FULL TEXT: Hotuba ya Lema bungeni

FULL TEXT: Hotuba ya Lema bungeni

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Waziri Mkuu wakati anahitimisha mjadala kuhusu bajeti ya Ofisi yake, alikubaliana na ushauri wa Kambi rasmi ya Upinzani, na kuahidi kwamba serikali itaanzisha mahakama ya kuchunguza mauaji hayo, yaani “Coroner’s Court”, kwa mujibu wa Sheria ya Uchunguzi wa Vifo, (The Inquest Act) Sura ya 24 ya Sheria zetu.

Mheshimiwa Spika, Kambi rasmi ya Upinzani inachotaka sasa ni kuona utekelezaji; Je, ni lini Waziri mwenye dhamana atatangazauteuzi wa kuundwa kwa mahakama hiyo katika Gazeti la Serikali, ili wauaji wahukumiwe? Tunataka uchunguzi ufanyike haraka ili haki iwe itendeke mapema.

Kutokuwepo coroners court ni mfano wa viongozi kushindwa kutawala nchi, hii taasisi ipo kisheria kinachotakiwa ni waziri wa sheria kuandika majina ya coroners na kupeleka Governement Printers ili iwe gazetted na hapohapo wanaanza kazi.

Je nu kweli tunahitaji upinzani kukumbusha hili?

Imekuwa ni sehemu ya utendaji wa nchii hii,

Hatuna wakuu wa mikoa kwa baadhi ya mikoa tunaona sawa tu, tume nyingi zimekwisha muda hakuna anayejua kukumbusha ili watu wateuliwe yaani mambo ya nchi hii yanenda mjinimjini
 
big up jembe Lema,anae kataa yaliomo kwenye hotuba ni 'cognitive disability'kama anabisha aje nimpime nimpe marisult yake....
 
Hapa sasa ndo twasema umakini wa chama cha upinzani na wabunge wenye hoja za nguvu kama hizi. Big up CHADEMA
 
Hii ni hotuba iliyojaa uhalisia kulingana na hali halisi ya usalama kwa sasa. Nawashukuru wote walio nyuma ya maandishi hayo na nimpongeze Mhe Lema kwa kuwa na ujasiri wa kuisoma.
 
Kumbe huyu speaker ndio mchochezi, mbona sini suala la uchozi kwenye hii hotuba. Tukumbuke kwamba kinga ni bora kulika tiba. Haya ni mawaidha mazuri tu, wala hakuna cha kuondoa kwenye hii hotuba.
 
Wenye macho wameona, wenye masikio wamesikia - We need change kabla ya nchi haijaangamia kwa ufisadi
 
Hongera mh lema usirudi nyuma tuko na wewe bega kwa bega. People's powerrrr
 
Hongera mh lema usirudi nyuma tuko na wewe bega kwa bega. People's powerrrr
 
Hii paragraph imenifurahisha sana Chadema wanajua target big up Lema

Kwa maana nyingine ni kwamba siku hiyo hatakuwepo wa kwenda kuwapiga mabomu kwa kuwa hata askari wenyewe watakuwa kwenye hayo maandamano!!!

Tiba
 
Hii ni hotuba iliyojaa uhalisia kulingana na hali halisi ya usalama kwa sasa. Nawashukuru wote walio nyuma ya maandishi hayo na nimpongeze Mhe Lema kwa kuwa na ujasiri wa kuisoma.
Tunampongeza yeye na wale wote waliohusika kuindaa maana hakika itakuwa imetumia vichwa vya watu kuiandaa
 
Hotuba ya kuandikiwa Lema anaitoa wapi akili hiyo ya kuandika hotuba! Bogus yule kaandikiwa tu
Lema yupo kwenye serikali kivuli ya cdm inayofanya mambo yake kwa pamoja na kwa umakini mkubwa ndio maana unaona hotuba hii imevuta hisia za watu wengi, hata ungeandikiwa wewe ungepata ujasiri wa kuisoma neno kwa neno? Unakumbuka ripoti ya richmond iliandaliwa na watu wangapi na ilisomwa na nani bungeni? Sifa zilimwendea aliyekuwa tayari kuisoma na pia kamati nzima, kwani huko kwenu (ndani ya magamba) hakuna anayejua ukweli au tatizo ni kuusema hadharani panapohusika?

