FORBES: Rais Magufuli ni ‘Rais Mwanamageuzi’

FORBES: Rais Magufuli ni ‘Rais Mwanamageuzi’

Forbes ni gazeti la kibiashara na wafanya biashara. Wanajua fika kuvunjika kwa koleo sio mwisho wa uhunzi. Ili mambo yakae sawa, lazima mistakes zitakuwepo.
Wajanja ni wale.wanao endelea mbele hata baada ya matatizo kutokea. Imagine kama kila mtu angelikuwa anakata tamaa first round, maisha yangekuwaje leo
Na ushahidi huu hapa! Hiyo habari imechapishwa na Penresa! Angalia Logo kwenye hiyo cover! Na Penresa wenyewe kwenye website yao wanaeleza hivi:-
Penresa is an independent consultancy agency, specialized in marketing and communication for emerging markets.
Hiyo ni kama marketing firm tu, kisha wanaendelea:-
We serve clients and partners around the clock, around the world. Our clients approach us for innovative campaigns with the spark to ignite sales and the staying power to build enduring brands. Our international experience and ability to deliver truly unique results is what keeps clients knocking on our door.
Unaona sasa?! Kumbe ukiwa na issue, mnaongea biashara, jamaa wanai-structure for innovative campaigns, kisha, this's how they do:-
We identify opportunities and develop platforms for organizations, from both the public and private sector, to better express themselves and connect with their target audience.

We create awareness and generate interest through targeted advertising platforms as per our client’s requirements. If you need fresh ideas or a new direction we can tailor a variety of campaigns and strategies to your specific needs.
Kumbe, wakishaandaa marketing and promotional campaign, depending na pesa yako, wanaangalia wakatangaze wapi na kwa mfumo upi! Kwa case hii, kwa vile pesa haikutosha kutangaza Forbes Original, tangazo likapelekwa Forbes Academia (Forbes Africa) na kutangazwa kwa mtindo wa habari, lakini in reality, ni sponsored article!!
 
Kumbe, wakishaandaa marketing and promotional campaign, depending na pesa yako, wanaangalia wakatangaze wapi na kwa mfumo upi!
Haya utayaona kwa wingi sana siku sio nyingi.
Umefanya vyema sana kufunua ujinga huu.

Sio kwamba "pesa haikutosha", wanajua majuha wakishaona 'Forbes' inatosha kuchota akili yote!


Mkuu 'Myplusbee' shukrani nyingi. Utakuwa umetoa somo la kutosha kwa anayetaka kujifunza.
 
Magufuli amefanya mageuzi, hilo halina ubishi.
Wanaompinga wanatakiwa waoneshe athari za mageuzi hayo kuwa ni hasi zaidi kuliko chanya, lakini kusema hajafanya ni ujinga tu.
Kuleta mafarakano nchini ndio kuleta 'mageuzi'? Kukandamiza haki za wengine ndio 'mageuzi'?...Kutofuata taratibu, sheria na hata katiba ya nchi, ndio 'mageuzi'?

"Ujinga" ni kuuza haki zako kwa kuona 'vitu vinavyojengwa' na kudhani ndio maendeleo, hata kama vitu hivyo vinajengwa kwa kukanyaga haki za wengine.
 
Na ushahidi huu hapa! Hiyo habari imechapishwa na Penresa! Angalia Logo kwenye hiyo cover! Na Penresa wenyewe kwenye website yao wanaeleza hivi:-Hiyo ni kama marketing firm tu, kisha wanaendelea:-Unaona sasa?! Kumbe ukiwa na issue, mnaongea biashara, jamaa wanai-structure for innovative campaigns, kisha, this's how they do:-Kumbe, wakishaandaa marketing and promotional campaign, depending na pesa yako, wanaangalia wakatangaze wapi na kwa mfumo upi! Kwa case hii, kwa vile pesa haikutosha kutangaza Forbes Original, tangazo likapelekwa Forbes Academia (Forbes Africa) na kutangazwa kwa mtindo wa habari, lakini in reality, ni sponsored article!!
Umechangia hoja kisomi hasa.
Safi sana
 
Kama korosjo itakua hasara itakua bahati mbaya tu kwa serikali lakini si kwa wakulima ambao serikali itakua imewapigia kifua kwa dhuluma ya wafanya biashara waliyotaka kuwadhulumu kwa kula njama kuweka bei ndogo. Hata hivyo bado kuna uwezekano wa korosho hizo kuuzwa.

