Fursa za kazi ughaibuni na mtazamo wangu

Iduku

Member
Aug 24, 2020
35
108
Habari wana jamvi! Leo nimewiwa kueleza machache kuhusu fursa za kufanya kazi nje ya nchi,mtazamo wangu binafsi na baadhi ya vijana waliopo hapa Tanzania na hata wale walio nje ya nchi wakifanya kazi huko au biashara. Hapa nitaeleza kile nilichokiona na kukutana nacho kwenye mchakato wa kutafuta ajira na fursa hizi za nje. Kwa vile Jamii forum ni jukwaa huru la watu kutoa mawazo,kuibua hoja,kukosoa na kujenga hoja basi ni sehemu sahihi kuleta mijadala.

Hata hivyo kuna wana jamvi humu sijui ni kwa kukosa elimu ya matumizi ya mitandao au kutokustaarabika au ushamba? Huwa hawana hoja mara zote hutukana au kutumia lugha za kuudhi,kila penye mijadala nyeti inayogusa maisha ya watu huleta kebehi na huchukua nafasi kutaka kutapeli watu: Hili ni tatizo kwa jamii yetu inatupasa tubadilike si busara sasa Jamii ya Kitanzania kukosa ustaarabu na kutokuaminika kwenye vitu nyeti.

Twende kwenye mada: Mwaka sasa nimekuwa nikipitia mada mbali mbali zinazoelezea fursa za kazi nje ya nchi hasa kwa nchi za Mashariki ya kati,Ulaya na Marekani; mada hizi zilinivutia na kunishawishi kujua zaidi na kutaka kupata fursa hizo maana nami ni miongoni mwa vijana wa Kitanzania tunaopambana kujikwamua kimaisha na imekuwa ndoto yangu kuwa penye nafasi nikafika nchi za nje nitachakarika sana kulingana na fursa zilizopo huko ili baadaye nirudi hapa kwetu Tanzania kuwekeza hata kama nitaajiri vijana watano shambani au kwenye gereji kwangu hiyo itakuwa ni furaha kuwa nimesaidia jamii yangu.

Kwanini vijana tunatamani kwenda huko (kuhalalisha nia),nitaeleza sababu chache ninazoona ni za msingi.
1. Mfumo wa elimu tulioipata toka shule za upili mpaka vyuo vikuu haujatujenga kuja kujikwamua kwa wakati. Sitaeleza kwa undani maana walio wengi wanaelewa homa ya graduates wengi hapa Tanzania; hivyo kukaa kusubiri ajira na kuzunguka kwenye ofisi za umma/watu na makampuni miaka nenda rudi ni upotezaji wa muda na nikutoelewa kuwa kijana ni rasilimali mhimu sana akiwa kwenye umri wa kufanya kazi; hivyo hii ni sababu tosha kwa kijana kushawishika kutafuta ajira nje ya nchi.

2. Uwepo wa fursa na rasilimali zinazohitaji mitaji yakueleweka kuzitumia. Si sahihi kuwa vijana wanaoenda nje ya nchi ni wavivu au wameacha fursa hapa nchini. Zipo fursa nyingi lakini zinahitaji rasilimali pesa kuzichangamkia. Vijana hawakopesheki kwenye mabenk au taasisi za fedha maana hawana dhamana nje ya vyeti vyao achana na waliotoka kwenye royal families, hapa naongelea kijana wa Kitanzania toka familia za chini.Fursa pekee wanayoiona ni kujiunga na makundi ya kisiasa kupata unafuu humo na wengine wamejikatia tamaa hawajui kesho itakuwaje maana hata mikopo ya vikundi ina milengo ya kisiasa. Je wote tuendeshe boda boda? Hivyo bado kuna sababu ya kutafuta suluhu hata beyond boarders.

3. Ipo mifano ya Watanzania waliotoka nje ya nchi na wamerudi wakiwa wamepiga hatua kubwa kiuchumi wamefungua biashara,wanamiradi mashambani na kwingineko. Hii haiondoi ukweli pia kuwa wapo vijana walipata bahati ya kutoka kwenda huko wamekumbwa na masaibu yali/nayowagharimu maisha yao;hii ni kutokana na sababu kuu mbili kukosa uaminifu binafsi wa kimaadili na tamaa ya pesa nyingi za haraka..hii sababu ya pili haiondoi ukweli kuwa vijana wa Kitanzania wana ari ya kufanya kazi halali,wanajituma wakipata nafasi na wanajielewa.

