Funguka Mbunge Wako Yukoje?

Funguka Mbunge Wako Yukoje?

Mbunge wangu ana sifa hizi:
i.Ni mbunge aliyekimbia na masanduku ya kura wakati wa uchaguzi

ii.Mbunge aliyejenga nyumba yake kwenye kiwanja chetu cha kujenga soko

iii.Mbunge aliyetangazwa na Fuime kwa maagizo ya JK

iv.Mbunge aliyetangazwa baada ya kuzimwa umeme

v:Mbunge ambaye jimbo lake lina shida ya maji kuliko yote hapa mjini Dar na anatamba hajali maana
hatukumchagua kwani alishinda kwa pesa yake'



Basi mkuu futa machozi ile nafasi naamini F,mpendazoe alipita kwa 2/3
 
Its a best n constructing thread yan huwez Ruka kusoma hata post moja...wel mbunge wangu ni mbunge wa mleta uzi kwa maana ya mohamed abdulaziz abood,mleta mada mbunge sio kupiga kelele bungen jimbon hali mbaya,kama hukai moro tuulize sisi anayofanya abood nadhan hakuna mbunge aliyetangulia aliyefanya hata robo ya anayofanya abood,ulishawahi msikia dewji anaongea bungeni?sasa nenda kaulize jimbon kwake mambo anayofanya...niwape heko pia walio mpigia kura Deo Filikunjombe yan dah ni mbunge ambaye ni bora na namkubali kupita wote popote ulipo mbunge mzalendo Deo filikunjombe shkamoo yako....KIMBANGU
 
wangu ni jeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeembe G.LEMA:kev:
 
mbunge wetu ni kijana. anavaa nguo za kijani. japokuwa wenye rangi yao ya kijani hawamtaki coz yeye ni msema ukweli. hamung'unyi maneno;

ni jasiri na ni mtetezi wa wanyonge. anatokea kule kwenye makaa ya mawe na chuma cha liganga na nchunchuma; deo filikunjombe - ni kipenzi chetu wana ludewa.

filikunjombe ni nuru yetu ya matumaini ludewa.
 
Mi Mbunge wangu naona hata aibu kumtaja ila inabidi kwa mujibu wa thread hii. Anaitwa Ndugu....ayiiiiiii!!! Hana udugu huyu. Kila siku anaongea pumba na kugombana na Kisu ( Lissu). Nikisikia kaongea kitu huwa najificha kwanza ili wenzangu wasinicheke!!! 2015 mbali sana.

Atakuwa JOB NDUGAI tu, hakuna mwingine mwenye vita vya wazi na Tundu Lissu. Pole sana mkuu...!!!
 
Wa kwangu ni mbinafsi, visasi na chuki sana kwa wanaomhoji utendaji wake, alijenga ofisi kubwa ya spika jimboni kwake kama vile atakuwa spika wa maisha. Kwa ufupi HAFAI.

Samwel Sitta....mmhh huyu kweli ni mnafiki namba moja....hana lolote.
 
Mzee WAPIGWE ndio jembe langu.

Kaka una hasara kweli...mbunge wako mara alie, mara atake kuondolewa kwa kura za ZITTO, mara LIWALO NA LIWE.....Leo anasema WAPIGWE TU...HAKUNA JINSI....Duu...karibu Mpanda Mjini kwa Jembe la Ukweli SAID AMOUR ARF...FULL MAENDELEO MPANDA MJINI...KITU CHA UKWELI.
 
Dah ! Naomba kukiri kwamba naishi Tandilka Mwembeyanga , sasa kwa bahati mbaya nikajikuta nipo jimbo la Temeke na Mbunge wangu akawa Abbas Mtemvu , kwa kweli kikubwa alichofanya Mh Mbunge ni kusimamia mauzo ya kata ya Kurasini kwa wachina , lengo likiwa ni kujenga viwanda kwa ajili ya kutengeneza vijiti vya kuchomea mishikaki , toothpick , cotton buds na toilet paper , katika hili ameshirikiana kwa dhati na diwani wa kata hiyo Mh Wilfred Kimati , kingine labda ni zile kazi za ndani alizowatafutia akina dada wa Tmk huko uarabuni , kwa leo ni hayo tu .
 
