For your EYES ONLY: From Salva to Rostam

Kweli serikali ya sasa iko mifukoni mwa watu!!! Enzi za mwalimu mtu alijitapa akawekwa ndani sasa hivi hajitapi mtu ila raia tumekubali JK & Co wamewekwa mifukoni mwa RA & Co
 
Hii nayo kali. Manyerere na Muhingo sasa waseme tena bisi wao si fisadi wakati wame operate illegally. ROSEMARY MWAKITWANGE anajua mengi na atueleze kuhusu hilo la usajili. na je kwa nini alikimbia NHL?

Madame Rose tuambie!

Rose alishindwa kukubaliana na mfumo wao... asingeweza kusurvive in that mess
 
Its a proof that politics is a dirty game..
here is a political clout cocktail recipe
:Ingredients & Method
Warning coz the cocktail can be deadly:Before you attempt this, make sure the power is well connected and you have the balls!
mix together in a large shaker the main ingredients:
cronism,corruption, abuse of power and authority,shake well
add a little boldness, continue shaking
then wait and see, if no changes in the consistency of the mixture...
add some clean blackmailing,shake even more
then the cocktail is ready for use....

N.B. You can improvise as per your need and taste


'Blackmail' also sprung up in my mind. But it seemed very subtle...the clever fox!!
 
Kazi nzuri sana Inzi. Kwa ufupi, hizi paragraph tatu zinaelezea vema yote juu ya nia ya Salva kumuandikia hii barua Rostam.








Fundisho kwetu;
  1. Serikali ya JK iliingia madarakani kwa msaada mkubwa sana wa Rostam na wapambe wake. Hivyo JK hawezi kumchukulia RA hatua yoyote licha ya kelele za wa TZ wengi ikiwemo Mengi aliyeamua kujitoa mhanga.
  2. Kama wengi wa walio madarakani wameingia kwa kujuana na sio sifa za utendaji wao, au hata kama zifa wanazo, watawajibika vipi ili kuendeleza nchi badala ya kutunisha kilichowavutia kwenye utumishi wa nchi yaani vibaba vyao?
  3. Hivi ni kwa nini JK aendelee kuwa raisi kama yeye na mafisadi ni timu moja?
  4. Je bunge letu linasemaje au watasubiri mpaka nchi ifilisike au tuchinjane ndio wamchukulie hatua JK?
Kwa wale wanaotaka JK apewe miaka mingine 5 wajitokeze na kutueleza apewe kwa uzalendo upi alionao?

Hapa ndipo pia tunaweza kuuona uzito wa tuzo ya Mwanamke Jasiri ya Wamarekani kwa Anne Kilango
 
Kama hii barua ni kweli ya Rweyemamu na ilimfikia Rostam ina maana Rostam ana uwezo wa kumuunganishia kazi mtu akawe presidential spokesman, nimekoma na Rostam Aziz.

By the way, to be the devil's lawyer for a minute, kama ungekuwa ni wewe Kikwete halafu kina Rostam na kina Rweyemamu ndio hao waliku propell into power kama Salva anavyosema humo, ungefanya nini wakija wanaomba na kuombeana kazi, ungejifanya huwajui? Sijui kama Kikwete atapokea tena favor ya mtu uchaguzi wa 2010. Labda 2011 Rais Kikwete hatakuwa mfukoni mwa kina Rostam na CCM financiers wengine.

Naona pia Salva kamtukana Johnson Mwambo kwamba ni "ki-mbwa cha J.U." akimaanisha Jenerali Ulimwengu, maana Ulimwengu ndie kibosile pale Raia Mwema. Salva Rweyemamu mwana haramu, kama ni barua yake hii.

Dilungaaa
........Unakumbuka Kagoda?
 
Tatizo ni kuwa tayari tumeshaona ngoma zikipigwa (Mzee Malecela) kuwa JK aendelee kwa miaka mingine 5 tena bila kupingwa.