Nini kifanyike? Huku tukiendelea kuwahimiza vijana wajiajiri ilihali sisi tumeajiriwa, viongozi na wanasiasa lazima waelewe kuwa tatizo la ajira ni suala mtambuka na halipo Tanzania tu,waelewe wao ndo watunga sera ambazo kwa kiasi kikubwa zimeshindwa kumsaidia kijana wa Kitanzania kujiajiri huku maelfu ya vijana wakihitimu vyuo na kubaki kulanda landa mijini: Ni wakati sasa Serikali iwe na sera za wazi kuhusu fursa za kazi nje ya nchi, mathalani huduma za uwakala wa kazi za nje kwa Tanzania bado zinafanyika kwa uficho; Taasisi ya Serikali kama TAeSa inapaswa iweke wazi Takwimu za mawakala walioidhinishwa Tanzania kufanya shughuli za kuunganisha watanzania na kazi za nje.

Serikali itoe elimu kuhusu dhana potofu ya kuwa watanzania wakienda nje kufanya kazi wanateswa,iendelee kuimarisha balozi zetu huko nje na watanzania wanaojikuta kwenye masaibu waelezwe taratibu za kufuata kabla hawajaenda nje,na waepuka kuvunja sheria za kazi au nchi hizo na waajiri wao na inapotokea wametendewa kinyume wajue pakuripoti.

Unyanyasaji haupo nje kwa kwa vile watu wapo kule ugenini,hata hapa nchini unyanyasaji upo mwingi na wakati mwingine ni mkubwa kuliko huo ambao jamii inaamini watu wanatendewa huko nje. Mfano kukosa kazi ni unyanyasaji tosha ambao athari yake kila mtu anaiona.

Nchi ya Kenya, Nigeria na nyingine barani Afrika wamepiga hatua sana kwenye hili,wale waliopo nje mara nyingi wanashuhudia kukuta wakenya wengi wakifanya kazi huko mashariki ya kati, ulaya na Marekani. Hata hapa kwetu inawezekana tukapunguza kiasi changamoto za ajira kwa kuwa na sera za wazi na usimamizi mzuri wa watu kwenda mataifa mengine kufanya kazi.

Naelewa zipo changamoto nyingine kama ugumu wa kupata hati ya kusafiria,hili linawezekana kuangaliwa upya hasa kama huduma za uwakala na kazi za nje zitakuwa nyingi na za uwazi.

Hii ni kuwatia moyo vijana wenzangu kuwa tunapotafuta ajira hapa nchini tujue pia kuwa hata huko nje kuna fursa na zinaweza kututoa toka tulipo kuliko kutafuta kazi miaka zaidi ya mitatu hapa hapa huku hujui utaipata lini,hujui utaishi wapi na vipi.Hii ni hatari na imeendelea kuongeza vijana wenye msongo wa mawazo na wengine wanafanya matukio ya ajabu sana maana wamekata tamaa.

Wito wangu kwa watanzania waliopo nje ni kuwa unganisha vijana wenzenu tulipo nyumbani huku na tupo tayari kuvuka boda kutafuta maisha; Ninyi ndiyo mabalozi wetu huko,akifika huko Mtanzania mwenzio hatachukua ridhiki yako ila atawajibika kivyake kujikwamua.

Hii tabia ya kutoaminiana na kutelekezana kwa watanzania inaanzia hapa hapa nyumbani,baadhi ya diaspora wanasema watanzania siyo wakuwaamini maana akifika huko anabadilika! Hii haiwezi kuwa jumla kiasi hiko na si wote, hivi kama wa- Nigeria tunaowajua ni matapeli sana lakini wao wanaitana huko nje,hata ndg zetu wakenya je sisi ndo mioyo yetu ni midogo tusiweze? Kwanini tuwaachie kina Ernest Makulilo peke yao, wakati watanzania wapo karibia mabara yote ya Dunia?

Ni wakati sasa wa kushare fursa za ajira nje ya nchi kwa watanzania wote,aliye tayari afuate taratibu na akipata akafanye kazi kwa uaminifu ili awe balozi kwa wengine. Nawatakia kazi nje na kila la heri wapambanaji wenzangu;
 
Kusafiri ni elimu tosha

Wengi wanaosafiri na kwenda kufanya kazi nje huwa wanajifunza mengi sana ingawa wakirudi tena waankutana na changamoto nyingi sana nyumbani

Waatalamu au wanaojiita wasomi ni wa kukariri tu ila kiuhalisia ni vilaza wa maisha ya ukweli
 
Habari wana jamvi! Leo nimewiwa kueleza machache kuhusu fursa za kufanya kazi nje ya nchi,mtazamo wangu binafsi na baadhi ya vijana waliopo hapa Tanzania na hata wale walio nje ya nchi wakifanya kazi huko au biashara. Hapa nitaeleza kile nilichokiona na kukutana nacho kwenye mchakato wa kutafuta ajira na fursa hizi za nje. Kwa vile Jamii forum ni jukwaa huru la watu kutoa mawazo,kuibua hoja,kukosoa na kujenga hoja basi ni sehemu sahihi kuleta mijadala.

