Aman Ng'oma
JF-Expert Member
- Nov 8, 2011
- 954
- 510
- Thread starter
- #101
KILIMO CHA VIAZI LISHE NI UTAJIRI WA WAZI, TUCHANGAMKIE!
Tukupe nini tena mkulima wetu. Kama soko tumekutafutia tena ni soko la uhakika kabisa. Kazi uliyobaki nayo kwa sasa ni moja tu, kuzalisha viazi. Sehemu ya kuuzia wala hutagangaika. Kinasoru East Africa Tanzania Ltd imefanya kazi kwa niaba yako.
Awali tuliegemea kwenye viazi aina ya Mataya na Jewel pekee, lakini kwa sasa, tunaendelea kuwashawishi wadau wetu ili waweze kuchukua na aina nyingine za viazi lishe ili wakulima wengi zaidi waweze kunufaika. Na kwa hili, kwakweli, tunaelekea kufanikiwa.
Tulikuwa kimya kwa muda mrefu lakini ukimya wetu ulikuwa na majukumu mengi na makubwa nyuma ya pazia. Moja ya jukumu tulilokuwa tukishughulika nalo, ilikuwa ni kutafuta barua ya ithibati kutoka kwenye taasisi inayotambulika ili kuwabebea dhamana wakulima ambao mbegu zao hawakuzitoa kutoka kwenye vyanzo vinavyotambulika.
Tunashukuru hilo tuliweza kulifanikisha na tunawashukuru sana wahusika waliyotusaidia.
Vilevile tulikuwa tunaandaa kanzi data ya wakulima wa viazi lishe na hasa wale wakulima ambao viazi vyao viko tayari kwenda sokoni. Hadi sasa tumefanikiwa kupata ekari zaidi ya 200 za viazi lishe vilivyozalishwa bila mkataba wetu na viko tayari kwenda sokoni. Na mashamba mengine zaidi ya ekari 100 ziko kwenye hatua mbalimbali. Na mashamba yote hayo tumeshayatambua na kuyaingiza kwenye kanzi data yetu.
Na juzi kulikuwa na kikao cha bodi kilichojadiri mambo ya uvunaji, upakiji na usafirishaji. Ni namna gani wakulima wavune, wapaki na wasafirishe viazi vyao kutoka shambani hadi kwenye ghala la kukusanyia viazi kabla ya kuvisafirisha kwenda kwenye soko la kimataifa.
Kwenye suala la uvunaji ilijadiliwa kuwa mkulima anapaswa kuwa makini sana kwani haitakiwi kiazi kichubuliwe kwa namna yoyote ile, lakini vile kiazi hakitakiwi kikatwa. Kiazi kinapochimbwa kinapaswa kitoke na ile kamba yake ya kwenye ncha.
Lakini kwenye upande wa upakiji, mkulima anatakiwa kupaki vizuri kwenye kreti maalum za plastiki au mabox ya mbao na si kwenye mifuko ya viroba ya sandarausi au magunia ya katani kama ilivyozoeleka. Vifaa hivyo ndivyo vitakavyotumika kusafirishia viazi kwenda Dsm kwenye ghala maalum lililoandaliwa kwa ajili ya kukusanyia viazi kabla ya kuvisafirisha kwenda kwenye soko letu la kimataifa.
Sasa hivi tuko kwenye hatua za mwisho mwisho za kukamilisha taratibu zitakazowezesha kuanza kwa zoezi la ununuaji wa viazi kutoka kwa wakulima. Na ikiwa wewe ni mkulima na una viazi ambavyo viko tayari kwenda sokoni, tafadhali tutumie sample kwa njia whatsap, chagua viazi vizuri ambavyo havijaliwa na wadudu na viazi hivyo vitatumika kutoa picha ya jumla ya viazi uliyonao shambani kwako. Katika picha za viazi utakazotutumia utapaswa kuonyesha urefu wa kiazi kwa maana ya sentimeta pamoja na uzito wake kwa maana ya Kilogram.
Kama una aina nyingi ya viazi katika shamba lako, basi utachimba viazi kadhaa kila aina kisha utafuata utaratibu wa upimaji wa kila aina ya viazi kama nilivyoelekeza hapo juu na kisha utapiga picha na kututumia kwa njia ya whatsap. Kiazi tunachokitaka kinatakiwa kiwe na wastani wa uzito angalau kuanzia gram 300 hadi 600 kwa kiazi kimoja.
