Freeman Mbowe afanikiwa kutoka Jela, ni baada ya Mabomu kupigwa, Wabunge wa CHADEMA walioenda kumpokea Segerea wakamatwa tena!

Quinine

JF-Expert Member
Jul 26, 2010
21,271
47,271
Kinachosubiriwa ni utaratibu wa kutolewa Segerea.

UPDATES:

=> Polisi wametumia mabomu ya machozi kuwatawanya wanachama wa Chadema akiwemo Mbunge Halima Mdee waliofika gereza la Segerea kumchukua Mwenyekiti Freeman Mbowe

=> Wabunge wawili wa Chadema, Halima Mdee na Ester Bulaya, Meya wa Ubungo Boniface Jacob na Katibu wa chama hicho Mkoa wa Dar, Henry Kileo wamekamatwa wakati wakifuatilia mwenyekiti wa Chadema kutoka gereza la Segerea

=> Kuhusu Mbowe bado mchakato wa kumtoa gerezani unaendelea maana dereva aliyekuwa na risiti akielekea Segerea naye amekamatwa baada ya Polisi kupiga mabomu.

=> Askari Magereza wametumia silaha za moto na kufyatua risasi hewani kuwatawanya wafuasi wa Chadema waliokuwa nje ya gereza hilo kumsubiri Mbowe akiachiwa. Baadhi ya viongozi na wananchi kadhaa wamejeruhiwa, akiwemo dereva mmoja wa bodaboda ambaye inadaiwa amevunjika mguu.

UPDATES: 1750HRS

Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe hatimaye ameachiwa kutoka Gereza la Segerea baada ya taratibu kukamilika. Sasa anaelekea Makao makuu ya CHADEMA mtaa wa Ufipa Kinondoni.
IMG_20200313_121837.jpg
1584107793685.png
 
God is great!!

Hata hivyo,tujiulize haya:

ACACIA walipgwa kodi ya matrilioni

Vyombo vya habari mwaka 2017 kama sio mwaka 2018 vilipigwa faini za mamilioni

Wanaoshitakiwa kwa uhujumu uchumi nao wanalipishwa mamilioni

Kina Mbowe nao wamelipishwa mamilioni

Je,hamuoni kuna kitu kinaendelea hapa?
 
Ila Mbowe ni kiongozi makini sana. CHADEMA ni watu makini sana. Ingekuwa nzi wa kijani wangeanza kumtoa mwenyekiti ila kwa ukomavu wa Mbowe na CHADEMA hajakubali kutoka akamwacha mtu ndani. Huu ni ukomavu mkubwa sana wa kisiasa na kiakili.
 
God is great!!

Hata hivyo,tujiulize haya:

ACACIA walipgwa kodi ya matrilioni

Vyombo vya habari vikapigwa faina za mamilioni

Wanaoshitakiwa kwa uhujumu uchumi nao wanalipishwa mamilioni

Kina Mbowe nao wamelipishwa mamilioni

Je,hamuoni kuna kitu kinaendelea hapa?

Na ukumbuke kuwa hizi zama za Kayafa za Mwisho hakuna pesa itafanyiwa ukaguzi...
Ni upigaji kama kawa...!!
 
Back
Top Bottom