Hata hivyo kuna wana jamvi humu sijui ni kwa kukosa elimu ya matumizi ya mitandao au kutokustaarabika au ushamba? Huwa hawana hoja mara zote hutukana au kutumia lugha za kuudhi,kila penye mijadala nyeti inayogusa maisha ya watu huleta kebehi na huchukua nafasi kutaka kutapeli watu: Hili ni tatizo kwa jamii yetu inatupasa tubadilike si busara sasa Jamii ya Kitanzania kukosa ustaarabu na kutokuaminika kwenye vitu nyeti.

Twende kwenye mada: Mwaka sasa nimekuwa nikipitia mada mbali mbali zinazoelezea fursa za kazi nje ya nchi hasa kwa nchi za Mashariki ya kati,Ulaya na Marekani; mada hizi zilinivutia na kunishawishi kujua zaidi na kutaka kupata fursa hizo maana nami ni miongoni mwa vijana wa Kitanzania tunaopambana kujikwamua kimaisha na imekuwa ndoto yangu kuwa penye nafasi nikafika nchi za nje nitachakarika sana kulingana na fursa zilizopo huko ili baadaye nirudi hapa kwetu Tanzania kuwekeza hata kama nitaajiri vijana watano shambani au kwenye gereji kwangu hiyo itakuwa ni furaha kuwa nimesaidia jamii yangu.

Kwanini vijana tunatamani kwenda huko (kuhalalisha nia),nitaeleza sababu chache ninazoona ni za msingi.
1. Mfumo wa elimu tulioipata toka shule za upili mpaka vyuo vikuu haujatujenga kuja kujikwamua kwa wakati. Sitaeleza kwa undani maana walio wengi wanaelewa homa ya graduates wengi hapa Tanzania; hivyo kukaa kusubiri ajira na kuzunguka kwenye ofisi za umma/watu na makampuni miaka nenda rudi ni upotezaji wa muda na nikutoelewa kuwa kijana ni rasilimali mhimu sana akiwa kwenye umri wa kufanya kazi; hivyo hii ni sababu tosha kwa kijana kushawishika kutafuta ajira nje ya nchi.

2. Uwepo wa fursa na rasilimali zinazohitaji mitaji yakueleweka kuzitumia. Si sahihi kuwa vijana wanaoenda nje ya nchi ni wavivu au wameacha fursa hapa nchini. Zipo fursa nyingi lakini zinahitaji rasilimali pesa kuzichangamkia. Vijana hawakopesheki kwenye mabenk au taasisi za fedha maana hawana dhamana nje ya vyeti vyao achana na waliotoka kwenye royal families, hapa naongelea kijana wa Kitanzania toka familia za chini.Fursa pekee wanayoiona ni kujiunga na makundi ya kisiasa kupata unafuu humo na wengine wamejikatia tamaa hawajui kesho itakuwaje maana hata mikopo ya vikundi ina milengo ya kisiasa. Je wote tuendeshe boda boda? Hivyo bado kuna sababu ya kutafuta suluhu hata beyond boarders.

3. Ipo mifano ya Watanzania waliotoka nje ya nchi na wamerudi wakiwa wamepiga hatua kubwa kiuchumi wamefungua biashara,wanamiradi mashambani na kwingineko. Hii haiondoi ukweli pia kuwa wapo vijana walipata bahati ya kutoka kwenda huko wamekumbwa na masaibu yali/nayowagharimu maisha yao;hii ni kutokana na sababu kuu mbili kukosa uaminifu binafsi wa kimaadili na tamaa ya pesa nyingi za haraka..hii sababu ya pili haiondoi ukweli kuwa vijana wa Kitanzania wana ari ya kufanya kazi halali,wanajituma wakipata nafasi na wanajielewa.