Kwa alivyoboronga, sidhani kama anastahili hata zaidi ya wiki moja, ila cha kushangaza ni kuwa hakuna mbunge hata mmoja anayezungumzia kumfukuza JK kwa kushindwa kazi, ingawa kikatiba uwezo huo wanao. Hata wale wa upinzani wako kimya kulizungumzia hilo. ..........Why??[/QUOTE]


Hujui kwa nini!! hebu kumbuka JK alivyoenda kulihutubia bunge alichoonge kilikuwa nini?; wengi tulidhani kuwa patakuwa hapatoshi kwamba Rais wa nchi anakwenda kulihutubia bunge. Lakini cha ajabu akaishia kuwaeleza kuwa serikali yake imewaboreshea mafao kwa kuongeza bajeti ya wabunge maradufu. Si umesikia walivyomuwakia Dr. Slaa pale aliposema kuwa wabunge wanalipwa mishahara mikubwa, hivyo inapaswa ipunguzwe. Nani atampinga JK?
 
Currently Active Users Viewing This Thread: 111 (70 members and 41 guests)
================================================
Baba_Enock, Arnold, bantuman, BATA, BINTI SAYUNI, Bluray, Chada, chakubanga, COMRADE44, dgeouff, Dilunga, DMussa, DoubleOSeven, Faraja77, fungamesa, globarch, Great Thinker, gulwa, Halisi, Harenga, Huduma, Hussein Njovu, Ikena, Ilulu, kadushik, Kaka Mdogo, kananyayo, Kibunango, kicheruka, Kijakazi, kinyambiss, Machiavelli, Magezi, Makaayamawe, masikini, Mburahati, MC, MiratKad, MkamaP, Mkora, Mpita Njia, mtuporimtupori, mujuni2, mwana siasa, MwanaHabari, Mwanjelwa, mzeeba, Ncha, ngambo ngali, Nsololi, NTIRU, nyauba, Poetik Justice, Renegade, REOLASTON, rolemodel, Shakazulu, Skills4Ever, Tajiri Mtoto, TooGood, Tristan, Tuandamane, tzengo, urassa, Waberoya, Wakuja, Wambandwa, Yo Yo, Zanaki
=================================
 
Nakumbuka Mkapa aliwahi tumia mbinu hiyo hiyo ya kuwajaza waheshimiwa pale Bungeni na katika kuhalalisha hilo alidai kwamba anaboresha ya wabunge kwanza kisha wafanyakazi kwa sababu wao ndio wanaopitisha mishahara ya wafanyakazi.

Hadi leo wafanyakazi wamebaki na kilio cha kifaranga kinapomuomba mama nyonyo naye humwahidi kwa kumwambia KESHO! JK naye anafuata nyayo, wabunge wetu hawawezi mwajibisha Rais kwa sababu wako pale kwa maslahi yao na si wanaowawakilisha.
 
Mimi sijaisoma kwa sababu haifunguki, lakini kwa jinsi nilivyofuatilia michango mbalimbali ya wachangiaji wakiwemo ninaowaheshimu sana, hali ni mbaya zaidi kuliko tunavyoiona katika bandiko hilo.

Kama unataka kuamini angalia jinsi serikali inavyopambana na kutisha wa juu ya kuvuja kwa "nyaraka za siri" hii nayo inaweza kuwa moja wapo ya hizo "nyaraka za siri", sijui.

Wataficha sana lakini atakuja kichaa mmoja ambaye atazianika hizo "siri" zao, siwamesema eti nyingine zinachukua miaka 20 kuharibiwa n.k, wajifunze kutoka kwa Obama na jinsi anavyowaanika walioficha uovu wao kwa kutoa memos zao.

Swali, je Tanzania tutafika huko lini? namanisha tutampata Obama wetu kabla ya miaka 20 kupita wasije ziharibu? kama kweli wanafuata huo utaratibu. Manake nimekuwa nikisikia mara file imepotea mahakamani, file imepotea Brela n.k, au ndo zinavyoondolewa/zitavyoondolewa kutoka mfumo rasmi wa kuziona.