Fungua macho na akili yako ujue tunakoelekea, woga, kujipendekeza sio siasa za cdm ndio maana hotuba imekuwa msumari wa moto kwenye kidonda.
 
CHADEMA, kwa mtaji huu sisi wananchi tumewasoma, tumefurahi kupindukia na hivyo jawabu letu kwenu ni KUWAONGEZEENI WABUNGE WENGI ZAIDI tangu sasa kwenda mbele ili hii kazi zuri mkaikamilishe uzuri zaidi na kuteketeza kabisa hii hulka ya UFISADI wa CCM nchini.
 
Hii hotuba inamgusa mwananchi moja kwa moja.Ndio mambo ya kawaida kabisa kwenye maisha ya watanzania.Nashangazwa sana na mgamba kuwa out of touch na kusema kuwa ukweli huo kwenye hotuba ni kuchochea vurugu.Nimefurahishwa sana na hotuba hii ambayo naamini kuwa ni ya kihistoria.Imenigusa sana kwasababu imezungumzia hali halisi ya maisha ya mtanzania especially kuhusiana na haki ambapo alim quote MLK kwamba ndiyo yenye ku determine amani.

Yaliosemwa kwenye hotuba ni mambo wanayokumbana nayo watanzania kwenye maisha yao ya kila siku.Na nimegunduwa kuwa serikali ilijenga taifa lenye wananchi wenye nidhamu ya woga kwa makusudi kabisa.Na bado wanataka ku maintain hali hiyo.Ndiyo maana hawataki wananchi wasikie hotuba hizo,si kwamba wananchi hawayajui yaliyosemwa,bali wamepata wa kuwasemea na ndiyo wanayotaka kusikia huko bungeni,mambo ambayo yanawagusa kila siku kwenye maisha yao.kwamba ni nini kianyike kuyabadili ili waweze kuishi kama binadamu wa kawaida wenye furaha na wenye kuwa proud of their country.Wananchi wana haki ya kusikia na kufanya maamuzi ya nini kifanyike,waweze kutambua kuwa kuwa things can be done in many different ways.

Ni kweli kabisa watanzania wengi wameshaona kama maisha hayo ni utamaduni na hawaoni ni kwa njia gani utamaduni huo utakomeshwa.Mfano rushwa ni jambo la kawaida sana kwenye maisha ya watanzania.Rushwa ni everywhere.

Hakuna kiachopatikana bila rushwa hata kama ni haki yako.Hakuna haki kabisa kwenye maisha ya kawaida ya mtanzania,hilo ni kweli lakini tumeshazoea sana kiasi cha kwamba imekuwa utamaduni wetu kutoa na kupokea rushwa,its part of our lives.Na hivyo wengi wetu ni shida kuona kama ni tatizo.

Hotuba hii inawakumbusha wananchi kwamba tunaweza kufanya mabadiliko yenye tija kwa taifa letu na vizazi vijavyo kama tukiamua.Swali kubwa ambalo huwa najiuliza,ni je tutaanzia wapi?
Taifa lenye rushwa haliwezi kuwa na amani wala maendeleo.
 
Kama kawaida..Sikio la kufa..........................!!! CCM Sikio La Kufa
 
wanachadema bana, kispeach njaa halafu mnakipa jina kubwa, huyu kweli ni mchochezi na wala hana sifa mnazo mpa. Tatizo lenu nyie imeshakua tabia yenu kuwatukuza hawa wabunge Njaa. Eti Lema na yeye ameshakua na sifa ya mwanasiasa baada ya speach yake. Mungu atawasaidia wanaCDM na mtarudi kwenye njia yenye heri na atatuepusha na huyu shetani hatari mwenye chuki mbaya sana.
 
Back
Top Bottom