Nini kifanyike? Huku tukiendelea kuwahimiza vijana wajiajiri ilihali sisi tumeajiriwa, viongozi na wanasiasa lazima waelewe kuwa tatizo la ajira ni suala mtambuka na halipo Tanzania tu,waelewe wao ndo watunga sera ambazo kwa kiasi kikubwa zimeshindwa kumsaidia kijana wa Kitanzania kujiajiri huku maelfu ya vijana wakihitimu vyuo na kubaki kulanda landa mijini: Ni wakati sasa Serikali iwe na sera za wazi kuhusu fursa za kazi nje ya nchi, mathalani huduma za uwakala wa kazi za nje kwa Tanzania bado zinafanyika kwa uficho; Taasisi ya Serikali kama TAeSa inapaswa iweke wazi Takwimu za mawakala walioidhinishwa Tanzania kufanya shughuli za kuunganisha watanzania na kazi za nje.

Serikali itoe elimu kuhusu dhana potofu ya kuwa watanzania wakienda nje kufanya kazi wanateswa,iendelee kuimarisha balozi zetu huko nje na watanzania wanaojikuta kwenye masaibu waelezwe taratibu za kufuata kabla hawajaenda nje,na waepuka kuvunja sheria za kazi au nchi hizo na waajiri wao na inapotokea wametendewa kinyume wajue pakuripoti.

Unyanyasaji haupo nje kwa kwa vile watu wapo kule ugenini,hata hapa nchini unyanyasaji upo mwingi na wakati mwingine ni mkubwa kuliko huo ambao jamii inaamini watu wanatendewa huko nje. Mfano kukosa kazi ni unyanyasaji tosha ambao athari yake kila mtu anaiona.

Nchi ya Kenya, Nigeria na nyingine barani Afrika wamepiga hatua sana kwenye hili,wale waliopo nje mara nyingi wanashuhudia kukuta wakenya wengi wakifanya kazi huko mashariki ya kati, ulaya na Marekani. Hata hapa kwetu inawezekana tukapunguza kiasi changamoto za ajira kwa kuwa na sera za wazi na usimamizi mzuri wa watu kwenda mataifa mengine kufanya kazi.

Naelewa zipo changamoto nyingine kama ugumu wa kupata hati ya kusafiria,hili linawezekana kuangaliwa upya hasa kama huduma za uwakala na kazi za nje zitakuwa nyingi na za uwazi.

Hii ni kuwatia moyo vijana wenzangu kuwa tunapotafuta ajira hapa nchini tujue pia kuwa hata huko nje kuna fursa na zinaweza kututoa toka tulipo kuliko kutafuta kazi miaka zaidi ya mitatu hapa hapa huku hujui utaipata lini,hujui utaishi wapi na vipi.Hii ni hatari na imeendelea kuongeza vijana wenye msongo wa mawazo na wengine wanafanya matukio ya ajabu sana maana wamekata tamaa.

Wito wangu kwa watanzania waliopo nje ni kuwa unganisha vijana wenzenu tulipo nyumbani huku na tupo tayari kuvuka boda kutafuta maisha; Ninyi ndiyo mabalozi wetu huko,akifika huko Mtanzania mwenzio hatachukua ridhiki yako ila atawajibika kivyake kujikwamua.

Hii tabia ya kutoaminiana na kutelekezana kwa watanzania inaanzia hapa hapa nyumbani,baadhi ya diaspora wanasema watanzania siyo wakuwaamini maana akifika huko anabadilika! Hii haiwezi kuwa jumla kiasi hiko na si wote, hivi kama wa- Nigeria tunaowajua ni matapeli sana lakini wao wanaitana huko nje,hata ndg zetu wakenya je sisi ndo mioyo yetu ni midogo tusiweze? Kwanini tuwaachie kina Ernest Makulilo peke yao, wakati watanzania wapo karibia mabara yote ya Dunia?

Ni wakati sasa wa kushare fursa za ajira nje ya nchi kwa watanzania wote,aliye tayari afuate taratibu na akipata akafanye kazi kwa uaminifu ili awe balozi kwa wengine. Nawatakia kazi nje na kila la heri wapambanaji wenzangu;
Umeongea kitu kikubwa mzee, kujilipua tu no way maana had uje kupata connection ngum sana
 
Mimi binafsi ni mmoja kati ya wanaoamini kutoboa katika nchi za ughaibuni, watanzania wengi tunakosa fikra ya kuwa maisha ni popote, wengi hatufikirii kabisa kama kuna uwezekano wa kutoka na kwenda ughaibuni na badala yake huwa tunaona kama ni ndoto na kitu ambacho kamwe hakiwezekani. utakatishwa tamaa mara tu utakaposema unatamani kutoka nje ya nchi kwa lengo la kutafuta maisha wengine watakutisha kuwa ukienda huko utaishia kunyanyasika na kubaguliwa kutokana na rangu yako, watakujaza maneno yatakayokufanya uone nje ya nchi ni kama gereza la segerea. Lakini ukweli ni kwamba ughaibuni ni rahisi sana kutoboa maisha kama utaenda na kujituma vizuri.

