FT: ASEC Mimosas 3-0 Simba SC | CAF Confederation Cup | Stade de L' amitie General

Sasa Ajabu Ni Kwamba Kwa Timu Bora Nyie Afrika Hii Ambapo Kwenye Kundi Lenu Kulingana Na Takwimu Zenu Zile Za Nafasi Ya 7 Hakuna Timu Iliyowazidi Pale Mbn Inakuwa Kila Mechi Sasa Mkienda Huko Hamuoneshi Huo Ubora Wenu Ule Ubora Unakwendaga Wapi Kama Mnavokuwa Kwenye Uwanja Wenu Wa Hatoki Mtu? Au Ubora Wenu Wa Kushika Nafasi Ya 7 Afrika Kama Mnavodai Kulingana Na Takwimu Zenu Ni Ubora Wa Kwenye Uwanja Wa Hatoki Mtu Pekee?
Hakuna protocol ya dzaini hiyo kwamba timu kubwa haifungwi na timu ndogo, hiyo ni wishfully thinking

Maswali uliyouliza kuhusu simba ugenini, jiulize hivyo hivyo kwa timu zilizopigika kipindi simba yuko nyumbani
 
Hivi uto mnapataga wapi ujasiri wakuicheka Simba ikifungwa kimataifa ? Wakati nyie makundi hamjawahi kusogeza pua zenu?
Umeanza lini kufatilia mpira? Makundi babu Hans katupeleka mara mbili utawala wake robo sisi ndio wa kwanza kufika nchi hii so kuyumba kwangu hii miaka 4 isifanye usisahau bwana mdogo hapa tunasaga kunguni usiingie nusu hatutalala mjini siiwazi robo mm nishaingia robo zaidi ya mara 3 nusu ndio utaniziba mdomo mm sio robo never
 
Sio mtaalamu wa soka lakini nikionacho mara zote Simba wanakawia sana kustukiza mashambulizi.

Wanafika golini kwa adui kisha wanasubiri adui ajipange ndio waanze sambusa zao goli kupatikana ni 1/10.

Wanafika golini au jirani na goli hata mita 20 hawa shoot. Wanataka kuingia na mpira langoni.

Ona magoli yaliyofungwa na Asec yote ni mita za kutosha na hakuna wa kuremba. Swali Simba wajiulize hawawezi ku geuka na ku shoot?

Naona watu pale mbele kuanguka anguka tu. Kibu akipokea pasi mara zote ataanguka tu. Boko vivyo hivyo. Kocha haoni hayo?

Ningetamani kuona Mkude na Bwalya wana shoot kila mmoja angalao mara 5 hata wakikosa wanajaribu. Wafanyie mazoezi jambo hilo.

Ningetamani kuona beki Mohamed ajifunze kwa Enock namna ya kuzuia washambuliaji matata anaweza sana.

Usajili ujao Simba isajili wabunifu pale mbele. Kongole kwa Morrison anaonesha umahiri na akili kubwa ya mpira.

Nimeumia lakini Simba bado ni timu nzuri irekenishe mapungufu.
Boko gani tena?
 
Hili kundi hata tukivuka robo huko mbele hatutoboi,game za ugenini at least kocha Gomez aliyeondoka aliweza kidogo japo mechi ya kaizer kule south ilimuharibia,hii inaonesha kuwa kuna matatizo haswa upande wa back line huwa hayarekebishwi,tutazidi kupigwa goli nyingi hadi watu wa usajili wabadilike,kingine japo sina utaalamu sana wa football ila naona Simba hawana mtu wa saikolojia mechi za ugenini confidence yote ya wachezaji huwa inapotea,baada ya hapo ni goli tu huwa zinaingia tatizo nini?,yote kwa yote katika dirisha la usajili msimu huu tulibahatika kupata wachezaji wawili tu wa maana Sakho na inonga basi,viongozi tunaomba watu kama kagere, kanoute au lwanga,mugalu,Wawa,bwallya na onyango watupishe tusajili wengine bila hivyo hakuna tutakachofanya.
Dah Mkuu unamjua Lwanga na Kanoute wewe!?
 
Umeanza lini kufatilia mpira? Makundi babu Hans katupeleka mara mbili utawala wake robo sisi ndio wa kwanza kufika nchi hii so kuyumba kwangu hii miaka 4 isifanye usisahau bwana mdogo hapa tunasaga kunguni usiingie nusu hatutalala mjini siiwazi robo mm nishaingia robo zaidi ya mara 3 nusu ndio utaniziba mdomo mm sio robo never
Hebu tupe nna matokeo yalikuwaje Sir.
 
WIKI hii tutafanikiwa kusikia kuhusu goli la wiki kama ilivyokuwa ile wiki ya SAKO, hebu tusikilizie
 
Yule namba 10 wa Assec, K. Aziz wachezaji na bench la ufundi la Simba hawata msahau. Alikua anawafundisha namna gani soka linachezwa.
 
Kinachoendelea...!

Sasa chache kabla ya mchezo Simba SC wamepata mashabiki 100 ambao wataishangilia mchezo wa leo, ambapo CAF wameruhusu mashabiki 3500 Uwanjani kwenye mchezo huu wa leo.

Na kwa kudhamini mchango na utayari wao kuwashangilia, Simba SC wamewaandalia tisheti zenye ujumbe ALLES LES SIMBA SC... maana yake LET'S GO SIMBA SC.

Ahmed Ally Meneja Habari na Mawasiliano Simba SC.
Mlichapwa vizuri sana bila fujo
 
Yule namba 10 wa Assec, K. Aziz wachezaji na bench la ufundi la Simba hawata msahau. Alikua anawafundisha namna gani soka linachezwa.
Msimu ujao atatua Msimbazi huyo pamoja yule wa Niger aliye wafunga.
 
Back
Top Bottom