Mathias Byabato
JF-Expert Member
- Nov 24, 2010
- 1,020
- 691
Wakuu.
Tanzania na Uganda zimesaini mkataba wa mwisho kuanza ujenzi wa bomba la mafuta kutoka Hoima nchini Uganda hadi Chongoleani bandari ya Tanga nchini Tanzania .
Ni heshima Kubwa nchi yetu ya Tanzania kupata fursa hii ya bomba la mafuta kupita nchini Tanzania ambao utapita mikoa 8, Wilaya 24 na vijiji 184.
Kuna faida nyingi sana kama Taifa tutapata kutokana na uwepo wa mradi huu wa bomba la mafuta.
Wakati wa ujenzi Watanzania wengi watapata fursa ya ajira ambapo jumla ya ajira 40,000 zitapatikana. Ajira za ufundi, ulinzi, upishi, usafiri, fursa za malazi, na huduma za kifedha.
Lakini hali ilivyo inaonesha watanzania wapo kimya sana na wenzeetu uganda wamekwisha changamkia fursa .
Mimi nipo hapa Kagera ambapo kutakuwa na kambi mbili za mwanzo kabisa wakati bomba linajengwa nchini Tanzania kutokea huko Uganda.
taarifa zote za mradi huu zinawekwa katika website kuu (kwa sasa) . ile ya mradi ambayo ni
EACOP – East African Crude Oil Pipe Line lakini waganda wanatumia website mahususi na vyombo vyao kusaidia wananchi wao kupeana tarifa mapema.
Fursa zinatangazwa na zitaendelea kutangazwa lakini ukifuatilia vyombo vya habari vya uganda unaona kabisa kuwa ajira nyingi,tenda zinaweza kutupita kama watanzania maana hatuna tarifa mpya za kila siku juu ya kinachoendelea.
Note:Mimi siyo mfanyakazi wa hiyo kampuni wala mwajiriwa bali najitolea kuwakumbusha watanzania fursa hizi kwa lugha rahisi tu ili vijana wetu na jamii yetu ijue kinachokuwa kinaendelea maana inaonesha sisi tunashindwa vitu vinapowekwa kwenye maandishi. maana hadi sasa kuna fursa nyingi zimekwisha tangazwa kupitia website hiyo na magazeti kongwe ya kila siku.
Napatikana pia twitter..>https://twitter.com/bukobaonline?lang=en
======================
1:Kituo cha kupata taarifa za kila siku.
Kituo kikuu kipo nchini Uganda lakini hapa Tanzania kituo kikuu cha kutoa taarifa kipo Jijijini Dar Es Salaam kupitia hii anuanwi.
Total EAST Africa Midstream B.V,
Msasani Peninsula,
429 Barabara ya Mahando, Kitalu D,
S.L.P 38568,
Dar es Salaam,
Tanzania.
Simu: +255 22 2214100/4102/4103
Barua pepe : EACOP.info@total.com
2:Ajira ambazo zimetangazwa hadi march 2021
Ajira zilizotangazwa hadi sasa bonyeza hapa.>> AJIRA BOMBA LA MAFUTA
3:Zabuni ambazo zimetangazwa hadi march 2021
Zabuni mbalimbali zilizokwisha tangazwa had sasa Bonyeza hapa==>> ZABUNI BOMBA LA MAFUTA
Rejeo za JF
Warsha kujadili fursa za bomba la mafuta kutoka Uganda hadi Tanga yafunguliwa
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu Mhe.Jenista Mhagama amefungua warsha ya siku moja ya majadiliano ya wadau kuhusu ushiriki wa Watanzania (Local content) katika sekta ya uziduaji mkoani Dodoma. Warsha hiyo imewakutanisha...
www.jamiiforums.com
Ajira bomba la mafuta kutoka Ohima- Uganda mpaka Chongoleani-Tanga
Ni miezi kadhaa sasa imepita tangu Rais wa Uganda Yoweri museveni na Rais wa Tanzania John Magufuli kusain makubaliano ya ujenzi wa bomba la mafuta katika nchi hizi mbili. Swali ni je, ujenzi utaanza lini? maana tuliambiwa kuna ajira zaid ya elf 10 na vijana wengi wamekaa mkao wa kula kusubir...
www.jamiiforums.com
Ujenzi wa Bomba la Mafuta: Ziara ya Rais Museveni nchini Tanzania - Septemba 13, 2020
Rais Museveni ametembelea tanzania Kikazi === Rais John Magufuli wa Tanzania na Rais Yoweri Museveni wa Uganda wamesaini makubaliano ya kuanza ujenzi wa Bomba la Mafuta ghafi kutoka Hoima, Uganda hadi Chongoleani mkoani Tanga, Tanzania Rais Magufuli: Tumeshuhudia uwekaji wa saini wa ujenzi...
www.jamiiforums.com