Hiki ndicho kilimo cha viazi lishe. Unaweza kuona kama unasumbuliwa lakini lengo ni kuona kama vinafaa kwa soko letu la kimataifa. Ni muhimu sana kila mkulima akazingatia kanuni za kilimo bora.
Mkulima ataweza kuuza kilo moja ya viazi vyake kwa TZS 800 haijalishi una mzigo kiasi, soko letu ni kubwa sana ndiyo maana kila siku tunaendelea kuhamasisha wakulima wengi zaidi ili waweze kuingia kwenye fursa hii. Fanya kazi upate hela.
Kwa wakulima wapya na hasa wakulima wanaolima pamoja yaani Block farming, tunaendelea kutoa mikataba kwa ajili ya kuwapa uhakika wa soko, vigezo na masharti kuzingatiwa.
Kinasoru East Africa (T) ina fursa nyingi kwenye kilimo biashara, na kwa sasa fursa zilizo tayari ni Kilimo cha Papai aina ya Malkia, Pilipili kichaa pamoja na viazi lishe vyenyewe.
Fursa ya Maboga Vibuyu au Butternut Squash iko njiani inakuja, kwa sasa unafanyika kwanza utaratibu wa kuagiza mbegu zinazotakiwa kwa ajili ya maboga hayo. Kwahakika, kwenye kilimo chetu hakuna kubeti, ukiweka jitihada utapata kadiri ya jitihada yako. Lazima tumuunge mkono Mheshimiwa Rais wetu kwa kutekeleza kauli mbiu yake ya hapa kazi tu kwa vitendo.
Papai moja lenye wastani wa uzito wa kilo moja linanunuliwa kwaTZS 500 wakati Pilipili Kichaa yenyewe ikiwa mbichi inanunuliwa kwa TZS 2000 kwa kilo moja na ile iliyokaushwa inanunuliwa kwa TZS 4000. Shamba la ekari moja lililolimwa pilipili kichaa linatoa si chini ya tani sita kwa wastani wa mivuno mnne.
Na hii ndiyo habari niliyopanga kuwapa siku ya leo.
Kama kuna lolote la ufafanuzi tafadhali tuwasiliane kwa anuani zetu hapo chini.
Aman Ng'oma
Mkurugenzi Mtendaji
Kinasoru East Africa Tanzania Ltd
Msalato Bible
+255767989713, +255655038210, +255786989713
Email: amanngoma@gmail.com
Dodoma
Tanzania.
Tukupe nini tena mkulima wetu. Kama soko tumekutafutia tena ni soko la uhakika kabisa. Kazi uliyobaki nayo kwa sasa ni moja tu, kuzalisha viazi. Sehemu ya kuuzia wala hutagangaika. Kinasoru East Africa Tanzania Ltd imefanya kazi kwa niaba yako.
Awali tuliegemea kwenye viazi aina ya Mataya na Jewel pekee, lakini kwa sasa, tunaendelea kuwashawishi wadau wetu ili waweze kuchukua na aina nyingine za viazi lishe ili wakulima wengi zaidi waweze kunufaika. Na kwa hili, kwakweli, tunaelekea kufanikiwa.
Tulikuwa kimya kwa muda mrefu lakini ukimya wetu ulikuwa na majukumu mengi na makubwa nyuma ya pazia. Moja ya jukumu tulilokuwa tukishughulika nalo, ilikuwa ni kutafuta barua ya ithibati kutoka kwenye taasisi inayotambulika ili kuwabebea dhamana wakulima ambao mbegu zao hawakuzitoa kutoka kwenye vyanzo vinavyotambulika.
Tunashukuru hilo tuliweza kulifanikisha na tunawashukuru sana wahusika waliyotusaidia.
Vilevile tulikuwa tunaandaa kanzi data ya wakulima wa viazi lishe na hasa wale wakulima ambao viazi vyao viko tayari kwenda sokoni. Hadi sasa tumefanikiwa kupata ekari zaidi ya 200 za viazi lishe vilivyozalishwa bila mkataba wetu na viko tayari kwenda sokoni. Na mashamba mengine zaidi ya ekari 100 ziko kwenye hatua mbalimbali. Na mashamba yote hayo tumeshayatambua na kuyaingiza kwenye kanzi data yetu.
Na juzi kulikuwa na kikao cha bodi kilichojadiri mambo ya uvunaji, upakiji na usafirishaji. Ni namna gani wakulima wavune, wapaki na wasafirishe viazi vyao kutoka shambani hadi kwenye ghala la kukusanyia viazi kabla ya kuvisafirisha kwenda kwenye soko la kimataifa.
