Funguka Mbunge Wako Yukoje?

Funguka Mbunge Wako Yukoje?

Mbunge wangu na mkubali sana Tundu Lissu sema CCM wanambania sana kuleta maendeleo jimboni kwake.
 
Wakuu,
Kama mwananchi wa TZ ninawakilishwa katika nyumba ya kutunga sheria na mbunge ambae alipata kura mingi kumtosha akatuwakilishe,cha ajabu ni analala,kawa bubu,haulizi swali wala hajibu lolote,hana hata ile kunyoosha mkono!
Najuta kuwakilishwa na jamaa. Jamaa anamiliki magari ya dar-moro yana rangi nyekundu.Ata kutaja jina naona uvivu..
Aya wakuu waliokula hasara kama mimi tufunguke!
Kama ni huyo sitaki hata kumsikia, si ndiyo yule aliyekosa penalti ya mwisho usiku wa matumaini pale National Stadium.

CC: Amavubi.
 
Hongereni mlio na wabunge wa ukweeeeli... Vp huyu mnamjua bw Agustino masele manyanda-mbogwe-geita aiseeee huyu ni janga la kitaifa... Tuna omba sana nguvu ya umma izamie pande hzo maana jimbo liko waz kabsa...
 
Wangu ni waziri lakini ameshakaa kwenye wizara zaidi ya nne sasa ktk awamu hii ya nene ya kiongozi wetu pendwa Dr. JK, sasa sijui kwanini amekuwa akihamishwa hamishwa, sijui ni utendaji uliotukuka au uliotokota!!!!!!! Wakati wabunge wakiongozawa na ZZK wakitaka kupiga kura ya no of confidence kwa PM na kupelekea mawaziri kadhaa kupigwa chini, huyu wa kwangu alikoswa koswana panga pangua kipindi akiwa wizara ya kilimo hivi sasa yupo Maji. Kabla ya wizara hizo aliwahi pia kupitia Elimu na Maliasili. Huku jimboni watu wamechoka, wamepigika ila kikubwa kinachotukera ni DHARAU kwa apiga kura wake. hana muda wa kumsikiliza mwananchi. Pamoja na kuwa kiongozi wa juu kabisa serikalini ktk sekta ya maji, jimboni kwake kina mama na watoto wanatumia saa zaidi ya 8-10 kuteka maji kwa siku. Bora ingekuwa hivyo halafu ni salama, mungu atuepushe, 2015 kwa huyu jamaa ni mbali sana, hata mtangulizi wake analitambua hilo.
 
kuna hiki kirusi kinaitwa juliana shonza ......................................serukamba yeye
 
mi wa kwangu toka nazaliwa enzi za nyerere hadi sasa yupo mjengoni ila kwa sasa mafisadi papa wamempa u monitor katika kijiwe cha mipasho inayoongozwa na viti maalum. Ana bahati kasema hagombei tena.
bi kidude nini?
 
MIMI WANGU NI YULE KIBARAKA MKUU WA LOWASSA (aka mwizi wa kura au mgawa nchi kwa ukabila). SIJUTI KWASABABU HATUMPA KURA BALI WALIIBA NA KUNUNUA na mkubwa wake aka FISADI MKUUU
 
Namshukuru mbunge wangu he is young but anapaticipate c sawa na aliyepita!mine n Joshua Nassary
 
Duu! Lusinde janga la mtera hata nashindwa kumwita mbunge wangu! Msiomfahamu ni yule aliyetukana alumeru na igunga, ni yule aliyesema nitaongoza wananchi kung'oa nguzo za umeme, ni yule aliyetuahid gari la kubebea maiti et wasiumie badala ya ambulance ya wagonjwa,ni yule aliyetuahid majokof ya kuhifadhia maiti, anapenda tufe? Ni yule wa darasa la 4 la zaman,ni mc wa malecela, ni mlopokaji, ni yule anayetukana wafanyakaz hasa walim, ni yule ambaye toka uchaguz hajakanyaga kijijin kwangu,ni yule aliyemwambia jk amsamehe kwa uropokaj kwan ni mgonjwa anayeanza kupona,kimaendeleo hajafanya lolote.

Duh wako naona anamatatizo kuliko wabunge wote!
 
Mbunge Wangu Niliyempigia Kura Ni Mh, Jembe, Kamanda La Ukweli, TUNDU LISSU, Japo Kwa Sasa Nipo Geita Mjini Kwa Mcheza Rumba Anaitwa Max (gambaz)
 
Pamoja na Mbagala, mie ukweni kwetu ni Madesa-nina nyumba na shamba. Mbunge wangu wa jimbo la CHALINZE ni SAID BWANAMDOGO! Huyu nilishawahi kumleta jamvini kumlalamikia. Manake hasikiki bungeni, iwe kwa hoja binafsi, swali la msingi wala la nyongeza. Jimboni kwetu HAKUNA mabadiliko yoyote. Wanajimbo BADO wanaendelea kulima kwa jembe la mkono kwa karibu 100%, hakuna shule za maana za msingi na sekondari ('O' na 'A')--zilizopo ni mbavu za mbwa, hakuna maabara, vitabu wala walimu wa kutosha; hakuna jitihada za kutosha kusaidia kusambaza umeme; maji ya mto wami yanapita Tu, hakuna jitihada za kuanzisha kilimo cha umwagiliaji. Pia michezo ni HOIIII!! Kwa sasa wanajimbo wameamua kuzamia katika ulevi wa kupindukia wa pombe za kienyeji. Hili jimbo la Chalinze ni kama lipo wazi tu? Kumbuka jimbo hili ndio limemtoa rahisi wa sasa wa JMT.
 
Mimi mbunge wangu nasikiaga anaishi Dar akijaga jimboni analala HOTEL mara ya Mwisho alikuja mwaka 2010 huku,mimi sijui anacho kiwakilisha huyu mtu maana hata Bungeni kwenyewe simwonagi Alipitaga bila kupingwa huyu Najuta Kumfahamu.
 
wa kwangu naogopa hata kumtaja ...TLP mmmh!!! :sad:
 
Mbunge wangu ana sifa hizi:
i.Ni mbunge aliyekimbia na masanduku ya kura wakati wa uchaguzi

ii.Mbunge aliyejenga nyumba yake kwenye kiwanja chetu cha kujenga soko

iii.Mbunge aliyetangazwa na Fuime kwa maagizo ya JK

iv.Mbunge aliyetangazwa baada ya kuzimwa umeme

v:Mbunge ambaye jimbo lake lina shida ya maji kuliko yote hapa mjini Dar na anatamba hajali maana
hatukumchagua kwani alishinda kwa pesa yake'

Ana sifa nyingi mbovu lakini ngoja niishie hapa maana mbunge wetu mwenyewe afya yake si nzuri sana

 
Back
Top Bottom