Firm sues Government on mining contracts

Ndugu Wana Jamii Forum,

Nawashukuru wote na nitakaribisha michango ili kuweza kuendesha kesi hii. Shida kubwa iko katika kutoa vivuli vya nyaraka nyingi ambazo tutatakiwa kuzitoa mahakamani pamoja na gharama za mawakili wenzangu ambao wamekubali kushirikiana nami katika kuendesha kesi hii.

Nawashukuru sana na tuzidi kusaidiana kuiokoa nchi yetu.

Asanteni

Rugemeleza Nshala

Tanzania ni yetu sisi na wajukuu wa wajukuu wa vitukuu vyetu. Tusipoilinda leo, hivyo vizazi havitairithi nchi. Hongera sana kwa ujasiri na uzalendo mkubwa. Tupo pamoja na tutasaidiana kwa hali na mali katika hili!

Roboti anaweza kutuandalia njia nzuri ya kuanza kubipiana katika hili! Shukrani.
 
Kuhusu nyaraka hizi zitakuwa nyingi kwani tunataka kuwasilisha machapisho mbalimbali yanayoonyesha jinsi uchimbaji ulivyosababisha raslimali madini kuchimbwa bila manufaa kwa Taifa.

Hizi ni pamoja na ripoti za serikali yenyewe pamoja na machapisho ya wasomi wa ndani na nje ya nchi. Ni dai letu kuwa Ibara ya 9, 27 na 28 za Katiba ya Nchi yetu zimekiukwa na kuwa mfumo wa sasa umesababisha kuporwa kwa madini yetu wakati ibara hizo zinadai kuwa raslimali za nchi zitumiwe kwa namna inayowanufaisha na kuwafaidi Watanzania.

Rugemeleza
Rugemeleza,

Worry not, mkiwa tayari tufahamishe... kwa niaba ya wana JF tutahakikisha kila kitu kinaenda sawa kuhusiana na nyaraka hizo, tena tutawaongezea za ziada ambazo najua ukiziona hutoamini zipo mikononi mwa watanzania siku nyingi.

Contact us - info@jamiiforums.com and we will (on behalf of our clients) do our best
 
Mkuu kwanza shukrani zangu za dhati kwa kuweza kufanya kile ambacho wengi wetu tumekuwa tukiombea kifanyike. Tuko wote kwa hali na mali katika hili.

Ingependeza pia kama inawezekana ungeifungulia mashtaka serikali ya jamhuri ya muungano ya Tanzania kwa matumizi mabaya sana ya kodi zetu. Mimi kile kitendo cha kuona fedha zetu zinatumika kununua Land Cruiser Series 200 kwa matumizi ya watumishi wake kinauma sana.

Yaani Tanzania hii asilimia kubwa ya magari yote mapya, mazuri na ya bei mbaya ni ya serikali. Hili haliingii akilini
 
Huyu ni mmoja ya watanzania wachache including hawa....Marehemu Ndyanabo, Lissu, Mrema, Mtikila, na Dr Slaa ambao wako tayari kupigania maslahi ya watanzania!
Unaweza ongeza orodha yako.........
Big up!
Mungu akuongezee miaka 200 mingine uone matunda ya kazi yako!
 
,

Ndugu zangu,

Nafurahi kuwa lile nililolisema siku nyingi kuwa hatuna Wawekezaji bali wachukuaji sasa limeanza kukubalika kwani makala hii ya Jenerali Ulimwengu inajieleza yenyewe. Ninawasihi tuache kutumia neno wawekezaji na tuseme bila kumung'unya kuwa wote hawa ni "Wachukuaji." Ninashauri watu wavinjari na kuitalii tovuti ya Raia Mwema la leohttp://www.raiamwema.co.tz.
Rugemeleza

