MIMI BABA YENU
JF-Expert Member
- Mar 1, 2019
- 319
- 755
Fred ambaye ni mtoto wa Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa amesema yeye pamoja na familia nzima ya Lowassa wamerejea nyumbani akimaanisha Chama cha Mapinduzi (CCM). Fred amezungumza maneno hayo leo jijini Arusha. Fred ambaye alijiunga na CHADEMA Julai 28, 2015 ameeleza kuwa anajisikia vizuri kurudi nyumbani kuendelea kushirikiana na marafiki zake aliowaacha CCM.