FIFA Confederations Cup Brazil 2013

FIFA Confederations Cup Brazil 2013

Tahiti ni bingwa wa confederation ile yenye timu za Australia New Zealand (Oceanic sijui?!)?
 
hebu wacheki wanasheria wetu tuone uwezekano wa kuhamia oceania

wazanzibar wakiwa wajanja wakijitoa ktk muungano wajiunge huko oceania badala ya caf

Bado Cavani na Suarez nao watashindana kufunga kama Torres na David Villa
 
ukiwa na kumbukumbu nzuri jaribu kufikiri Yugoslavia alifunga mangapi Congo kwenye World cup
 
mechi yao ya mwisho na uruguay watachezea kipigo kikali zaidi,suarez pekee atafunga goli 6!
ciao
 
Mie still ntabaki kuwa wa mwiisho kabisa kuamini kuwa Naima atatamba Ulaya kwa Lavel za Ronaldinho.

Naima nasikia kawachachafya sana mabeki wa Mexico...
Hongera zake sana.
Jaribio lake la kwanza ni siku watakapocheza na ngoma ngumu za Buluda zikiongozwa na Golikipa bora Duniani Gianluigi Gigi Buffon.
So hapo ndo tutatofautisha kati ya Tende na Mende.

mkuu sijasema kuwa atafikia level za Gaucho ila si mchezaji wa kubeza.ni mzuri sana tu.tusimhukumu kwa mechi moja tu ya England.nimemtazama mechi nyingi kuna kitu ananifurahisha,anachezesha forward line,yaani anamiliki half nzima ya uwanja.ana kasi,hana mambo mengi,ana pasi deadly!kwa timu yenye watu kama Messi,ni hatari tupu.sijajua tu kuwa atapangwaje pale barca manake free role tayari yupo Messi pale.Neymar anaweza kupata shida kwa Italia lakini haina maana ndio mwisho wa uzuri wake.Italia inaeleweka dunia nzima huyo Messi mwenyewe alikutana na Inter akapoa,huyo Bebeto na Romario walikutana na akina Baresi wakacheza dk 120 kwenye half ya italy bila kupata goli,Zidane alikutana na Ferrara akatulizwa,lakini bado watu hao ni wachezaji bora duniani,so Neymar kufichwa na Barzagli haitamuondolea uzuri wake.wapo mabeki wengi tu ulaya watakalishwa na chenga zake.mie niko positive nae sana na hasa kwa kikosi cha Barca kilivyo.
 
Back
Top Bottom