Seran
JF-Expert Member
- Feb 7, 2025
- 12,110
- 35,914
Habari wana jukwaa,
Hii iwafikie wanaojua sheria za Tanroads
Naomba kuuliza wajuzi, hivi ikitokea kuna mradi wa ujenzi barabara njia imekuwa diverted na wewe ni mgeni eneo hilo kwa bahati mbaya ukapita ila ukashtuka haiko sawa ukaona ugeuze.
Unafika mbele kidogo kuna mtu katufata chap kwa haraka na boda nyuma anatusimamisha anadai twende tanroad tukalipe fine ya tsh 1,800,000/- tumeomba msamaha sana na kumwambia mmoja wetu ni mgonjwa kaja tu hospitali na hatukujua, hiyo pesa hatuna labda tusaidiane tu, haelewi huyu mtu, anauliza tumepungukiwa shingapi atusaidie! baadaye tukaanza kupiga simu kwa tunaowajua ili tufanyiwe wepesi tuendelee na safari zetu ndio akasema katusamehe tuendelee na safari!
Kwahiyo nataka kujua ni kosa kisheria kupita eneo lililozuiliwa kupita maana yake ni kuingilia mradi, na umeingilia huo mradi kivipi? Na kama unapaswa kulipa fine, hiyo fine ni shingapi?
Hii iwafikie wanaojua sheria za Tanroads
Naomba kuuliza wajuzi, hivi ikitokea kuna mradi wa ujenzi barabara njia imekuwa diverted na wewe ni mgeni eneo hilo kwa bahati mbaya ukapita ila ukashtuka haiko sawa ukaona ugeuze.
Unafika mbele kidogo kuna mtu katufata chap kwa haraka na boda nyuma anatusimamisha anadai twende tanroad tukalipe fine ya tsh 1,800,000/- tumeomba msamaha sana na kumwambia mmoja wetu ni mgonjwa kaja tu hospitali na hatukujua, hiyo pesa hatuna labda tusaidiane tu, haelewi huyu mtu, anauliza tumepungukiwa shingapi atusaidie! baadaye tukaanza kupiga simu kwa tunaowajua ili tufanyiwe wepesi tuendelee na safari zetu ndio akasema katusamehe tuendelee na safari!
Kwahiyo nataka kujua ni kosa kisheria kupita eneo lililozuiliwa kupita maana yake ni kuingilia mradi, na umeingilia huo mradi kivipi? Na kama unapaswa kulipa fine, hiyo fine ni shingapi?