Nilifanya utafiti nikagundua kuwa pesa ya tanzania inathamani ndogo sana ukilinganisha na pesa za nchi nyingine za afrika na hata nchi za ughaibuni. Hili suala la pesa kuwa na thamani ndogo ni tatizo kwa uchumi wa nchi lakini mimi binafsi nimetokea kuliona kama fursa kwa vijana watakaokuwa tayari kwenda kutafuta maisha nchi za ughaibuni. Pindi utakapoamua kuvaa mabomu na kujiripua kwenda ughaibuni kutafuta kazi amini lazima utatoboa kama utakuwa unajua ulichokifuata. Ukisikia mtu ameenda ughaibuni na akarudi anamaisha mazuri, sio kwamba kule ughaibuni analipwa mshahara mkubwa sana, HAPANA. Huwa wanalipwa pesa ya kawaida sana kwa matumizi na mahutaji ya kule ila ukiibadilisha ile fedha kuja kuwa pesa ya kitanzania (Tsh) inageuka kuwa ni pesa ndefu mno kiasi kwamba hata mlinzi wa kule anaweza kulipwa mshahara mara mbili ya mtu mwenye elimu ya masters hapa tanzania. Hii ndio sababu watu walitunga ule msemo wa kwamba NI BORA KUWA MBWA ULAYA KULIKO KUWA BINADAMU TANZANIA, msemo huu haukumaanisha MBWA kama tunavouchukulia bali ni kwamba BORA KUWA MTU WA HADHI YA CHINI KATIKA NCHI ZA UGHAIBUNI KULIKO KUWA MWENYE HADHI HAPA BONGO.

Nilishangazwa sana kuona HOMELESS katika nchi kama za marekani anamiliki gari ambayo huku Tanzania anamiliki Lecturer wa chuo kikuu na anavimba nayo na watu wote tunamsujudia (HII NI TRUE NA SIJAONGEZA CHUMVI). Kwa hali kama hiyo kwanini tusifikirie kwenda kutafuta maisha kwenye nchi za ughaibuni?

Nchi kama marekani hata ukiwa huna elimu na ukajua tu kusoma na kuandika, kupata kazi ya kuingiza dola 15 kwa saa ni kawaida, muda wa kazi kwa siku ni masaa 8 kwaio kuna uwezekano wa kutengeneza dola 120 au zaidi. Ndani ya wiki utakuwa na uwezo wa kupata sio chini ya dola 400 ukitoa matumizi muhimu. Huku tanzania dola 400 ni zaidi ya laki 8. Hii inamaanisha kwamba kwa nchi kama marekani hata kama huna elimu kupata smartphone ni swala la siku tatu hadi nne, mradi tu uwe na kazi ya kukuingizia kipato. Wakati hapa bongo kupata smartphone kwa mtu wa kawaida ni bajeti ya wiki au miezi kadhaa. fikiria ni mfanya kazi gani anayeingiza laki 8 kwa wiki hapa tanzania. Hii ndiyo sababu vijana tunatakiwa tuhamasike kwenda kutafuta maisha nje ya nchi na kuja kuwekeza nyumbani ambako pesa haina thamani. Kwanini tusitoboe?, kwanini tusiokoe familia zetu?, Tutafuteni fursa za kwenda kutafuta maisha nje ya nchi.

Kuna jamaa mmoja anaitwa Dulla star anachaneli yake pele mjini youtube, huyu jamaa anaeleza ni namna gani maisha yanawezekana kutoboka kupitia kwenda ughaibuni, huwa anaonesha mishe ambazo watu wanafanya na kutoboa maisha wakiwa ughaibuni. (Mfuatilieni uyo jamaa, anainspire sana)

Mimi binafsi ni mwanachuo na nakaribia kuhitimu shahada ya elimu. Lakini najua kabisa kuwa kwa sasa hapa bongo amna cha kupata, naamua kuvaa mabomu kwenda ughaibuni kutafuta mkwanja, sijaanza process yoyote bado lakini naamini kila kitu kitakaa sawa na kama kuna mtu anajuana na agent yoyote anayefanikisha michongo ya kazi katika nchi za kiarabu basi anipe namba yake nianze kufanya mipango mapema nataka nikaanzie Asia kwanza alafu uko kwingine tutafika tu. Tafadhali kama unaconnection ya agent share na mimi utakuwa umenisaidia sana.

