waumini 10 tu, nilipofika hapa swali la kwanza niliulizwa na wanakijiji kwa nini nimenenepa?” ,anaeleza

Alibainisha kuwa alitumia mbinu mbalimbali zikiwemo kujumuika nao katika shuguli za maendeleo na burudani, lengo likiwa kutaka kubadilisha mienendo yao na kuanza kumtegemea mungu.

Hata hivyo anasema kuwa aliwashawishi hadi kufanikiwa na kuanza harakati za ujenzi wa kanisa, ambalo alieleza ndilo linazinduliwa na Askofu Sangu, huku likiwa na wahumini zaidi ya 200 kutoka 10.

Katekista Thomas Masenema ndiye kiongozi wa dini wa kanisa hilo, anaeleza kuwa amekuwa akishangaa maelezo yaliyoko mitaani kuwa tofauti sana na maisha ya kijijini hapo.

Anaeleza toka amefika Gamboshi kwa ajili ya kufanya kazi hiyo hajawahi kuona yale ambayo yanaelezwa ikiwemo kijiji hicho kubadilika inapofika nyakati za usiku pamoja na kuwa na wachawi wengi.

“ Niko hapa zaidi ya miaka 3, nafanya kazi vizuri naishi hapa, sijawahi kuona hayo ambayo yanasemwa, Gamboshi ni kijiji kama vijiji vingine, ni kweli uchawi ulikuwa lakini ilikuwa zamani” ,anasema Masenema.

Kutajwa kuwa ni kiongozi wa juu wa dini na wa kwanza kufika Gambosi kunaonekana kumshangaza Askofu Liberatus Sangu, ambapo anaeleza ni historia kubwa kwake na wananchi wa kijiji hicho.

Askofu Sangu anaeleza “ natamani kama ratiba ingelisema nilale hapa, mimi ningelilala, wala siogopi maneno ya watu, furaha yenu niliyoikuta na kuiona toka nimefika inanifanya nijiulizwe maswali mengi”

Anasema kuwa hali hiyo inamfanya kutoamini kuwa Gamboshi ni ikulu ya wachawi bali ni sehemu ambayo wananchi wake wanampenda mungu na kumtegemea kuliko inavyosemwa.

“ Mimi nimefurahi kukuta kumbe wananchi wa huku wanampenda mungu sana, nilipofika hapa sikuamini kama ni kweli na ambacho kimekuwa kikiandikwa katika vyombo vya habari, Ni kweli GambosHi siyo ikulu ya wachawi”, anasema .

Kiongozi huyo anawataka waandishi wa habari, viongozi wa dini, siasa na serikali kutumia nafasi zao katika kuhakikisha Gamboshi inasafishwa kwa kuwaeleza watanzani kuwa siyo ikulu ya wachawi tena.

Askofu Sangu anawataka wananchi wa Gamboshi kubadilisha tabia na maisha yao kwa kuanza kumtegemea mungu, huku akisisitiza kuwapeleka shule na kanisani watoto wao.

“ Ujumbe wangu mkubwa kwenu badilikeni sasa, kuweni watu wa mungu, wapelekeni watoto weni shule, pamoja na kanisani ili wakapate mafundisho yaliyo mema ya kujenga kijiji chenu”, anaeleza

Kiongozi huyo anahitimisha kwa kuwataka watanzania kuacha fikra hasi kwa kijiji hicho, huku akiwataka kuamini kuwa kijiji hicho siyo tena ikulu ya wachawi bali ni kijiji kinachomtegemea mungu.
Enendeni Ulimwenguni Kote! Mtaitangaze Injili
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom