The Boss
JF-Expert Member
- Aug 18, 2009
- 49,320
- 117,653
Huwa najiuliza ili kuweza kuwa na free Wi-Fi..... Mfano kwenye vyuo vyetu
au maeneo yetu sehemu mbali mbali nini kinatakiwa kifanyike?
Nchi zingine wamewezaje? Ni lazima serikali ishiriki?
Wadau binafsi wakiamua wafanye ni ghali sana? Humu kuna watu mna uelewa zaidi hebu tuelewesheni..
==========
BAADHI YA MAONI YA WADAU
<<UPDATE (Oktoba, 2016)>>
SERIKALI: Dar kupata huduma ya internet Wi-Fi bure!
au maeneo yetu sehemu mbali mbali nini kinatakiwa kifanyike?
Nchi zingine wamewezaje? Ni lazima serikali ishiriki?
Wadau binafsi wakiamua wafanye ni ghali sana? Humu kuna watu mna uelewa zaidi hebu tuelewesheni..
==========
BAADHI YA MAONI YA WADAU
Kuweka internet swala ni kuwa na wifi router tu, wifi router inachukua internet kupitia labda cable then inadistrubute via wifi kwa users wote, challenge inakuja kwenye number of users, wakiwa wengi speed inapungua alafu inakua vigumu sana kuconnect kwenye router moja, hizi consumer grade routers haziwezi handle 100+ users, ila kama ni restaurant wanakaa watu 20 kwa wakati moja router moja ya wifi ac 1GBPs inaweza ikawahandle vizuri tu bila shida. Kama ni area kama park ambayo ina watu wengi inabidi kuweka router nyingi kidogo ziwe distrubuted sehemu tofauti.
Haina complications zozote zile, swala ni mlipiaji tu wa hiyo internet, kama anapata unlimited then hamna shida, ila kama ni bundle za kulipia hizi wakikaa wanaopenda kudownload movie lazima aumie.
Hii fibre optic toka naondoka Tanzania miaka 5 iliyopita walisema wanaiweka sijui hadi leo naona kimya, ingekuwepo wanadistribute kupitia cable kila nyumba mtu unalipa unakaa mwezi mzima na unlimited internet ya 1GBPs huna mawazo kabisa, kudistribute internet ingekua rahisi sana, kila mtu angekua na wifi access points hata uchumi ungekua maana online business zinalipa vizuri mno.
Njia pekee ya kuliwezesha hili kwa sasa ni kama huu mkongo wa optic fibre waliokua wanauongelea utatimia kama ilivyokua imepangwa, kupitisha internet kupitia cable ni very very cheap, waya moja unaweza pitisha bandwidth kubwa mno kwa bei nafuu, ndio maana hata hawa providers badala ya satellite waliamua kutumia optic cable ikapita kutoka china chini ya bahari hadi east africa.
Kwa Tanzania hili linawezekana sana tu sema nadhani hawafanyi hivyo maana wanataka waendelee kupiga hela, wireless networks ni gharama sana, hii mikongo ya 3G, 4G, bandwidth cap yake ni ndogo na bado kuna interference, ni challenge hata nchi kama US wanasumbuka sana kuhandle wireless networks ndio maana nyumba na ofisi karibia zote wanatumia cable, wireless watu wanatumia wakiwa nje tu mara chache kwa kazi ndogondogo kama kuchat. Kwenye coffee shops, restaurants au convenience stores wakiwa na wifi jua imeungwa kwenye cable, so its still cheap all the way.
=======Tatizo kubwa ni network structure yetu, websites na blogs nyiingi zilizoko bongo zimekuwa hosted nje ya nchi, hii inasababisha gaharama ya kuaccess mtandao ziwe kubwa zaidi.
Ila kama mitandao miingi ya kibongo ingekuwa hosted bongo ingesababisha gharama ya kui-access iwe rahisi, tungekuwa tunapata taabu kuaccess email, Facebook...,
Hapo ndo nchi zilizoendelea wanapotupiga bao,
<<UPDATE (Oktoba, 2016)>>
SERIKALI: Dar kupata huduma ya internet Wi-Fi bure!