WATANZANIA TUAMKE TUKAPAMBANE UGHAIBUNI.
 
Mimi binafsi ni mmoja kati ya wanaoamini kutoboa katika nchi za ughaibuni, watanzania wengi tunakosa fikra ya kuwa maisha ni popote, wengi hatufikirii kabisa kama kuna uwezekano wa kutoka na kwenda ughaibuni na badala yake huwa tunaona kama ni ndoto na kitu ambacho kamwe hakiwezekani. utakatishwa tamaa mara tu utakaposema unatamani kutoka nje ya nchi kwa lengo la kutafuta maisha wengine watakutisha kuwa ukienda huko utaishia kunyanyasika na kubaguliwa kutokana na rangu yako, watakujaza maneno yatakayokufanya uone nje ya nchi ni kama gereza la segerea. Lakini ukweli ni kwamba ughaibuni ni rahisi sana kutoboa maisha kama utaenda na kujituma vizuri.

Nilifanya utafiti nikagundua kuwa pesa ya tanzania inathamani ndogo sana ukilinganisha na pesa za nchi nyingine za afrika na hata nchi za ughaibuni. Hili suala la pesa kuwa na thamani ndogo ni tatizo kwa uchumi wa nchi lakini mimi binafsi nimetokea kuliona kama fursa kwa vijana watakaokuwa tayari kwenda kutafuta maisha nchi za ughaibuni. Pindi utakapoamua kuvaa mabomu na kujiripua kwenda ughaibuni kutafuta kazi amini lazima utatoboa kama utakuwa unajua ulichokifuata. Ukisikia mtu ameenda ughaibuni na akarudi anamaisha mazuri, sio kwamba kule ughaibuni analipwa mshahara mkubwa sana, HAPANA. Huwa wanalipwa pesa ya kawaida sana kwa matumizi na mahutaji ya kule ila ukiibadilisha ile fedha kuja kuwa pesa ya kitanzania (Tsh) inageuka kuwa ni pesa ndefu mno kiasi kwamba hata mlinzi wa kule anaweza kulipwa mshahara mara mbili ya mtu mwenye elimu ya masters hapa tanzania. Hii ndio sababu watu walitunga ule msemo wa kwamba NI BORA KUWA MBWA ULAYA KULIKO KUWA BINADAMU TANZANIA, msemo huu haukumaanisha MBWA kama tunavouchukulia bali ni kwamba BORA KUWA MTU WA HADHI YA CHINI KATIKA NCHI ZA UGHAIBUNI KULIKO KUWA MWENYE HADHI HAPA BONGO.

Nilishangazwa sana kuona HOMELESS katika nchi kama za marekani anamiliki gari ambayo huku Tanzania anamiliki Lecturer wa chuo kikuu na anavimba nayo na watu wote tunamsujudia (HII NI TRUE NA SIJAONGEZA CHUMVI). Kwa hali kama hiyo kwanini tusifikirie kwenda kutafuta maisha kwenye nchi za ughaibuni?

Nchi kama marekani hata ukiwa huna elimu na ukajua tu kusoma na kuandika, kupata kazi ya kuingiza dola 15 kwa saa ni kawaida, muda wa kazi kwa siku ni masaa 8 kwaio kuna uwezekano wa kutengeneza dola 120 au zaidi. Ndani ya wiki utakuwa na uwezo wa kupata sio chini ya dola 400 ukitoa matumizi muhimu. Huku tanzania dola 400 ni zaidi ya laki 8. Hii inamaanisha kwamba kwa nchi kama marekani hata kama huna elimu kupata smartphone ni swala la siku tatu hadi nne, mradi tu uwe na kazi ya kukuingizia kipato. Wakati hapa bongo kupata smartphone kwa mtu wa kawaida ni bajeti ya wiki au miezi kadhaa. fikiria ni mfanya kazi gani anayeingiza laki 8 kwa wiki hapa tanzania. Hii ndiyo sababu vijana tunatakiwa tuhamasike kwenda kutafuta maisha nje ya nchi na kuja kuwekeza nyumbani ambako pesa haina thamani. Kwanini tusitoboe?, kwanini tusiokoe familia zetu?, Tutafuteni fursa za kwenda kutafuta maisha nje ya nchi.

