Kuna vitu hapa bado hujafafanua. Kitaalamu katika hesabu au aina za Gharama Kuna Gharama zinazobadilika kulingana na Uzalishaji (Variable Costs), na kuna zenye hazibadiliki kulingana na Uzalishaji (Fixed Costs).
Mfano hapo usafiri wa pembejeo kwenda shambani ina maana hata nikitaka heka 3 utaongexeka?
Halafu pili Kuna Gharama ambazo kadiri unavyozalisha zaidi ndio zinajifidia na zingine. Labda mbolea mfuko mmoja ni kweli ni heka moja kamili haibaki hata kidogo?
Pia mtu akihitaji heka 10 gharama za usimamizi ni bei hiyo hiyo 100,000/- haipungui?