Mungu atusaidie watanzania tuamke kutoka katika usingizi huu.

Heshima mbele Enigma
 
Baada ya habari hebu tupeni mlichokifahamu au mlichokiona na kinachoendelea au hii story inahusiana na nini haswa ili nasi tuingie mitaani kupakazia ndio mambo yanavyokwenda kuliko wengine kuonekana kupiga vigeregere kumbe awajafaamu kitu. kama kuna mtu anaweza kuweka muhtasari wa habari yote ,najua wengi mmekwenda shule na kuweza kufupisha kisa kizima kikaonekana kama unatotoa Hadithi ya paukwa pakawa.
 
huku sasa sijui tunakwenda wapi! kama ni kuumbuana sasa ndio tumefikia patamu kweli kweli! He he he he eeeeeeeeeeeee
 
Mimi sijaisoma kwa sababu haifunguki, lakini kwa jinsi nilivyofuatilia michango mbalimbali ya wachangiaji wakiwemo ninaowaheshimu sana, hali ni mbaya zaidi kuliko tunavyoiona katika bandiko hilo.

Kama unataka kuamini angalia jinsi serikali inavyopambana na kutisha wa juu ya kuvuja kwa "nyaraka za siri" hii nayo inaweza kuwa moja wapo ya hizo "nyaraka za siri", sijui.

Wataficha sana lakini atakuja kichaa mmoja ambaye atazianika hizo "siri" zao, siwamesema eti nyingine zinachukua miaka 20 kuharibiwa n.k, wajifunze kutoka kwa Obama na jinsi anavyowaanika walioficha uovu wao kwa kutoa memos zao.

Swali, je Tanzania tutafika huko lini? namanisha tutampata Obama wetu kabla ya miaka 20 kupita wasije ziharibu? kama kweli wanafuata huo utaratibu. Manake nimekuwa nikisikia mara file imepotea mahakamani, file imepotea Brela n.k, au ndo zinavyoondolewa/zitavyoondolewa kutoka mfumo rasmi wa kuziona.

Mungu atusaidie watanzania tuamke kutoka katika usingizi huu.

Heshima mbele Enigma

Mkuu,
You really need to read the document maana its more than "kuvuja siri za serikali " -
Hii kwanza siyo siri ya serikali bali ni siri ya watu wawili kuonesha ni kwa vipi serikali inapata mamluki through urafiki - mtindo wa nikune nami nikukune.
Pia inaonyesha kuwa kuna watu very poweful nje ya serikali lakini wenye nguvu kama au kuliko serikali.Hawa wanatisha maana ndiyo vinara wa ku steer mambo mengi yanayoiyumbisha serikali na kuwafanya wananchi kuishia na hali duni.
 
Hivi tuna uhakika gani kama ni kweli ni Salva ndie kaandika yote hayo?

Uyasemayo ni kweli, lakini ukisoma mtiririko na facts, kuna ukweli wa zaidi ya asilimia 75. Sehemu kubwa ya yaliyoandikwa ni ya kweli tupu kulingana na data zilizopo. Na pia kwa michango ya wengi humu inatupeleka huko. Tusubiri hiyo 15% kama itatupa data za kinyume nyume, maana huenda Ikulu wakatoa taarifa, maana na wao wana mambo mengi mazito ya kuyatolea maelezo.

Jambo la pili, naweza kuona pia kwamba huenda hii thread ikamuokoa Salva maana kuna mahali humu kulikua na tetesi za hatima yake Ikulu, kwa hiyo kama kulikua na sababu tofauti ya kumuondoa ama kama alimaliza mkataba (kama upo) basi huenda mambo yakasimama kusubiri huu 'moto wa JF' upoe.
 
Back
Top Bottom