KISHINDO
JF-Expert Member
- Jun 23, 2013
- 2,112
- 1,798
Habarini za mahangaiko wasakatonge wenzangu.
Naamini mnaendelea na mahangaiko ya kuitafuta shilingi kwa udi na uvumba.
Narejea katika kichwa cha thread hii, ombi limetolewa kwa Rais kuwa MBOWE pamoja na wenzake wafutiwe mashitaka lakini kwa kufanya hivyo ndo utakuwa mwanzo wa kifo cha CCM na mwanzo wa CHADEMA kukua kuliko nyakati nyingine zote.
Kwa mujibu wa maisha kuwa magumu, vitu kupanda bei kila kukicha, umeme kukatika katika, ukosefu wa madawa mahospitalini, ajira kuwa kizungumkuti n.k. Kupitia hayo kama MBOWE atafutiwa mashitaka yake kwanza itaonekana CHADEMA wamekuwa wakionewa na CCM kila mwaka.
Pili, inamaana kuwa mwaka 2025 wabunge wengi wa CCM hawatarudi Dodoma kwa sababu wengi wao watapigwa chini kwa kutomtetea mwananchi wa kipato cha chini dhidi ya kupanda holela kwa bei za bidhaa mbalimbali nchini ikiwa ni pamoja na kusinzia kwa wabunge bungeni. Hata kura za Rais naamini zitapungua sana 2025.
CHADEMA shangilieni maana USHINDI WA MWAKA 2025 UMEPATIKANA MWAKA 2022.
Naamini mnaendelea na mahangaiko ya kuitafuta shilingi kwa udi na uvumba.
Narejea katika kichwa cha thread hii, ombi limetolewa kwa Rais kuwa MBOWE pamoja na wenzake wafutiwe mashitaka lakini kwa kufanya hivyo ndo utakuwa mwanzo wa kifo cha CCM na mwanzo wa CHADEMA kukua kuliko nyakati nyingine zote.
Kwa mujibu wa maisha kuwa magumu, vitu kupanda bei kila kukicha, umeme kukatika katika, ukosefu wa madawa mahospitalini, ajira kuwa kizungumkuti n.k. Kupitia hayo kama MBOWE atafutiwa mashitaka yake kwanza itaonekana CHADEMA wamekuwa wakionewa na CCM kila mwaka.
Pili, inamaana kuwa mwaka 2025 wabunge wengi wa CCM hawatarudi Dodoma kwa sababu wengi wao watapigwa chini kwa kutomtetea mwananchi wa kipato cha chini dhidi ya kupanda holela kwa bei za bidhaa mbalimbali nchini ikiwa ni pamoja na kusinzia kwa wabunge bungeni. Hata kura za Rais naamini zitapungua sana 2025.
CHADEMA shangilieni maana USHINDI WA MWAKA 2025 UMEPATIKANA MWAKA 2022.