Former IGP Harun G. Mahundi IS NO MORE

Former IGP Harun G. Mahundi IS NO MORE

oh! Jamani kamfuata mkewe.let them rest in peace.bwana ametoa na ametwaa.jina la bwana lihimidiwe.
 
RIP Mahundi, Jeshi la polisi lilikuwa na utendaji mzuri. Ni utumishi uliotukuka. Mwenyez Mungu awape nguvu wanafamilia waweze kupita katika kipindi hiki kigumu
 
our prayers and condolences to the bereaved family
 
Namjua mwanae mmoja ni pilot wa ndege za TANAPA.
Mungu ailaze roho ya marehemu pema peponi...
 
mwache aende alikuwa anapendelea rafiki zake akiwa igp, akina mwansasu,mahita piter lukas, rashid hemed,
 
HABARI LEO:

MWILI wa aliyewahi kuwa Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, Inspekta Jenerali mstaafu Haruni Mahundi unatarajiwa kuagwa keshokutwa katika Viwanja vya Karimjee na kuzikwa katika makaburi ya Kinondoni, Dar es Salaam.

Mwenyekiti wa Kamati ya Mazishi hayo, Naibu Kamishna wa Polisi Suleiman Kova alisema jana kuwa shughuli za mazishi zitaanzia Karimjee ambapo kuanzia saa 4 asubuhi hadi saa 6 mchana zitatolewa heshima za mwisho.

Kova, ambaye pia ni Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, alisema viongozi mbalimbali watakuwepo Karimjee na zitaendeshwa shughuli za dini na kijeshi ambapo pia kutakuwepo gwaride rasmi.

Mahundi alikuwa IGP kwa miaka 10 na amefariki akiwa na umri wa miaka 72. Alifariki ghafla Jumatatu wiki hii
 
Alikuwa hana tamaa na siasa bt alimtesa sana mrema na mabomu mwaka 95 akastaafu 96
 
Back
Top Bottom