Kuna jamaa mmoja anaitwa Dulla star anachaneli yake pele mjini youtube, huyu jamaa anaeleza ni namna gani maisha yanawezekana kutoboka kupitia kwenda ughaibuni, huwa anaonesha mishe ambazo watu wanafanya na kutoboa maisha wakiwa ughaibuni. (Mfuatilieni uyo jamaa, anainspire sana)

Mimi binafsi ni mwanachuo na nakaribia kuhitimu shahada ya elimu. Lakini najua kabisa kuwa kwa sasa hapa bongo amna cha kupata, naamua kuvaa mabomu kwenda ughaibuni kutafuta mkwanja, sijaanza process yoyote bado lakini naamini kila kitu kitakaa sawa na kama kuna mtu anajuana na agent yoyote anayefanikisha michongo ya kazi katika nchi za kiarabu basi anipe namba yake nianze kufanya mipango mapema nataka nikaanzie Asia kwanza alafu uko kwingine tutafika tu. Tafadhali kama unaconnection ya agent share na mimi utakuwa umenisaidia sana.

WATANZANIA TUAMKE TUKAPAMBANE UGHAIBUNI.
CIML Man Power
[Mobile] 0752 564 154
 
CIML Man Power
[Mobile] 0752 564 154
Hawa CIML Man Power hawako serious na recruitment yao, huwezi itisha watu kwa ajili ya usaili zaidi ya miezi sita huku hawajui unafanya usaili mwezi gani, tangazo la kutuma maombi ya kazi lipo tangu Disemba lakini hakuna usaili unafanywa, just simple wanakusanya ada ya usaili elfu 50 kwa kila mwombaji..embu hawa agents wa bongo wawe serious na hizi mambo,weka bayana mchakato,ita watu hata kama wanalipa ada ya usaili au commission fee wajue process yote kuepusha maswali.

Sent from my TECNO KG5j using JamiiForums mobile app
 
Hawa CIML Man Power hawako serious na recruitment yao, huwezi itisha watu kwa ajili ya usaili zaidi ya miezi sita huku hawajui unafanya usaili mwezi gani, tangazo la kutuma maombi ya kazi lipo tangu Disemba lakini hakuna usaili unafanywa, just simple wanakusanya ada ya usaili elfu 50 kwa kila mwombaji..embu hawa agents wa bongo wawe serious na hizi mambo,weka bayana mchakato,ita watu hata kama wanalipa ada ya usaili au commission fee wajue process yote kuepusha maswali.

Sent from my TECNO KG5j using JamiiForums mobile app
So Ina maana umelipa Registration fee tangu Mwaka jana hadi Leo hujaitwa kwenye interview?
 
Pengine target ya namba ya idadi ya watu wanaowataka Bado haijafikia kama wanavyodai
Kwa kiwanda wanachotaka watu waende ni sahihi namba haijafikia.. jambo la muhimu ambalo wanakosea ni kitowaeleza waombaji kuhusu hilo. Maana kwa haraka kwa uchunguzi binafsi nilioufanya kujua namna nguvu kazi inavyochukuliwa na na kampuni ya Alamarai huwa inafanya usaili mara moja kwa mwaka na wanaochagiliwa huwa wanaenda kwa batch,..hii nimeishuhudua kupitia kampuni ya Bravo ya Abas Mtemvu. Maana huko pia kuna watu walichaguliwa mwaka jana lakini batch nyingine ndiyo imeondoka wili iliyopita (TBC TV ) Waliwaonesha na kuwahoji airport.
 
Kwa kiwanda wanachotaka watu waende ni sahihi namba haijafikia.. jambo la muhimu ambalo wanakosea ni kitowaeleza waombaji kuhusu hilo. Maana kwa haraka kwa uchunguzi binafsi nilioufanya kujua namna nguvu kazi inavyochukuliwa na na kampuni ya Alamarai huwa inafanya usaili mara moja kwa mwaka na wanaochagiliwa huwa wanaenda kwa batch,..hii nimeishuhudua kupitia kampuni ya Bravo ya Abas Mtemvu. Maana huko pia kuna watu walichaguliwa mwaka jana lakini batch nyingine ndiyo imeondoka wili iliyopita (TBC TV ) Waliwaonesha na kuwahoji airport.
Halafu samahani naomba kuuliza, coz hii Kampuni mm nimeijua kupitia jamaa angu ndio kanipa connection naye kashafanya registration anasubiri tu interview

Sasa swali langu ni, hao watu wanaoenda huko kuna maendeleo yeyote wanafanya huku nchini kwao, Yani Namaanisha kazi zinalipa au tu inawalipa kwa wao kuishi maisha mazuri huko nje?
 
