Kuhusu kuomba fedha, kwanza namuona kila Mara yuko busy na familia yake, muda wote utasikia wanampigia simu za wagonjwa, misiba, ada za shule etc. Hill si tatizo kwangu. Zikitulia simu za ndugu ataanza kudeal na ujenzi, simu za mafundi zinapishana, bado service za magari, utasikia kununua viwanja au mashamba...... Hela yake yote ni kama ni ya maendeleo yake, sasa ukisikia analalamika kaelemewa, utapata nguvu ya kumuomba? Nikikasirika anavurugwa, hapo napo kuna mawili, ataniomba niongee naye private, akiona sijisikii,atatafuta namna tuonane akiwa na rafiki zake, huwa siwezi kuonesha hasira mbele za watu. Tukitoka hapo,ataomba kuongea na Mimi!
Miaka yote nimekuwa kwenye distant relationship, ila muda huu nikaamua niwe na mahusiano ya karibu labda ntaona tofauti, kinacho niboa hata akija kwangu akaona hela anachukua! Mwanzoni nilikuwa nachukulia poa, ila muda huu akijichanganya achukue huwa anapata habari yake,nilisha acha hata kupika akija kunitembelea. Nilikuwa nafanya kwa kupenda lakini nikaona inakuwa kama sheria huku hela yake siijui. Nikijisikia kwenda kwake sijusumbui tena na kazi za nyumbani kama mwanzo. Yaani natafuta stability tu ya moyo wangu then niondoke. Msiseme ni Mario, hapana. Ni MTU mwenye kazi yake, na sikujipeleka, ilimchukua muda kunitafuta na kunipata, na mwanzo alikuwa akifanya kila kitu mpaka nalia!
Alipo kuja kugundua kuwa Nina vimifereji vya hela, nikawa nimejiroga. Na sikuwa na namna maana kama ni safari atajua kuwa nimesafiri nk!