Mkuu acha kabisa, ukifika hapo kibirizi ukawa unawauliza michongo ya biashara, hawataki kabisa kukwambia sana sana ni kukukatisha tamaa, ila wao kila mala unaona wanapakiza bidhaa wanaondoka, na vitisho juu, kuwa bila kutumia uchawi huwezi!!nikaamua kujitoa muhanga mwenyewe wakaja kunikuta DRC, daaa bifu likahamia huko tena kuwa kwanini nimewaingilia bila ruhusa yao, hadi wakongo man wakawa wanashangaa, nyie watanzia vipi mbona hampendani, nikafanya yangu yaliyonipeleka, kurudi sasa wakasema nitajua sitapanda boti lolote lao kwani mengi ni ya waha, wenzao!!yaani majamaa hata kule congo yana jeuri kama kwao!!nilipoona mikwala imezidi nikaona kama mbwai iwe mbwai, tu nikatafuta wanajeshi watatu nikawapa franca 20000, kwa kutumia mwenyeji wangu, walipelekwa kambi ya jeshi, kutoka huko tuliheshimiana hadi natoka huko.kisa nilipeleka mzigo mzuri sana, nikauuza mala moja tu, ukaisha huku wao wakiwa hawauzi hadi wangu ulipoisha!!!