Free Wi-Fi: Nchi zingine wamewezaje?

Free Wi-Fi: Nchi zingine wamewezaje?

Majiji yetu yamelala mno ingetakiwa ukiingia Dar/Mwanza/Arusha/Mbeya/Moshi unaconnect free wifi?
Vyuoni ni upofu wa TCRA na TCU. Ingekuwa ni lazima na wapewe special rates unlimited.
Kwanini basi la mwarabu liwe na wifi vyuo vikuu ishindikane?

TCRA na TCU wanaingiaje hapa ?
Mitandao ya simu (Tigo,Airtel,Vodacom &Halotel) wana vifurushi maalum kwa wanavyuo
 
Hivi si nilisikiaga wanataka kuweka free wifi kwenye makazi ya watu hiyo project imeishia wapi
 
kuna cable zilichimbiwa chini wenyewe wanaita mkongo wa taifa hizi unaweza ukazivuta hadi mahali unapotaka kuna vitu wanakufungia kisha unaweza kuruhusu free wife eneo hilo

Samahani bwana Mo11....jamaa alitaka kujua kwann huu ufundi wa free wifi....husiye kati ya huduma zinazotolewa na serikali tukufu ya Bro.Magu.....ili mimi wa huku mbwinde nikifika sehemu flan nakuta free wifi naanza kuburudika JF bureeee?
 
Nilishawahi kukaa nchi fulani ya mashariki ya mbali nchi hiyo haijaendelea sana. Lakini wi-fi zimetapakaa kila sehemu ukienda bar, kwenye mgahawa hadi salooni kuna wi -fi. Ukifika tu unaona password iko displayed pale counter.
 
Mara chache huduma hii huwa naipata kwny mabasi ya mikoani (Dodoma)Luxury buses..

Nao huwa wana figisufigisu wanasemaga Hawaja nunua bundle.
huwa na keleka kweli..
Niliwahi rudisha tikiti kisa bus halina wifi..konda akaesema ipo..
Kufika mbele mbele huko..namuuliza konda akasema Walisahau kununua bundle..
nilikasirika.
Nikaamua kujiunga..nilifaidi kuchaji simu janja tu..(chini ya seat)

Huku kwt bado sana..ukanjanja umejaa sana.
 
UDSM kuna free wifi hii imewekwa kuwasaidia wanafunzi ku-download material yao lakini wengine wanaitumia ku-download movie/music.Nimesikia TTCL wamesign contract na DART kuweka wifi kwenye vituo vyote vya DART

Hii ni tabia ya wanafunzi dunia nzima.
 
Mkuu The Boss free wi fi ni kitu kinachowezekana sana. Hata katika 'state-of-the art' Stesheni mpya ya Daladala pale Mawasiliano Manispaa ya Kinondoni wameweka free wi fi.. Ni manispaa kufikiria 'stage' nyingine waanze kuweka katika maeneo muhimu ya manispaa na hii itategemea kama hawatapata figisu kutoka katika makampuni ya simu..
 
Jamani tunaelewa wi fi inaweza ikawepo na ukaungnisha lakini ikawa haina bando tatizo ni bando...!!
 
Bossman, unajua kuwa JNIA kuwa Wi-Fi ya bure?

Na naijua migawaha mingi Dar ambayo ina hiyo huduma.

Boogie Woogie wanayo, Samaki Samaki wanayo, Rhapsody's wanayo....na wengineo wengi tu.

Hizo sehemu nafahamu zipo....
but nilikuwa hasa nafikiria maeneo ya watu weengi zaidi....
mfano labda eneo lote la ferry na posta....
au vituo vyote vya UDART....
 
Hizo sehemu nafahamu zipo....
but nilikuwa hasa nafikiria maeneo ya watu weengi zaidi....
mfano labda eneo lote la ferry na posta....
au vituo vyote vya UDART....

Mbona inawezekana kabisa..

Kama uwanja wa ndege wameweza sioni kwa nini hapo feri ishindikane!
 
Kuna fibre zilipitishwa chini ya ardhi maeneo ya Mbezi Beach zaidi ya miezi miwili iliyopita, sina hakika kama kuna Watu wameunganishwa! Ingewezekana sana kutumia huo mfumo nafuu kwa ajili ya Wifi hasa kwenye eneo lote la beach.
 
Tatizo kubwa ni network structure yetu, websites na blogs nyiingi zilizoko bongo zimekuwa hosted nje ya nchi hii inasababisha gaharama ya kuaccess mtandao ziwe kubwa zaidi
Ila kama mitandao miingi ya kibongo ingekuwa hosted bongo ingrsababisha gharama ya kuiaccess iwe rahisi tungekuwa tunapata taabu kuaccess email,Facebook....,
Hapo ndo nchi zilizoendelea wanapotupiga bao,
 
Kuna fibre zilipitishwa chini ya ardhi maeneo ya Mbezi Beach zaidi ya miezi miwili iliyopita, sina hakika kama kuna Watu wameunganishwa! Ingewezekana sana kutumia huo mfumo nafuu kwa ajili ya Wifi hasa kwenye eneo lote la beach.

kampuni gani walipitisha?
 
Back
Top Bottom