Funza hutokea wapi?

Funza hutokea wapi?

Ukipata majibu ya chawa wanatokea wapi, ndipo na majibu ya swali lako litapatikana hapo!!
 
Ndio maana rasta hali nyama, huwezi kuta mboga ya majani mfano mchicha ukioza ukatoa funza, niko tayari kuthibitishiwa vinginevyo, nahisi vyakula ama viumbe vyenye damu ndio huwa na funza
 
Hili swali ni pasua kichwa. Nilijiuliza nilipokua drs la 7. Wataalamu fungukeni mtutoe tongotongo machoni
 
Sikubaliani na wanaotuaminisha kuwa ukiona funza basi lzm kuna inzi au mdudu mwingine katagia mayai hapo. mi japo sio msomi naweza kukubari kuwa kuna aina fulani ya funza kweli wanaweza kuwa ni hatua fulani ya mdudu katika ukuaji, lkn sio kila funza lzm atasababishwa na mdudu mwingine eti katagwa kama mayai. nilijaribu kuweka kipande cha nyama mbichi ndani ya chupa,kisha nikafunika vizuri bila kuruhusu nafasi ya hewa. Lkn baada ya Sikh kadhaa niliona funza kibao ndani ya chupa.
 
Ndio maana rasta hali nyama, huwezi kuta mboga ya majani mfano mchicha ukioza ukatoa funza, niko tayari kuthibitishiwa vinginevyo, nahisi vyakula ama viumbe vyenye damu ndio huwa na funza

Mkuu Rasta hawali Nyama si kwa sababu hiyo,aidha si kweli kwamba Eti mboga majani hazishikwi na funza zikioza,Mkuu kaa mkao wa kula nitaleta Somo hapa JF muda si mrefu,ila ni Full Sayansi na ni Full Biology.
 
Hili swali ni pasua kichwa. Nilijiuliza nilipokua drs la 7. Wataalamu fungukeni mtutoe tongotongo machoni

Mkuu majibu yake unaweza kuyapata ukisoma Biolojia kwenye topic iitwayo Evolution,hasa theories of Evolution.Kuna jamaa alifanya Majaribio mengi sana ya Kisayansi kuthibitisha utafiti wake.
 
Sikubaliani na wanaotuaminisha kuwa ukiona funza basi lzm kuna inzi au mdudu mwingine katagia mayai hapo. mi japo sio msomi naweza kukubari kuwa kuna aina fulani ya funza kweli wanaweza kuwa ni hatua fulani ya mdudu katika ukuaji, lkn sio kila funza lzm atasababishwa na mdudu mwingine eti katagwa kama mayai. nilijaribu kuweka kipande cha nyama mbichi ndani ya chupa,kisha nikafunika vizuri bila kuruhusu nafasi ya hewa. Lkn baada ya Sikh kadhaa niliona funza kibao ndani ya chupa.

"Bila kuruhusu nafasi ya hewa"? ulitumia kifaa gani ku eleminate air iliyokuwemo ndani ya chupa kabla huja introduce hiyo nyama mbichi?.Lazima kulikuwa na air ndani ya chupa na air imebeba bacteria wengi sana waliosaidia kuozesha hiyo nyama.
 
Du, sikutaka kuchangia nikisubiri majibu ya kuridhisha lakini ola.
OK, Kama unasema kuwa funza ni hatua ya ukuwaji wa mdudu kama nzi (nakubaliana na hili) kwanini hao wadudu wasubiri kwanza mpaka kitu kioze ndo watokee? tunajua kuwa inzi wanataga majai popote, nimesafiri kwa mwezi nimeacha nyumba yangu safi, kwanini baada ya kurudi sijakuta mafunza kila mahali? nimechemsha nyama yangu vizuri na kbla hata kupoa sana nimeweka kwenye friji safi, kesho yake nikasafiri kwa mwezi mzima na huku nyuma kumbe luku imekisha, nimekuta nyama imeoza na kutoa wadudu je wadudu waliingiaje?
 
sijui niandike hapa kitu au niache nisiandike maana hao funza funzaaa
 
Ndio maana rasta hali nyama, huwezi kuta mboga ya majani mfano mchicha ukioza ukatoa funza, niko tayari kuthibitishiwa vinginevyo, nahisi vyakula ama viumbe vyenye damu ndio huwa na funza

siyo kweli mkuu..nikatakata mboga za majani..nikazisahau nilikuta funza kibao baada ya 2 days tu!!
 
Umefunika chakula vizuri kabisaa, hakuna nafasi ya kuingia mdudu yeyote, ila bahati mbaya ukasahau kukiweka kwenye friji.

Siku kadhaa zinapita unafunua chakula unakuta kimeharibika na funza tele wamejaa, wametokea wapi hawa funza?

Nyama ipo ndani ya mfuko au chombo bahati mbaya imeoza unakuta funza kibao, tena wakubwa, wanatokea wapi hawa funza?

Hawa funza huwa wanatokea wapi? ninajiuliza mara nyingi sijawahi pata majibu!!
wewe si mathematics hebu tueleze inakuaje bana acha masihara
 
Bacteria uishi hewani na ndio chanzo cha hao funza. ..hata mdomoni kuna normal floral ambao kimsingi wanabadilika na kuwa funza kama watakuwa disturbed
 
Mimi nilidhana unaongelea funza wa kwenye miguu (Tunga penetrans) kumbe ni maggots? Hao ni larvae wa nzi ambao ili wazaliwe lazima hicho chakula kuna wakati kilitembelewa na nzi kabla ya kufunikwa.

Vinginevyo haiwezekani kuwa na maggots ila chakula kitaoza ama kwa sababu ya bacteria au kuvunjwa vunjwa na enzymes.
 
microbes wanagrow kwenye hicho chakula na wanasababisha decomposition.Microbes huwezi waona kwa macho but they are every where
 
Ndio maana rasta hali nyama, huwezi kuta mboga ya majani mfano mchicha ukioza ukatoa funza, niko tayari kuthibitishiwa vinginevyo, nahisi vyakula ama viumbe vyenye damu ndio huwa na funza

Mkuu hapo mdomoni una wadudu wengi sana wanaitwa trichomonas temax na gangivalis
 
nami nashangaa sana hawa wadudu hata ununue kama nyama safi uiweke hata ghorofa ya kumi tena uifunge vizuri baada ya siku kadhaaa lazima funza wataibuka tu,na hata kama nzi hakuna[/QUOTEinawezekana nzi alitaga mayai yake ikiwa buchani mkuu bacteria hawawezi geuka funza hata siku moja
 
"Bila kuruhusu nafasi ya hewa"? ulitumia kifaa gani ku eleminate air iliyokuwemo ndani ya chupa kabla huja introduce hiyo nyama mbichi?.Lazima kulikuwa na air ndani ya chupa na air imebeba bacteria wengi sana waliosaidia kuozesha hiyo nyama.

Kumbuka mada si nyama kuoza bali funza kutokea.labda uniambie bacteria ndio funza.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom