Nachukizwa sana na viongozi wetu Africa. Ni wanafiki sana, hawana misimamo, wanauza uhuru kwa maslahi binafsi. Tumeona haya kwa Mugabe na sasa Gadafi. Congo wamarekani wanashabikia vita huku wakiiba utajiri wa wananchi wake. Libya kwa kutumia branketi la demakrasia wanaisambaratisha nchi, watu wake na uchumi wake ili waendelee kututawala na kutuibia. Na sishangai urafiki wao hata kwa nchi kama Tanzania utapelekea kupata mkong'oto tu siku moja ili wachukue mali zetu. Jamaa asili yake Kenya. Iweje aipende Tanzania zaidi kuliko aliko na nasaba? Ama kweli, wajinga ndio wali wao.