Hapa naona mnajaribu kutakatisha Kaniki, msihangaike kwani hiyo ndio rangi yake.
 
Magufuli amefanya mageuzi, hilo halina ubishi.
Wanaompinga wanatakiwa waoneshe athari za mageuzi hayo kuwa ni hasi zaidi kuliko chanya, lakini kusema hajafanya ni ujinga tu.

Amefanya mageuzi au amejikita kwenye miundombinu mbinu kwa nguvu zake zote? Mageuzi yangeanzia kwenye taratibu, sheria na katiba. Huenda hujui mageuzi yana maana gani kwa upana wake, hivyo unajikuta unachanganya kati ya mageuzi na miundombinu mbinu mingi.

Mfano mrahisi wa mageuzi tungeliona sera zingebadilika, tungeona mifumo ikibadilika kama badala ya yeye kuteua kila Mkuu wa taasisi za umma zoezi hilo lingefanywa na taasisi nyingine. Nguvu zingehama kutoka kwa mtu na kuwa na taasisi imara. Kama hayo hayajafanywa basi ujue hiyo miundo mbinu sio mageuzi bali ndio matumizi halisi ya mikopo na kodi za wananchi. Kama ili mtu kuwa kiongozi bado wizi wa kura kupitia tume isiyo huru ya uchaguzi ndio inatoa maamuzi hayo sio mageuzi.
 
Cc pascal mayala
nakusaidia kumuita CC: Pascal Mayalla
Asante kuniita, nimeitika,
Haya ndio majarida ya kizalendo na kiukweli kwa ajili ya kuleta maendeleo ya Africa, sio the Economist, kila siku wao ni kukandia.

Ni ukweli uliowazi, rais Magufuli amefanya mageuzi makubwa ambayo by 2025, yatakuwa yameibadili Tanzania kuwa ni nchi ya viwanda, nchi ya uchumi wa gesi na nchi ya uchumi wa kati kupitia :

Shirika kubwa la ndege la ATC, litakalo kuwa la 3 baada ya Ethiopia na SAA,
Tutakuwa na SGR ambapo bandari za Tanzania ndizo zita handle cargo ya Uganda, Rwanda, Burundi, Zambia, Malawi na DRC.

Umeme wa Stigler sio tuu tuta export electricity, tunaweza ku electrify DART, magari yakatumia umeme.

Uchumi wa gesi kwa industrial power, na domestic use, hadi gesi ya majumbani, na magari kutumia gesi badala ya mafuta, India, hadi bajaj, zinatumia gesi!.

Maeneo yote yatakuwa accessible kupitia miondombinu ya mabarabara, reli, ndege, ma flyovers na ma interchanges kama ya Ubungo yatashehenezwa kote hivyo kurahisisha movement of people, goods and services.

Tutaboresha kilimo chetu kuwa ni kilimo cha kisasa kwa kutumia mechanized agriculture, na kutumia kilimo biashara kuzalisha malighafi ya viwanda.

Kupitia elimu bure, tutatengeneza taifa la kisomi lenye nguvu kazi ya kutosha na teknolojia ya kisasa kuendesha Tanzania ya viwanda.

Tanzania, itakuwa ni nchi ya viwanda, everything we producer kinakuwa processed humu humu nchini to add value, badala ya kuuza korosho ghafi, ambayo ina short life span, tutabangua korosho yote na ku export. Badala ya kuuza mahindi, tutauza unga, etc. Tutatengeneza almost everything, hivyo Tanzania kuwa an industrial power.

Yote haya hayawezi kufanikiwa bila a price to pay kwa mageuzi ya kisiasa kwenye democracy na human rights. 2020 yanakuja mageuzi makubwa ya Tanzanian democracy, uchaguzi wa 2020 utairudisha CCM in full control of this country, hivyo kufuatia hii kazi nzuri ya kuleta maendeleo anayoifanya rais Magufuli na serikali yake ya awamu ya 5, kutakako ifanya CCM, ikubalike sana na Watanzania, uchaguzi wa 2020 kwa huku bara, Watanzania wote wataichagua CCM tuu, hivyo Bunge lijalo ni Bunge la chama kimoja, na kukitokea mpinzani kurudi bungeni, ni mpinzani mmoja tuu, Zitto, kama asipogombea urais kwa tiketi ya upinzani, tena huyu atarejea kwa sababu yeye ni Mwami.
Haya pia ni mageuzi.