:confused::confused:

lC.gif
Jenerali Ulimwengu​
Disemba 2, 2009
rC.jpg

KWAMBA sekta muhimu kama kilimo inaweza kusahaulika, watawala wakaiweka kando, na bado wakaendelea kuwa watawala, ni jambo linaloendana na mantiki ya jumla ya mahusiano kati ya watawala na watawaliwa na pia mahusiano kati ya nchi zetu na maslahi ya wakubwa wa uchumi wa dunia. Nitaeleza.
Kwa muda mrefu sasa, nchi zetu zimekuwa zikielekezwa nini zifanye ili zipate maendeleo ya kiuchumi. Tanzania, ambayo kwa kipindi fulani huko nyuma iliwahi kufurukuta ikitafuta njia ya kuleta maendeleo bila kulazimika kufuata maagizo ya wakubwa hao, sasa imekuwa msitari wa mbele katika kukubali kila agizo tunaloletewa kutoka Washington na London.
Ule uhuru kidogo wa kufikiri tuliokuwa tumeujenga, hata kama ulikuwa bado haujakomaa vilivyo, sasa haupo tena. Tumeruhusu asasi za nje zifikiri kwa niaba yetu, kisha zituletee maelekezo nasi tuyatekeleze. Kwa jinsi hii uwezo wetu wa kufikiri umevizwa, na tumekubali kuhasiwa kisaikolojia kiasi kwamba hatuamini uwezo wetu wa kufikiri wala kutenda.
Kwa njia ya kusikitisha sana, watu weupe, ambao si zamani sana tuliwaona kama watu wa kawaida na wenye akili sawa na zetu, sasa tunawaona kama miungu. Nilikwisha kueleza katika makala zangu za nyuma jinsi vitoto vidogo, ambavyo vinaonekana kama vinahitaji kuwa shuleni bado, vilivyoketi katika ofisi zetu muhimu vikiitwa “washauri wa kiufundi,” vikiwashauri mawaziri wetu na makatibu wakuu wao. Tumehasiwa kisaikolojia, na baada ya hapo kila kitu kinakuwa rahisi kwa ye yote anayetaka kututawala.
Kuhasiwa huko kumetufanya tufike hatua ya kushindwa kutambua kilicho na thamani nchini mwetu, tukianzia na watu wetu, ambao ndiyo hazina kubwa kuliko zote: watu wanaoweza kufikiri, kupanga na kutenda, alimradi wapewe mwanya wa kufanya hivyo. Badala ya kubuni njia za kuimarisha mawasiliano baina ya watawala na watu wao ili kuchakata fikra za kitaifa kwa lengo la kupata mwafaka kuhusu masuala muhimu yanayohusu mustakabali wa nchi yetu, sasa imekuwa rahisi zaidi kwa watawala wetu kupokea maagizo kutoka nje na kuwalazimisha wananchi wayatekeleze.
Hili ninalolisema si jipya, sote tunalijua, na wala si la hapa kwetu pekee, kwani nchi takriban zote za Kiafrika zimeingizwa katika utaratibu huo. Katika mijadala na mihadhara mingi katika ujana wa rika langu tulijadili sana masuala yanayohusu ukoloni mamboleo na ubeberu. Wakati ule mijadala ile ilikuwa ni ya kinadharia zaidi; sasa ndiyo tunaona ile nadharia ndani ya matendo halisi. Tumegubikwa na ukoloni mamboleo.
Kama kawaida, mtu aliye na nia ya kukutawala huanzia kwa kukuteka akili, na akiisha kuiteka akili yako kila anachotaka umfanyie utamfanyia, tena kwa moyo mkunjufu. Kama anachotaka ni rasilimali zako, utazitoa, tena kwa hiari, na kisha utakwenda kwake kuomba akupe misaada. Kwa jinsi hii utampa dhahabu yako yenye thamani ya mabilioni ya dola za Kimarekani naye atakupa “msaada” wenye thamani ya shilingi milioni chache tu, nawe utaridhika na kushangilia na kutangaza kwa fahari.
Baadhi yetu tunakumbuka jinsi serikali yetu ilivyotangaza kwa furaha kubwa taarifa kwamba tumekubaliwa kuwa miongoni mwa HIPC, au kwa Kiswahili kisicho rasmi, Nchi Masikini za Kutupwa zenye Madeni Makubwa. Eti tunashangilia sifa kama hiyo, na serikali yetu inajiona imefanya kazi kubwa!
Yote haya yanahusiana vipi na jinsi tunavyoendesha utawala wetu? Uhusiano mkubwa hapa ni kwamba wananchi wetu hawana mamlaka yo yote juu ya maisha yao na juu ya rasilimali zao. Hili nalo si jipya, na wala si la nchi yetu pekee; ni ukweli usipingika katika nchi nyingi za Kiafrika.
