Nani anaweza kulinganishwa na Freeman Mbowe? Mtu ambaye alikuwa na uwezo wa kuishi bila bugdha, tena angetaka angeweza kuishi kwa anasa na starehe, lakini akayaacha yote, akachagua maisha ya mateso kwaajili ya mapenzi ya kweli kwa Taifa lake!! Wangapi wanaoliweza hilo? Wengi tumeshindwa. Mbowe ameliishi hilo.
Mungu wa haki na uhuru, kwa rehema zako, endelea kumlinda, kumbariki, kumwinua Mbowe na wengine wote wanaopigania na kupenda haki, bila ya kuangalia vyama vyao, maana wanapigania haki na ule uhuru wa kweli ambao Mungu alimwumba nao mwanadamu. Na wale wadidimizaji wa haki na uhuru wa kweli wazidi kudhaririki hata siku za uzee wao.
Shukrani kwa Ruto kuitambua nafasi ya Mbowe katika kupigania haki, uhuru na demokrasia ya kweli..