Magufuli atainyoosha nchi, hakutakuwa na rushwa na ufisadi, uzembe, uvivu kwa kusingizia mikutano ya kisiasa, na uzururaji kusingizia kufanya maandamano, kila mtu sio anaombwa kufanya kazi, au anabembelezwa kufanya kazi, bali kila mtu ni lazima afanye kazj, na asiye fanya kazi na asile, afe, hapa kazi tuu hata ikibidi kwa mijeledi. Ndivyo walivyofanya kina Seretse Khama wa Botswana, Tito wa Yugoslavia, Lee Kuan Yew wa Singapore, Mustafa Kemal wa Uturuki, hawa wote walitawala kwa mkono wa chuma kuzikomboa nchi zao toka umasikini na kuzigeuza tajiri, hivyo Magufuli ataigeuza Tanzania kuwa a Donor Country.

Pia tutakuwa na mageuzi kwenye media, right of information, access to information, na mambo ya human rights, ikiwemo freedom of expression, nchi yetu itakuwa iko vitani kwenye vita vya kiuchumi, mtu yoyote atakaye turudisha nyuma kwa mawazo, maneno na matendo, hawezi kuachwa hivi hivi akasurvive. Atafanywa nini, hili sio langu ni la vyombo husika, wakiwemo wale waodhaniwa ni wasiojulikana.

No gain without pain, hivi ndivyo the tiger walivyo pata maendeleo, anachikifanya Magufuli sasa, wengi mtakielewa 2025, na ikifika hayo hayakamilika, aendelee, akamilishe ndipo apumzike.
P
 
Paskakali hulali uko kwenye huu urahibu wako JF!
Its true, JF ni very addictive, nahisi hata mahitaji ya zile services yamepungua, siku hizi hata umuone mtu anatisha vipi, zigo zigo, zamani suruali zinabana, sasa suruali hazibani!, hili la jf kuwekwa kwenye mobile version, kunapelekea mtu kupanda kitandani na simu, ndio partner wako, hadi wife unamuona kama dada, ni mwendo wa mzungu wa nne, kisa JF!.
huu urahibu utakuja kuwa na matokeo mabaya kwa ndoa changa!.
P
 
FORBES wanasema Rais Magufuli ni ‘Rais Mwanamageuzi, mleta maendeleo’, ndani ya story hiyo wanaeleza mafanikio kedekede ya serikali yake

View attachment 1131146
No kweli huyu rais ana mafanikio yake hasa katika miundo mbinu.
Lakini pia anamapungufu makubwa hasa kwenye maeneo ya;

1. Uchumi
2. Democrasia
3. Diplomasia


wao Forbes hawazi kuyaona haya maana kwao ni non concern na macho yao makubwa yako kwenye;

1. Infrastructure Projects
2. National bogus contracts awareness
3. Corruptions in some cases
 
FORBES wanasema Rais Magufuli ni ‘Rais Mwanamageuzi, mleta maendeleo’, ndani ya story hiyo wanaeleza mafanikio kedekede ya serikali yake

View attachment 1131146
Ipo hapa
 
Its true, JF ni very addictive, nahisi hata mahitaji ya zile services yamepungua, siku hizi hata umuone mtu anatusha vipi, suruali hazibani, wife kama dada, ni mwendo wa mzungu wa nne, kisa JF!.
P
Umeiona hii? Hasa pale anapokiri kuwa hawawezi kutushinda mahakamani. Jaribu kuidadavua kama kawaida yako Pascal Mayalla
 
Kumbe ni sponsored article iliyoandaliwa na Penresa na kuwekwa Forbes Africa! Siyo article ya Forbes, na wala haipo ndani ya Jarida la Forbes.

Forbes hawawezi kuandika kitu kisichofanyiwa utafiti. Penresa ni marketing company, wamefanya hii marketing kwa gharama gani? Na nani amelipia hiyo gharama? Walioamua kwenda Penresa kuomba kufanyiwa hiyo marketing, wamefanya hivyo kwa lengo gani?

Ama kweli, kizuri chajiuza, kibaya chajitembeza. Hatuwezi kujiuza mpaka tukafanye kazi ya kuomba kupambwa?
 
Back
Top Bottom