Khaa!!! mie wangu ni jembe kupitiliza, jeshi la mtu mmoja, mwiba mkali wenye sumu hasa kwa wapinzani wake na anawapiga hanyahanya usiku kucha hawalali wanakesha wakimuombea mabaya lakini harudi nyuma. Wengine mnamwita Jonas :tape:
 
Hahaaa mkuu kumbe tuko jimbo moja.Nimeipenda hiyo yaani badala yakusambaza maji yeye kutwa kucha anasambaza namba za viongozi ili watukanwe utadhani hao ndio waliotuomba dhamana 2010.

We naona 0713 inawasha,mpaka wa ku-"LINAHLIZE" ndo utaongea point...Mlokole usie na misimamo!umeambiwa JJMnyika ndo ana "koki" ya kufungulia maji?
 
Wa kwangu ni mbinafsi, visasi na chuki sana kwa wanaomhoji utendaji wake, alijenga ofisi kubwa ya spika jimboni kwake kama vile atakuwa spika wa maisha. Kwa ufupi HAFAI.

Habari jirani,mi Kapuya hata sijui inakuwje anarudi kila uchaguzi
 
Daah.,mi ndo humu nimegundua yaweza ikawa jimbo zima mimi tu ndo naijua JF...Mi wangu ni yule mwenye kiburi,mzee wa kubetua mdomo kama anasutana..wanamuita Mzee wa kanuni,kifungu cha 65(b) fasili ndogo ya 4 ukurasa wa 64 wa kitabu cha Kanuni za kudumu za Bunge...huyu jamaa anatudharau sana...akienda jimboni hataki maswali,ukimuliza swali anakuitia polisi wakunuse mdomo,anasema huwezi kuwa jasiri ivo kumuliza maswali kama hujaswata ulanzi na kuvuta ganja!...anakutia ndani kwa sheria ya Vinywaji Baridi na Vileo...eti sheria hiyo haimtaki mwananchi kunywa pombe isiyo na muhuli wa TBS....Ajabu wakati wa kura za maoni anawahonga watu na vijombero vya ulanzi,mana huwa hatupigi kura za Mbunge,akipita tu kura za maoni hana mpinzani anapita bila kupingwa!!Kama unataka kile kimnyama kinyegere kije kuvunja mlango kikwarue chukua form umpinge kwa upinzani
 
Mbunge wangu ni mnene sana, anaongea kwa sauti ya kupayuka, anaongoza kwa kukata mauno na kuneng'ua majukwaani, aliwahi kumtungia baba taifa nyimbo za msiba kabla hajafa and recently kajituliza kimahaba kwa kabinti kadogo ka bongo movie.!!
Jina mtataja wenyewe me naona mpaka kichefuchefu.
 
jimbo langu CDM na NCCR wamedhihirisha ubinafsi na kwamba wapo tayari kutawaliwa milele,wamechakachuana hatimaye wameiachia CCM nafas zote za.M/kiti na Makamu wake

Polee sana aisee, ndio shida ya chama pandikizi mie mbuge wango dogo janja arumeru taifa huru vyanzo vya maji vinatoka kwetu. Ingawa nipo kwa mbuge aliyedanganywa na magufuli watajenga lami mwaka huu wa fedha wakati hata upembuzi wa barabara bado. zee moja la TISS
 
Daah.,mi ndo humu nimegundua yaweza ikawa jimbo zima mimi tu ndo naijua JF...Mi wangu ni yule mwenye kiburi,mzee wa kubetua mdomo kama anasutana..wanamuita Mzee wa kanuni,kifungu cha 65(b) fasili ndogo ya 4 ukurasa wa 64 wa kitabu cha Kanuni za kudumu za Bunge...huyu jamaa anatudharau sana...akienda jimboni hataki maswali,ukimuliza swali anakuitia polisi wakunuse mdomo,anasema huwezi kuwa jasiri ivo kumuliza maswali kama hujaswata ulanzi na kuvuta ganja!...anakutia ndani kwa sheria ya Vinywaji Baridi na Vileo...eti sheria hiyo haimtaki mwananchi kunywa pombe isiyo na muhuli wa TBS....Ajabu wakati wa kura za maoni anawahonga watu na vijombero vya ulanzi,mana huwa hatupigi kura za Mbunge,akipita tu kura za maoni hana mpinzani anapita bila kupingwa!!Kama unataka kile kimnyama kinyegere kije kuvunja mlango kikwarue chukua form umpinge kwa upinzani

Lukuvi majanga teh teh teh
 
Back
Top Bottom