Pole mkuu kumbe ni muathirika wa PMNimejifunza na sitorudia tena...!!!!
Nasema sitokaa nirudie huu upuuzi tena....!!!!
Hahahahahaa sawa mkuu nimekupata tunayemuongelea hapa ni 'valentina'
Kama kutembea tu umeshindwa utaweza kulala kwenye ngozi ya ng'ombe kweli au tunadanganyana?
Sio kweli ......!!!!!!!
Hahahahaaha mke wa mtu huyooo
Mapenzi yaanziayo humu kizungumkuti mtupu!
Mmekutana kwa majina feki ndani ya msitu msitegemee la maana sana, japo kuna mapekee ya hapa na pale.
We waweza kudhani huyo uliyempata ndo wako pekee kumbe huko kwenye maPM ni wa wengi.
Waweza dhani (unajua) kuwa ana anatumia jina moja kumbe wapi, hola!
Ana mijina lukuki na kila jina lina bebi na la'aziz wake.
Sisemi hakuna wakweli lakini kujua kama ni wakweli ndo kazi.
Nimejikuta nacheka sana
Asante sana mkuu kwa kunifurahisha jioni hii!
Ni kweli kabisa
Kama unaingia kwenye mahusiano ni bora ukawa makini ili kuepuka matatizo yasiyohitajika
Ukijidai wewe ni wa kumuamini kila mmoja itakuja kula kwako
Hii mambo ya ID kibao nayo ni tatizo lingine!
Ukweli si huo nimeusema kwani kuna ukweli gani tena?Siuseme tu ukweli jmn!
Jmambo lingime ni kuwa unaweza kuvutiwa na mtu hapa na ukaanza kujenga kwenye fikra zako jambo ambalo litakufanya uwe na matarajio fulani kwako.Unaweza kudhani labda mtu huyo ana elimu fulani,kazi fulani au uwezo wa kifedha wa aina fulani kumbe ni mtu wa kawaida sana na kiwango chake chake cha elimu na kipato ni karibu na kile cha chini kabisa na unapenda kukutana nae unaanza kujilaumu au kukata mawasiliano nae kisa umemuona sio kama vile ulivyokuwa unadhania
!
Halafu sasa watu kwa kujifanya wajuaji huko kwenye maPM.
Jitu halikujui lakini linajifanya linakujua utadhani lilikuzaa.
Sasa likifuma mjinga mjinga ndo kabisaa...litamjaza ujinga weee na yeye ataumeza tu kama peremende.
Anyway, ni heri mijitu ijifanye inakujua ilhali haikujui kuliko kukujua kidogo na kupata chanzo cha uzabinazabina na uhasidi.