Kwenye suala la uvunaji ilijadiliwa kuwa mkulima anapaswa kuwa makini sana kwani haitakiwi kiazi kichubuliwe kwa namna yoyote ile, lakini vile kiazi hakitakiwi kikatwa. Kiazi kinapochimbwa kinapaswa kitoke na ile kamba yake ya kwenye ncha.
Lakini kwenye upande wa upakiji, mkulima anatakiwa kupaki vizuri kwenye kreti maalum za plastiki au mabox ya mbao na si kwenye mifuko ya viroba ya sandarausi au magunia ya katani kama ilivyozoeleka. Vifaa hivyo ndivyo vitakavyotumika kusafirishia viazi kwenda Dsm kwenye ghala maalum lililoandaliwa kwa ajili ya kukusanyia viazi kabla ya kuvisafirisha kwenda kwenye soko letu la kimataifa.
Sasa hivi tuko kwenye hatua za mwisho mwisho za kukamilisha taratibu zitakazowezesha kuanza kwa zoezi la ununuaji wa viazi kutoka kwa wakulima. Na ikiwa wewe ni mkulima na una viazi ambavyo viko tayari kwenda sokoni, tafadhali tutumie sample kwa njia whatsap, chagua viazi vizuri ambavyo havijaliwa na wadudu na viazi hivyo vitatumika kutoa picha ya jumla ya viazi uliyonao shambani kwako. Katika picha za viazi utakazotutumia utapaswa kuonyesha urefu wa kiazi kwa maana ya sentimeta pamoja na uzito wake kwa maana ya Kilogram.
Kama una aina nyingi ya viazi katika shamba lako, basi utachimba viazi kadhaa kila aina kisha utafuata utaratibu wa upimaji wa kila aina ya viazi kama nilivyoelekeza hapo juu na kisha utapiga picha na kututumia kwa njia ya whatsap. Kiazi tunachokitaka kinatakiwa kiwe na wastani wa uzito angalau kuanzia gram 300 hadi 600 kwa kiazi kimoja.
Hiki ndicho kilimo cha viazi lishe. Unaweza kuona kama unasumbuliwa lakini lengo ni kuona kama vinafaa kwa soko letu la kimataifa. Ni muhimu sana kila mkulima akazingatia kanuni za kilimo bora.
Mkulima ataweza kuuza kilo moja ya viazi vyake kwa TZS 800 haijalishi una mzigo kiasi, soko letu ni kubwa sana ndiyo maana kila siku tunaendelea kuhamasisha wakulima wengi zaidi ili waweze kuingia kwenye fursa hii. Fanya kazi upate hela.
Kwa wakulima wapya na hasa wakulima wanaolima pamoja yaani Block farming, tunaendelea kutoa mikataba kwa ajili ya kuwapa uhakika wa soko, vigezo na masharti kuzingatiwa.
Kinasoru East Africa (T) ina fursa nyingi kwenye kilimo biashara, na kwa sasa fursa zilizo tayari ni Kilimo cha Papai aina ya Malkia, Pilipili kichaa pamoja na viazi lishe vyenyewe.
Fursa ya Maboga Vibuyu au Butternut Squash iko njiani inakuja, kwa sasa unafanyika kwanza utaratibu wa kuagiza mbegu zinazotakiwa kwa ajili ya maboga hayo. Kwahakika, kwenye kilimo chetu hakuna kubeti, ukiweka jitihada utapata kadiri ya jitihada yako. Lazima tumuunge mkono Mheshimiwa Rais wetu kwa kutekeleza kauli mbiu yake ya hapa kazi tu kwa vitendo.
Papai moja lenye wastani wa uzito wa kilo moja linanunuliwa kwaTZS 500 wakati Pilipili Kichaa yenyewe ikiwa mbichi inanunuliwa kwa TZS 2000 kwa kilo moja na ile iliyokaushwa inanunuliwa kwa TZS 4000. Shamba la ekari moja lililolimwa pilipili kichaa linatoa si chini ya tani sita kwa wastani wa mivuno mnne.
Na hii ndiyo habari niliyopanga kuwapa siku ya leo.
Kama kuna lolote la ufafanuzi tafadhali tuwasiliane kwa anuani zetu hapo chini.
Aman Ng'oma
Mkurugenzi Mtendaji
Kinasoru East Africa Tanzania Ltd
Msalato Bible
+255767989713, +255655038210, +255786989713
Email: amanngoma@gmail.com
Dodoma
Tanzania.