Bwana Gadafi, amekaa madarakani kwa zaidi ya miaka 40, akiwaambia kuwa anawapenda watu wake. Cha ajabu ni kwamba, anawaua wale wanaompinga! Je, ni kweli anawapenda? Ikumbukwe kuwa hawa ni watu wake!
Amejaribu kumtumia mwanae kugawa mkwara au hata na kuua watu bila huruma, lakini wananchi wanapandisha HASIRA zaidi.
Amejaribu kulitumia jeshi, lakini, jeshi linamgeuka wakati mwingine na kujiunga na wananchi.
Amezuia internet, na mawasiliano mengine, akidhani kuwa watu wataacha, WAPI, wanazidi kumkomalia tu.
Amejitokeza mwenyewe kugawa mkwara, watu wanamwambia NCHI SIYO YAKO, LAZIMA UACHIE NGAZI!
Mkwara anaogawa, na visingizio rukuki, inaonyesha kuwa hakuota kuwa ipo siku atakuwa naye kama kina yahe! Haamini kuwa, MWISHO WAKE UMEFIKA. Anasema atafia kwenye tundu la asali! Ukiangalia muda aliotumia rais wa Tunisia kuachia ngazi, na muda aliotumia rais wa Misri kuachia ngazi (sambamba na mikwara aliyotoa), inaomnyesha kuwa Gadafi ataachia ngazi baada ya Februari na kabla ya April, 2011! Nadhani ndani ya siku 40!
Hata hivyo, anaweza kuwa ameua maelfu ya watu... siajabu hata elfu 3 au zaidi,
Mungu Ibariki AFRIKA.....Epusha bara hili na dhuruma.....