barafu
JF-Expert Member
- Apr 28, 2013
- 6,739
- 32,916
Lukuvi majanga teh teh teh
ha ha ha ha jamaa majanga!toka achaguliwe 1995 hakuna alilofanya
Lukuvi majanga teh teh teh
Pamoja na Mbagala, mie ukweni kwetu ni Madesa-nina nyumba na shamba. Mbunge wangu wa jimbo la CHALINZE ni SAID BWANAMDOGO! Huyu nilishawahi kumleta jamvini kumlalamikia. Manake hasikiki bungeni, iwe kwa hoja binafsi, swali la msingi wala la nyongeza. Jimboni kwetu HAKUNA mabadiliko yoyote. Wanajimbo BADO wanaendelea kulima kwa jembe la mkono kwa karibu 100%, hakuna shule za maana za msingi na sekondari ('O' na 'A')--zilizopo ni mbavu za mbwa, hakuna maabara, vitabu wala walimu wa kutosha; hakuna jitihada za kutosha kusaidia kusambaza umeme; maji ya mto wami yanapita Tu, hakuna jitihada za kuanzisha kilimo cha umwagiliaji. Pia michezo ni HOIIII!! Kwa sasa wanajimbo wameamua kuzamia katika ulevi wa kupindukia wa pombe za kienyeji. Hili jimbo la Chalinze ni kama lipo wazi tu? Kumbuka jimbo hili ndio limemtoa rahisi wa sasa wa JMT.
pole sana mkuu maana ndo choir master kwenye ile bendihuyo huyo.
Nipo ukonga naombeni mnijuze jina la mbunge wa huku.Nisaidieni wanajfhahahaha. Ni kilaza zaidi ya serurope kwa kweli.. Hata darasa la saba hakuwah kufika. Ni majanga yaani.
Daah.,mi ndo humu nimegundua yaweza ikawa jimbo zima mimi tu ndo naijua JF...Mi wangu ni yule mwenye kiburi,mzee wa kubetua mdomo kama anasutana..wanamuita Mzee wa kanuni,kifungu cha 65(b) fasili ndogo ya 4 ukurasa wa 64 wa kitabu cha Kanuni za kudumu za Bunge...huyu jamaa anatudharau sana...akienda jimboni hataki maswali,ukimuliza swali anakuitia polisi wakunuse mdomo,anasema huwezi kuwa jasiri ivo kumuliza maswali kama hujaswata ulanzi na kuvuta ganja!...anakutia ndani kwa sheria ya Vinywaji Baridi na Vileo...eti sheria hiyo haimtaki mwananchi kunywa pombe isiyo na muhuli wa TBS....Ajabu wakati wa kura za maoni anawahonga watu na vijombero vya ulanzi,mana huwa hatupigi kura za Mbunge,akipita tu kura za maoni hana mpinzani anapita bila kupingwa!!Kama unataka kile kimnyama kinyegere kije kuvunja mlango kikwarue chukua form umpinge kwa upinzani
Mimi pamoja na kuwa ni mkazi wa Mbagala, ukweni kwangu ni Madesa-Jimbo la Chalinze. Nina shamba na nyumba huko. Mbunge wetu huko ni SAID BWANAMDOGO. Kama mwezi hivi uliopita nilishamlalamikia humu jamvini, manake jimbo letu hilo ni kama lipo wazi. Manake huduma za afya ni kama hakuna kabisaaa, zipo duni mno, hadi watu ni kama wameshahalalisha huduma za 'kienyeji' style; Mto wami unapita katika vijiji vingi, lakini hakuna mkakati wowote wa kuanzisha kilimo cha umwagiliaji; Kilimo kwa karibu 100% kinategemea jembe la mkono, hata teknolojia za jembe la kukokotwa na ng'ombe hakuna, matrekta ni ya kuhesabu nk; Shule nyingi ni hoi kabisa! hakuna maabara, madarasa, mabweni, vitabu na waalimu wa kutosha; michezo hakuna kitu kabisa; NA hakuna jitihada za wazi za kusambaza umeme vijijini. Zaidi bungeni hasikiki kabisa, iwe katika hoja binafsi, maswali ya msingi wala maswali ya nyongeza! Zaidi hajaweza hata kujitokeza na kukukutana na wadau wa jimbo ili kubadilishana mawazo tufanyeje ili kuendeleza jimbo letu. Kwa sasa wanakijiji wamezamia kabisa katika unywaji pombe za kienyeji! sijui ni stress au vipi? Kumbuka hili ndio jimbo ambalo tumetoa rais wa sasa wa JMT.
Hahaaa mkuu kumbe tuko jimbo moja.Nimeipenda hiyo yaani badala yakusambaza maji yeye kutwa kucha anasambaza namba za viongozi ili watukanwe utadhani hao ndio waliotuomba dhamana 2010.
Mwe! Wa kwangu anamabasi tu! Hana muda na maisha ya raia, ila anagawa viposho vijiweni. Yupo mpakan kati ya Moro na Dom...