Four cylinder Vs six cylinder

Kiongozi Mazda rx 8 nilisikia inatumia Rotary Engine, cc ndogo lakini inabugia wese kuliko hizi za piston zenye cc sawa. Ila inakuwa na nguvu sana
Ni kweli mkuu inatumia rotary engine inakula wese si mchezo na oil balaa lkn ukiiweka barabarani ni heshima mkuu inakimbia si mchezo na iko stable uzuri weight ratio yake ni 50:50 kwa hiyo kukata kona na speed kubwa sana wala sio tatizo mkuu.
 

Una maelezo mazuri sana. Nikuulize swali nje kidogo ya mada. Nissan X-Trail (2002) ni 4 cylinders, 2000cc. Gari hii inatembea 6km/Ltr hapa Dar es Salaam. Unaweza kusemaje, ni ulaji wa mafuta wa kawaida kutokana na aina au muundo wa gari au kuna part inahitaji kubadilishwa. Gari ni used from Japan.
 
Najitahidi kuelewa ulicho andika, vipi hapo una assume kuwa combustion chambers na pistons zina same measurement?
Mkuu si assume hivyo, na Assume discharge tu yanayopita kwenye hizo nozzle, combustion system sijagusia ingawa of course una matokeo pia ya matumizi ya mafuta
 
Habari wakuu naomba kuweka kwenu huu mjadala mtu anayetumia cc 2000 lakini four cylinder na anayetumia cc 2000 lakini six cylinder.
Hapo tofauti ni nin
Hapo cubic capacity ni sawa kws maana ya ujumla wake,tofauti hapo ukubwa wa chamber(cylinder) cylinder za six zitakuwa ndogo ukilinganisha na za four respectively.
 

Mkuu unachoongea ni sawa kabisa provided cc ni tofauti, let's say kuna v4=2000cc, v6=2500, v8=3000cc.
Lakini kutokana na mleta maada hapa kauliza kuhusu engine zenye cc sawa yaani 2000cc each lakini tofauti katika namba za pistoni.
  1. Engine ya kwanza ni cc 2000 lakini pistoni 4, ambapo ni sawa na 500cc per piston
  2. Engine ya pili pia ni cc 2000 lakini pistoni 6, ambapo ni sawa na 333.3cc per piston.
Now ukiangalia hapo ni kuwa hakuta kuwa na tofauti ukiwasha gari lako la pistoni 4 na mwenzako akawasha lake la pistoni 6 kwasababu kwa sababu kwa gari lako na la mwenzako kwa kila dakika moja yatatumia ujazo sawa wa mixture ya gasi/air ila tofauti itakuja kwenye revolutions.

Ila kama ingekuwa ni cc tofauti lazima utumiaji wa mafuta ungekuwa tofauti pia.
 
Kaka nakubaliana na wewe, ILA tofauti ipo, ujazo ni sawa ila kama huyo wa Cylinder Sita atatumia masaa 2 kumaliza, huyo wa pili atatumia masaa mawili na nusu kumaliza mafuta yote. Kadri ya masaa yatakavyo kuwa mengi ndivyo umbali unaweza kuongezeka kabla ya kuongeza mafuta na hapo ndipo linapokuja swala la kuwa gari halili mafuta mengi maana unaagalia urefu wa route dhidi ya mafuta yaliyitumika. So kimsingi kila kitu kiko sawa kiujazo ila kuyamaliza kwa haraka huo ndiyo ulaji wenyewe.
 
Alteza zipo hivi zina cc 2000 ila kuna ya 4cylinder na 6
 
Mkuu nimekuelewa mpaka nimefurahhh...embu kunywa soda moja apo kwa hela yako... Kwa furaha yangu
 
Mkuu hii gari ninachojua ni Engine yake haitumii cylinders kama za kawaida.. Inatumia rotor engine..ndo maana cc ndogo ulaji mkubwa..google rotor engine utaiona mfumo wake..upo tofauti kabisah na huu wa cylinders
 
Ufafanua vizuri kabisa and this is a fact
 
Injini ya gari langu ni 5.7L V8, kwa hiyo ninasoma 2000 cc cylinder 6 ninakuwa kama siamini ninachosoma, kwani nafikiri 2000 cc ni kama lita mbili tu. Kwa injini kama hiyo kuwa na cylinder sita ina maana itakuwa na vipistoni vidogo sana katika karne hii, hivyo sehemu ya energy inapotea bure kukabiliana na friction baina ya moving parts.
 
Inategemea na izo cork umeweka za ukubwa gani...je zote zinalingana? We huoni kama umeweka cork 6 za inch 1 alafu ukaweka cork 4 za nchi 2 ni vitu tofauti? Ivo ndo ilivo kwny piston....kuna piston nyngne ni chache ila kubwa kiumbo....nyngne nyng ila ndogo kiumbo...inapokua kubwa pigo lake moja ni takatifu.
 
Upo sahihi kabisa.
Kumrahisishia kwanini 4cylinder engine 2000cc and 6cylinder engine 2000cc.
Kama wewe ulivyoainisha ya kuwa tofauti yake kwa lugha yetu, na kiutaalam tunasema zimetofautiana ktk bore and stroke.
Sasa kwa nini muundo wa engine uwe tofauti lkn cc ziwe sawa?

2000cc 4cylinder=bore kubwa na stroke kubwa
-Ni nzuri kwa matumizi ya mjini with low consumption ya mafuta at low speed.
-high consumption ya mafuta ktk masafa marefu
-ktk masafa marefuni rahisi kutumia engine up 95% kitu ambacho kinamaliza uhai wa engine.

2000cc 6cylinder=bore ndogo na stroke ndogo
-Ni nzuri kwa matumizi ya masafa, au safari ndefu sio mjini
-High consumption ya mafuta at low speed.
-Ktk masafa marefu engine hutumika up to 80% uhai wa engine unakuwa mrefu.
 

ufafanuzi malidhawa kabisa huu...kutoa uelewa wa ziada maana ya maneno bore-ni kipenyo cha cylinder wakati stroke-ni urefu wa piston au tuseme ni umbali ambao pistoni inatembea ndani ya cylinder.

ndio maana ufaanuzi wa huyu bwana unaonyesha unapokuwa na bore(kipenyo kikubwa cha cylinder) kubwa lazima pawe na stroke(pistoni itembee umbali zaidi ndani ya cylinder) kubwa pia.
 
Habari wakuu naomba kuweka kwenu huu mjadala mtu anayetumia cc 2000 lakini four cylinder na anayetumia cc 2000 lakini six cylinder.
Hapo tofauti ni nin
Nachojua ni Cylinder 4 haili mafuta maana zinafunguka piston 4 so haichanganyi mapema, lakini Piston 6 inakula mafuta na inachanganya fasta! Gari kama Mark X ambayo ina pistoni 6 ukikanyaga tu ni fasta haupo, gari kama Vx V8 ukipiga tu unahama fasta! Lakini Mafuta ndiyo shughuli
 
good pia six mara zote huwa haitoi muungurumo mkubwa km four na hii inachangiwa na kuwa na cyrinder nyingi zaidi ya gari zenye four. chukulia mfano pikipiki yenye piston moja au mashine ya disel yenye piston zilivyo na kelele
ni kweli kwa kadri ingine inavyokuwa na cylinder nyingi ndivyo kiwango cha kelele inachozalisha hupungua
 
Maelezo mazuri sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…