Maamuzi ya kiutawala na ya kiuchumi yanafanyika katika miji mikuu, hata pale maamuzi hayo yanapohusu maisha ya watu walio kilomita elfu na zaidi kutoka miji hiyo. Mara nyingi maamuzi hayo hutokana na shinikizo la wakubwa niliowataja hapo mapema, ambao wana maslahi yao mahsusi, ambayo karibu mara zote yanakinzana na maslahi ya watu wetu.
Aidha, mara nyingi wanaofanya maamuzi hayo yanayopora rasilimali za nchi watarubuniwa kwa kupewa “kitu kidogo”, fedha, gari au karo ya mtoto. Lakini si lazima, kwa sababu watawala waliokwisha kutekwa akili na “wazungu” watafanya wanavyoagizwa kwa sababu utaahira waliopandikizwa nao unawafanya waamini kwamba asemacho “mzungu” ndicho sahihi.
Kadri maamuzi yanavyozidi kufanywa katika miji mikuu bila kuwahusisha wananchi wa maeneo yanayoathiriwa na maamuzi hayo ndivyo maslahi ya nchi yanavyozidi kuhujumiwa na watawala wenye ajenda za hovyo. Kimsingi watawala hawana sababu ya kuumiza vichwa vyao wakihangaika na matatizo yanayoelekea yatachukua muda mrefu mno kupata utatuzi. Nitaeleza.
Ni kwa nini mkuu wa nchi anadiriki “kusahau” kilimo. Kilimo ni kazi ngumu, hasa kama mtawala anataka kuwaongoza watu wake waondokane na kilimo duni cha jembe la mkono na walime kwa mbinu na nyenzo za kisasa.
Shughuli yake ni nzito. Itabidi aweke mifumo ya elimu ya kilimo cha kisasa; aandae pembejeo zilizo bora; awe na viwanda vya kutengeneza zana za kilimo za kisasa; aweke mtandao wa huduma za ugani; ahakikishe pambejeo zinafika zinakohitajiwa kwa muda mwafaka; apambane na hali ya hewa inayobadilika kila mara; akae chonjo dhidi ya magonjwa na wadudu waharibifu, ahakikishe mazao ya wakulima wake yana soko lenye tija, na kadhalika. Ni mambo mengi, na baadhi yake hayatabiriki.
Taabu yote ya nini kwa mtawala anayetaka kula raha na kufurahia neema ya ukubwa? Inakuwa ni rahisi zaidi kwake kukaribisha “wawekezaji” kutoka nje, kuwasabilia migodi yenye thamani kubwa, kuwaruhusu wachimbe wanavyotaka na wakadirie wenyewe ni kiasi gani watakulipa kama pango, na siku akitindikiwa anaweza kuziendea serikali zao kuomba “msaada” wa chakula kwa sababu watu wake wana njaa kutokana na kwamba mwaka uliopita hakusimamia kilimo kwa sababu alizidiwa na shughuli ya kutia saini mikataba ya uchimbaji. Kama huo si ujuha niambie ni nini.
Tumefikia mahali pabaya, hivyo kwamba sasa wageni wanaweza kuingia nchini mwetu na kuzungumza na watawala wawili au watatu jijini Dar es Salaam na kisha wakamegewa kipande cha ardhi ya watu bila wahusika kushiriki, na kisha tukaambiwa kwamba hao waachwe kwani ni wageni ‘spesheli”. Kuna mtu anataka kuchokoza vita, lakini ukimwambia atakwambia wewe ndiye mchokozi.
Labda ni muhimu kuwakumbusha watawala wetu yale baadhi yetu tuliyomwambia Benjamin Mkapa akiwa Rais. Kilimo ni shughuli nzito iliyojaa ngwamba na suluba. Inahenyesha, inachosha, na wakati mwingine ni tombola, kwani hujui kama utapata ama utakosa. Lakini ndiyo shughuli ya watu wako kwa kiwango cha asilimia 80. Huwezi “ukaisahau,” na kukimbilia kwenye madini.
Sekta ya madini haina “wawekezaji” bali ina “wachukuaji.”
Njia moja thabiti ya kuhakikisha kwamba watawala “hawasahau” sekta muhimu kama kilimo na maeneo mengine yanayobeba maslahi makuu ya wananchi ni kuondokana na utaratibu unaotoa madaraka ya maamuzi yote makubwa na muhimu mikononi mwa watawala wa serikali kuu, na kuwapa wananchi mamlaka makubwa zaidi katika maamuzi yanayowahusu.
 