Halafu samahani naomba kuuliza, coz hii Kampuni mm nimeijua kupitia jamaa angu ndio kanipa connection naye kashafanya registration anasubiri tu interview

Sasa swali langu ni, hao watu wanaoenda huko kuna maendeleo yeyote wanafanya huku nchini kwao, Yani Namaanisha kazi zinalipa au tu inawalipa kwa wao kuishi maisha mazuri huko nje?
Nitatoa details mhimu nilizozifahamu hapa kuhusu hizo kazi jioni.
 
Iko hivi wao wanachukua nguvu kazi toka huku,kabla hujaondoka utafanya maandalizi ya awali kama vile vipimo vya magonjwa (medical examination), police clearance kulipia wakala wa serikali wa kazi za nje (TAESA) na vingine vidogo vidogo vya muhimu wakala wa kazi aliyekuunganisha nao atakujuza. Kabla hujaondoka wao (kampuni hiyo ya uarabuni inayotaka wafanyakazi) wanakutumia visa yako ambayo mara nyingi itaonesha ni ya kwenda na kurudi,utasoma mkataba wa kazi na kama utakubaliana utasaini huku huku kabla ya safari. Maandalizi na vielelezo hivyo vikikamilika utasafiri kwenda huko Uarabuni. Huko unaenda kufanya kazi mara nyingi kwa hizi nchi za uarabuni wanakupa chakula na malazi (food/allowance and accommodation). Utakapopokea mshahara mwisho wa mwezi,ni juu yako utume nyumbani au ununue IPHONE hakuna atakayekupangia matumizi ya hela yako,hata kama utaamua utunze zote utatumia ukirudi ni wewe tu. Wao wanataka upige kazi yao kwa wakati na ufanisi.. nadhani hapo nitakuwa nimekujibu swali lako.
 
Iko hivi wao wanachukua nguvu kazi toka huku,kabla hujaondoka utafanya maandalizi ya awali kama vile vipimo vya magonjwa (medical examination), police clearance kulipia wakala wa serikali wa kazi za nje (TAESA) na vingine vidogo vidogo vya muhimu wakala wa kazi aliyekuunganisha nao atakujuza. Kabla hujaondoka wao (kampuni hiyo ya uarabuni inayotaka wafanyakazi) wanakutumia visa yako ambayo mara nyingi itaonesha ni ya kwenda na kurudi,utasoma mkataba wa kazi na kama utakubaliana utasaini huku huku kabla ya safari. Maandalizi na vielelezo hivyo vikikamilika utasafiri kwenda huko Uarabuni. Huko unaenda kufanya kazi mara nyingi kwa hizi nchi za uarabuni wanakupa chakula na malazi (food/allowance and accommodation). Utakapopokea mshahara mwisho wa mwezi,ni juu yako utume nyumbani au ununue IPHONE hakuna atakayekupangia matumizi ya hela yako,hata kama utaamua utunze zote utatumia ukirudi ni wewe tu. Wao wanataka upige kazi yao kwa wakati na ufanisi.. nadhani hapo nitakuwa nimekujibu swali lako.
Shukrani mkuu, umejibu Barbara kabisa, na Nini maoni yako kwa mtu anayetaka kwenda kufanya usaili kati ya CIML Man power na hiyo Bravo ya mtemvu utamshauri aende kufanya usaili Kampuni gani kati ya hizo mbili?
 
Shukrani mkuu, umejibu Barbara kabisa, na Nini maoni yako kwa mtu anayetaka kwenda kufanya usaili kati ya CIML Man power na hiyo Bravo ya mtemvu utamshauri aende kufanya usaili Kampuni gani kati ya hizo mbili?
Bravo wana idadi kubwa ya waombaji hivyo inaweza kukuchukua muda sana kufikiwa batch yako. Mfano walioenda Wiki mbili zilizopita wamefanyiwa usaili mwezi wa 10 mwaka jana. Kwa maelezo ya mzee Mtemvu this coming interview watahitajika karibia watu elfu moja,hao wote hawaendi kwa mkupuo wataenda kwa batch kulingana na uharaka kwa section zinazohitaji man power replenishment.. nadhani kwa hizi kazi za Armarai-Saudi Arabia hazihitaji mtu uwe na haraka hata kama ukifanyiwa usaili. Hivyo ili uwe kwenye nafasi ya kwenda walau kwa wakati heri ukajisajili CIML maana wao hawajulikani sana na hawana namba kubwa ya waombaji.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom