Furaha ya Migogoro ya Serikali

Furaha ya Migogoro ya Serikali

Wanamitandao? So hao wanamitandao wana ndugu ambao wananchi wapo vijijini?

Kwa hiyo hawa wanamitandao wapo mjini si ndo hivyo?

Hivi hawa wanamitandao wanaishi wapi
Nikusahihishe sio wananchi, sema wanamitandao, hiki tunachoongea haps jaribu kumpigia simu ndugu yako kule kijijini mlize kuhusu ndege kukamatwa atakushangaa. Ujinga tulio nap sisi wanamtandao hatujui watanzania wako wapi.
Nikirudi kwenye mada yako, uwezi kuisemea vizuri serikali kama ulikuwa una makandokando au mnufaika Wa makandokando kisha serikali ikakata mirija au ukafukuzwa. Chunguza vizuri wote wale wanaotukana na kuisema ovyo mitandaoni ni wahanga. Watataka wawe na hati miliki ya Tanzania, rais anavyo fanya mageuzi ya kimfumo kuziba mianya ya upigaji roho zinawauma, hakuna linguine zaidi ya kuwa mijitu yenye roho mbaya wanataka watanzania walipe ada za shule za milioni walipe private hospital wakati hawana uwakika Wa milo mitatu. Watatukana sana ila wameshikwa korodani na koleo.
 
Kutokana na Ndege yetu kuzuiwa na mahakama kuu nchi South Africa, nimepitia mitandao ya kijamii kusoma maoni ya watu ambao ni wananchi na wanufaikaji pengne wa kila miladi inayoihusu nchi.

Jambo la kusikitisha watanzania wanafurahi kwa kitendo cha ndege yetu kuwekewa kizuizi.


Kabla sijawalaumu nimejiuliza maswali

1. Kwanini wanafurahi serikali inapokuwa kwenye migogoro fulani?

Swali hili limekuja baada ya kujiridhisha kuwa si hili tu la Air Tanzania bali imekuwa ni jambo la kawaida wananchi kufurahi pale nchi (serikali) inapokuwa kwenye migogoro.


2. Je Serikali inajifunza nini kupitia wananchi wake wanapofurahi pale inapokuwa na migogoro ya aina hii?


3.Je kama nchi tunapaswa kufurahi au tuwe na namna nyingne ya kufikisha ujumbe kwa serikali ili kuwajibika inavyopaswa?

4.Je Serikali inajua chanzo pelekewa kwa wananchi kufurahia pindi inapokuwa na migogoro? Kama ndio je haioni kutafta suluhisho la tatizo?

Pamoja na maswali yangu lakini Leo ningependa kujua swali msingi ni Kwanini tunafurahi nchi inapoingia kwenye migogoro?
Tunarimia meno!!
 
Matumizi mabaya ya Kodi zetu,

Majuzi Prof Kabudi alikuwa China kufanikisha Mkopo wa Mabilioni.

Sasa subiri siku China nao wakamate Mali zetu.

Tatizo ni matumizi sahihi ya hiyo Mikopo haimnufaishi Mwananchi moja kwa moja, mwisho wa siku yeye ndiyo mlipaji.
 
Kimsingi nilitaka kujua je watu wanafurahi kwa sababu pengne hawanufaiki na hiyo miladi au kuna tatizo lingne linalopelekea haya tunayoyaona...

Sidhani kama nchi kama marekani hufurahi pale nchi inapoingia kwenye migogoro...

Mimi nilitegemea wananchi kulaani na kuitaka serikali kutafta majibu ya haraka ya tatizo na ndege yetu kuachiwa na si kufurahi..

Nilitegemea serikali kutoa majibu ya haraka kwa sababu ya uwajibishwaji wa wananchi...
Nadhani watu wengi wanafurahia matatizo yanapotokea kutokana na nguvu kubwa inayotumika kutangaza baadhi ya mambo ambayo ni kawaida,
Kingine kuonekana kana kwamba waliotangulia hawakufanya lolote, hivyo wengi wana roho ya wacha tuone
 
Kuna mambo yanasiktisha sana...

Wananchi kufurahia serikali yao inapopatwa na migogoro na nchi zingine... nadhani ni kwa sababu serikali yenyewe ndani tayari ina migogoro na wanachi wake...

Ni sawa na baba awe mbabe kwa familia yake, siku familia wakisikia huko nje baba nae kataitiwa, lazima watasema afadhali nao kidogo apitie ghadhabu kama anazotupatia sisi...



Cc: mahondaw
 
Back
Top Bottom