Firm sues Government on mining contracts

By Bernard James

A constitutional petition has been filed in the High Court, seeking to have all the mining contracts entered into by the government without Parliament's approval declared null and avoid, in an effort to curb the plunder of the country's natural resources.

A Dar es Salaam-based environmental and human rights activist, Mr Rugemeleza Nshala, and a company called Mtetezi Limited, have sued the minister for Energy and Minerals and the Attorney General.

They want the court to immediately stop the operations of the holders of special mining licences and mining companies that have signed Mining Development Agreements (MDAs) with the government "because their activities are unconstitutional".

The petitioners claim that the powers conferred on the minister for Energy and Minerals to sign MDAs are unconstitutional, as they interfere with the duties of other ministries, councils, agencies and departments.

The petitioners are challenging the Mining Act No 5 of 1998 that gives the minister powers to sign MDAs on behalf of the government.

They now want the court to declare that all the MDAs signed with the holders of the special mining licences, which were not approved by Parliament in line with the mandatory requirements of articles 63 (3) (a-e) of the Constitution, be scrapped.

The article gives the National Assembly powers to deliberate on and ratify all treaties and agreements to which the United Republic of Tanzania is a party, and lists provisions, which require ratification. It also empowers Parliament to put any questions to any minister concerning public affairs.

The petitioners are accusing the energy minister of granting mining concessions to foreign mining companies of unlawfully, and allocating large areas that were initially owned by villagers and artisanal miners to foreign firms.

They assert that the allocations are responsible for the forceful displacement of millions of agriculturalists, peasants, pastoralists and artisan miners from their lands, in total disregard of their land and property rights enshrined and protected in the Constitution.

The petitioners want the court to order that all the people displaced to pave the way for large-scale mining be resettled on their land and paid compensation.

"We feel that our country's mineral resources are being squandered, as the current exploitation is only benefiting the foreign mining companies and yet the current mining and its taxation legal regime are not only illegal, but also unconstitutional," they argue.

The petitioners are also arguing that the granting of mining concessions to foreign companies through local affiliates under the guise of Section 10 (1) and (2) of the Mining Act No 5 1998, not only grants unconscionable incentives to those firms, but also purports to supplant the laws of the land, and curtail the legislative powers of Parliament.

The section prevents Parliament from passing any law that might in "one way or another interfere with their tax, social and economic obligations that they found at the time they came to invest in the country".

The petitioners argue that "the curtailment of the parliamentary powers is not only wantonly violates Article 13, which calls for equal treatment under the law, but also the entire democratic framework enshrined in the Constitution."

Article 63 (3) (a) to (e) grant Parliament powers to oversee, monitor and supervise the workings and operations of the government, including the ratification of all agreements signed in the name of the United Republic of Tanzania.

"Yet the respondents have never presented any Mining Development Agreement (MDAs) signed with foreign mining companies to Parliament for deliberation, review, ratification or rejection."

The petitioners are also accusing the government of granting "generous and unwise incentives", including tax-holidays, tax exemptions, "unlimited immigration quotas for their so-called experts", and the fuel levy, all of which, they claim, have led to the plunder the country's mineral resources.

To back up their petition, the petitioners are citing the tax-free sale of several mining companies.

These include Lusu gold mine, which was sold by Samax Resources of Canada to Ashanti Goldfield in 1998, at $213 million, the Bulyanhulu gold mine disposed of by Sutton Resources of Canada to Barrick Gold, at $348 million in 1999, and Nyabigena and Nyabirama mines in Tarime district that were sold by East Africa Gold Mine to the Placer Dome at $252 million.

During the hearing, the petitioners say they w HILI JAMBO JEMA LIMEFIKIA WAPI?
 
Back
Top Bottom